Baadhi ya vipengele vya mkataba wa Sports pesa na Yanga ,mkataba wa "Ki Mangungo"

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
Sasa naanza kuelewa kwanini Manji ameamua kujiudhuru,sasa nafasi ya quality group au Manji ipo wapi hapo [emoji23] [emoji23]

Sports pesa wametoa 900M hivyo hakuna mdhamini yeyote atakayeruhusiwa na wachezaji pia image zao zimeuzwa

Image na voice za wachezaji 22+ ,nembo ya timu nk nk kwa 900M na hakuna sponsor mwingine atakayekubaliwa





 
Mnahangaika duh [emoji23][emoji23][emoji23] mara mko FIFA hatujatulia mmetufuata Sports Pesa heeee heee huu ushuzi kawadanganye mikia maana ndio timu inayoongoza kwa mashabiki fuata upepo
 
Kuhusu image rights hiyo ni kawaida main sponsor anakua na rights ya kumtumia mchezaji au nembo ya timu kwenye matangazo yake.
Ila kuhusu kuzuia sponsors wengine sidhani na wala sijawai kusikia sehemu yoyote. Kama kweli wameingia mkataba unaoizuia Yanga kusaini na Sponsor mwingine tofauti na betting company itakua ni jambo la kushangaza.
 
Mkuu! Mbona unapotosha watu?

Leta mkataba genuine na sio hiki kipande kilicho fanyiwa editing kutoka Kwenye mkataba ule wa Manji.

Msiangaike Sana jamani! Mkataba nimeusoma na hakuna vipengele vya namna hiyo.

Nimeshangaa sana kuona mkataba wa namna hiyo.
 
Hivi hilo neno nyanya lipo kwel kwenye huo mkataba jaman?
 
Hakuna mkataba wa namna hiyo!

Aliyefanya editing amechukua baadhi ya vipengele vya mkataba uliokiwa usainiwe baina ya Yanga na QG.

Kwahiyo QF walitaka kuifunga Yanga wasiweze kuingia mikataba na makampuni mengine?
 
Mkuu! Mbona unapotosha watu?

Leta mkataba genuine na sio hiki kipande kilicho fanyiwa editing kutoka Kwenye mkataba ule wa Manji.

Msiangaike Sana jamani! Mkataba nimeusoma na hakuna vipengele vya namna hiyo.
Hayo ndo mambo mkuu. Watu hawasomi original bali wanaedit na kuleta thread za uongo.
 
We jamaa..muongo.huoni hata aibu,kwanz maana ya udhini ndo nin?
 
Hayo ndo mambo mkuu. Watu hawasomi original bali wanaedit na kuleta thread za uongo.
Nashangaa kuona shabiki wa Simba anaandika suala kama hili kwa namna ya kama kukashifu upande wa pili...


Ninaamini kuwa hata kama Yanga wangekuwa wamesaini mkataba wa vipengele vya namna hii, basi bila shaka na huko Simba kungekuwa na vipengele vya namna hii.
Wasingekuwa na uwezo wa kupinga vipengele vya namna hii, kama tu walishindwa kufanya bargaining ili wapate mkwanja mrefu wa sportpesa kama wenzao Yanga walivyo kuwa na guts hiyo.
 
Kwahiyo QF walitaka kuifunga Yanga wasiweze kuingia mikataba na makampuni mengine?
Hapana! Kwenye ule mkataba QG ndio waliotaka kujipa mamlaka ya wao kuingia mkataba na wadhamini wengine, na isiwe Yanga ambayo inayoingia mikataba na wadhamini wengine..

Yaani wao ndio wasimamie mikataba yote klabu inayotaka kuingia.
 
Mkuu! Mbona unapotosha watu?

Leta mkataba genuine na sio hiki kipande kilicho fanyiwa editing kutoka Kwenye mkataba ule wa Manji.

Msiangaike Sana jamani! Mkataba nimeusoma na hakuna vipengele vya namna hiyo.
Eti mkataba tena kwa timu kubwa unasema MARUFUKU, dah!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…