DOKEZO Baadhi ya wahadhiri UDOM wanaweka mazingira ya rushwa ili kuwaongezea maksi wanafunzi

DOKEZO Baadhi ya wahadhiri UDOM wanaweka mazingira ya rushwa ili kuwaongezea maksi wanafunzi

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Serikali yetu inahimiza suala la haki, inapinga unyonyaji. Lakini hii imekuwa tofauti katika baadhi ya wahadhiri wa baadhi ya kozi za kiswahili mwaka wa tatu (CoED & Co. Of social sciences)katika chuo kikuu cha Dodoma.
  • Kuna wanafunzi hawakufikisha coursework ya somo moja la kiswahili.
  • Walienda kwa mwalimu kuomba alama chache zilizopungua lakini mwalimu alidai hana access kwa sasa.
  • Ajabu mwalimu anamtumia Cr wa kozi hiyo kuchukua pesa kwa wanafunzi ili waongezewe alama.
  • AWamu ya kwanza walitoa 50,000/= na kuongezewa alama zilizopungua kufika 16.
  • Ilipobaki siku mbili kufika siku ya mtihani (UE) dau likapanda hadi 100,000/= hapo waliongezewa hadi alama 20, yaani kama mtu alikuwa na CW ya 10 inakuwa 10+20 =30(total CW)
  • Jambo hili sio sawa. Wanafunzi hatupendi kuwa na carry over mwaka wa tatu ndo maana inapelekea hivyo.
  • Hakuna mtu anapata nguvu ya kulisemea hili kwa sababu maisha ya mwanafunzi yapo kwa mhadhiri.. nitaanzaje kusema je likitokea la kutokea itakuwaje mtoto wa kijijini kidumu na mfagio mimi.
  • Si wahadhiri tu bali wanafunzi wote wanaoshiriki hivyo sio jambo zuri.
 
Back
Top Bottom