Uchaguzi 2020 Baadhi ya wagombea washauriwe kusitisha kampeni, hawana jipya

Uchaguzi 2020 Baadhi ya wagombea washauriwe kusitisha kampeni, hawana jipya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

Palikuwa na haja ya kuwashauri baadhi ya wagombea kusitisha tu kampeni zao hasa hasa kampeni zenyewe zinapokuwa za gharama kubwa, zisizokuwa na tija na huku zikiwa hazina jipya kabisa.

Kwa mfano, wengine tangia kuzinduliwa kwa kampeni mwishoni mwa August ile mbele ya macamera lukuki ya TV stations zote zilizopo nchini, hamna jipya lolote waliosema bali ni yale yale ya kabla hata ya uzinduzi.

Jamani eeh tufanye tumesikia basi!

Maana tumenunua madege, tunajenga meli maziwani, tumejenga mahospitali na dispensaries kadhaa, tunajenga SGR, Stiggler's Gorge, nk nk. Habari ni hiyo hiyo kote wanakokwenda utadhani ni recorded CD inachezwa.

Ukizingatia kuna huyu anayeambatana na magari si ya kitoto zaidi 100 na watu wasiopungua 400 kwenye misafara yake. Huu ni upotezaji wa raslimali usio na tija kwa ajili ya kwenda kusema yale yale?!

Kwa kweli hawana jipya na hii hadithi wanayoirudia rudia kwa hakika imechokwa na imedoda vilivyo.

Kwamba tuliamua kupumzika hizi siku mbili tatu? Bora tungepumzika jumla tu. Hizi kampeni hazina tija wala manufaa hata kulinganisha na juhudi tu.

Bora kama tungekuwa na mapya labda kuhusiana na mipango kuelekea kuangazia haki au uhuru wetu. Haya mengine mbona mgombea huyu yamemletea tafrani zaidi kuliko umaarufu?

Habari ndiyo hiyo.
 
Sasa nani mwenye jipya kila mmoja yale yale risasi 16 uhuru wa mara 2 na mengine hayohayo unadhani kutakua na mapya labda litokee yukio jipya ndo mapya yataibuka
 
Kwakweli alie karibu na Magufuli amshauri jamaa, hana mvuto kabisaaa
Ushindi wa Magufuli utaletwa na jiji la Dsm. Hili jiji naona ccm wamelishika vilivyo, kila chaka na kila chocho unayokatiza unakutana na lipicha la Magufuli yaani kama vile hakuna wagombea wengine wa nafasi ya urais.

To my suprise tapeli mashuhuri bwana Gwajima amebandika hadi mabasi yake ya kusomba misukule wake mipicha picha ya kwake na ya msukuma mwenzake.
 
Sasa nani mwenye jipya kila mmoja yale yale risasi 16 uhuru wa mara 2 na mengine hayohayo unadhani kutakua na mapya labda litokee yukio jipya ndo mapya yataibuka

Mkuu risasi mwilini mwa nguruwe ni sawa Ila kwa binadamu labda kama ni msukule.

Kumwona tu aliyepitishwa kwenye dhahama hilo na wanaojifanya watakatifu na wanyenyekevu kuliko kondoo wanaoendelea kudunda huru mitaani ilikuwa Sunna tosha.

Huyu mfufuka fanya kusikiliza hotuba zake. Kila siku ni darasa jipya.

Waulize kina Maalim, Hussein, Shein, Samia, Majaliwa na hata jiwe.
 
Bora ya Uhuru na Haki. Kuna mapya yanazungumziwa.

Hii ya SGR, elimu bure, meli, Barabara, zahanati... Miaka 5 tu nasikia same things.

Hii wanaita "too monotonous" ndiyo sababu ya kukosa mvuto. Hana jipya kabisa. Pia "known information is no news any more!"

Ongezea pia kwa maelekezo ya bwana yule hata media access anabaniwa vilivyo.
 
Nilifikiri unashauri waache kampeni kwa sababu ya corona ila naona corona imetulia inaheshimu kampeni au pengine bora watu wafe tu maana kampeni ni muhimu sana kuliko uhai wa mtu.

Ila tukumbuketu kuwa kama Magufuli angetumia sayansi kukabiliana na corona(kama ambavyo walikuwa wakipiga kelele humu kuwa afanye hivyo) basi sasa hata hizo kampeni tungekuwa tunazisikiliza kwenye majumbani na kusingekuwa na wa kushauriwa kuacha kampeni.
 
Kuna watu walijiaminisha kuwa mgombea wao atakuwa anapunga mkono tu amemaliza, nina mashaka kama bado wanafikiria hivyo hivyo.

Hao watakuwa wachezaji wa ile timu pendwa ya utopolo FC.

Huyu bwana aache kutwambia yaliyosemwa kila leo kwa miaka 5. Atueleze angalau sasa:

1. Wapi Tr 1.5/- yetu.
2. Vipi uhuru wetu.
3. Vipi haki zetu.
4. Vipi maendeleo yetu.

Maendeleo yetu yamekwama kwani nyongeza za mishahara, upandaji madaraja, biashara za watu vyote vimekufa kama si kusimama kabisa.

Ni vizuri akajua tuliomchoka hatuko wachache!
 
Ushindi wa Magufuli utaletwa na jiji la Dsm. Hili jiji naona ccm wamelishika vilivyo, kila chaka na kila chocho unayokatiza unakutana na lipicha la Magufuli yaani kama vile hakuna wagombea wengine wa nafasi ya urais.

To my suprise tapeli mashuhuri bwana Gwajima amebandika hadi mabasi yake ya kusomba misukule wake mipicha picha ya kwake na ya msukuma mwenzake.

Wanaume wa Dar tusiangushane. Kimbunga cha 2015 ni somo tosha. Mambo ni kampeni nyumba kwa nyumba.

Huyu akachunge ng'ombe na farasi wake Chatto. Wala hatalipiziwa visasi kama afanyavyo yeye.
 
Kuna mtu kila siku anatupa story ya kupigwa risasi

Kwani bwana yule hakutaka kumwua?

Kwani bwana yule keshaacha sasa kutaka kumwua?

Hivi Mangula ile sumu siku ile high table walikuwapo kina nani?

Kwa Mungu wengi watapigwa mshangao.
 
Ungefanya jambo la maana kama ungemwambia Lissu asitishe kampeni maana iko wazi na hata yeye anajua kuwa hatoshinda. Watanzania bado tuna imani na Magufuli na tutamchagua tena
 
Back
Top Bottom