KWELI Baadhi ya Watu wenye Mshono (Kidonda cha Upasuaji) huwa wanapata maumivu kipindi cha hali ya hewa ya Mawingu na Mvua

KWELI Baadhi ya Watu wenye Mshono (Kidonda cha Upasuaji) huwa wanapata maumivu kipindi cha hali ya hewa ya Mawingu na Mvua

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Mtaani kumekuwa na maneno mengi sana Juu ya suala la Watu Mshono (Kidonda cha upasuaji) Kuwa wanapata Maumivu Kipindi cha hali ya hewa ya Baridi, Mvua au mawingu, Japo wapo kadhaa ambao walithibitisha kupata maumivu katika vipindi hivyo, Lakini ningependa kufahamu zaidi katika Ngazi ya Utabibu.


tummy-tuck-scar-1184x650 conv.jpeg
 
Tunachokijua
Kovu la upasuaji (mshono) ni alama inayobaki baada ya jeraha la upasuaji kupona. Kovu linaweza kuwa laini au ngumu, jembamba au pana kutegemea ukubwa wa jeraha kabla ya kushonwa, rangi yake hutofautiana kutoka kwenye ngozi ya kawaida. Wataalamu wa afya wanasema uangalizi mzuri wa kovu hili unaweza kusaidia kupunguza ukubwa wak na kulifanya lisionekane sana.

Kumekuwapo watu mbalimbali ambao wamekuwa wakilalamika kupata maumivu kwenye Kovu la upasuaji (mshono) katika mazingira ya baridi na mvua. Hoja hii imekuwa kawaida sana kwa wazazi ambao wamewahi kujifungua kwa njia ya upasuaji.

Upi ukweli kuhusu hoja hii?
JamiiCheck imefuatilia hoja hii katika vyanzo mbalimbali vya Wataalamu wa Afya na kubaini kuwa ni kweli baadhi ya watu wenye makovu ya upasuaji (mshono) hupata maumivu kwenye eneo la mshono wawapo katika mazingira ya baridi. Majukwaa mbalimbali ya Afya yakiwamo Medical News Today, Kituo cha Kutibu Majeraha cha Marekani, Marivale Hand Clinic yanakubaliana kuwa hali ya hewa ya baridi inaweza kusababisha mishipa ya fahamu karibu na mshono kukaza au kuvuta na kupelekea hisia za maumivu sehemu yenye kovu la upasuaji (mshono) au hata jeraha la zamani (kovu).

Medical News Today wanaelezea kwa ujumla wake namna baridi inavyoweza kusababisha maumivu kwenye jeraha lolote la zamani hata kama halikuwa na mshono wala upasuaji. Wachambuzi hawa wa taarifa za Afya wanaeleza kuwa hali ya hewa inaweza kuwa na athari kubwa kwenye maumivu ya mwili, hasa kwa watu walio na majeraha ya zamani au mashono ya upasuaji.
1719125068886-png.3023627

Picha kutokea mtandaoni

Wakifafanua zaidi hoja yao Medical News Today wanasema:

Wakati joto linaposhuka, tishu za mwili huanza kukaza. Hii ni pamoja na ngozi, misuli, na mishipa. Wakati tishu hizi zinakaza, inaweza kuongeza shinikizo kwenye mishipa ya fahamu, ambayo husababisha maumivu. Tishu mbalimbali hukaza kwa viwango tofauti wakati wa baridi. Kwa mfano, tishu za kovu (scar tissue) hukaza kwa kiwango tofauti na tishu za kawaida, na hivyo inaweza kusababisha maumivu zaidi kwenye eneo la jeraha la zamani au mshono wa upasuaji.

Kwa upande wao, Kituo cha Kutibu Majeraha cha Marekani hawatofautiano na Marivale Hand Clinic ambao wote wanafafanua kuwa wanaeleza kuwa hali ya hewa ya baridi inaweza kuwa na athari kubwa kwa mwili wa binadamu, hasa kwa wale walio na majeraha ya zamani au mashono ya upasuaji. Wakielezea zaidi hoja hii sehemu ya maandiko yao wanasema:

Wakati wa baridi, mwili wa binadamu hufanya mabadiliko mbalimbali ili kuhifadhi joto, mabadiliko ambayo yanaweza kusababisha mvutano wa misuli, kukaza kwa viungo, na maumivu kwa wale walio na majeraha ya zamani au mashono ya upasuaji.
1719126691068-png.3023644


picha kutokea mtandaoni
Hivyo, kutokana na vyanzo na ufafanuzi huo kutoka kwa wataalamu wa Afya mbalimbali JamiiCheck inaona kuwa hoja ya baadhi ya watu kulalamika kupata maumivu kwenye mshono au makovu ya zamani ni ya kweli.
Uko sahihi mkuu, kumekuwa na imani ya muda mrefu miongoni mwa watu wengi kuwa kuna uhusiano kati ya hali ya hewa na maumivu ya kidonda cha upasuaji. Watu wengine hudai kupata maumivu zaidi wakati wa hali ya hewa ya baridi, mvua, au mawingu, huku wengine wakisema hawahisi mabadiliko yoyote.

Hata hivyo, hakuna ushahidi wa kisayansi unaothibitisha uhusiano huu moja kwa moja.

Nawasilisha
 
Hiyo ni kweli na huwakuta wale watu waliofanyiwa upasuaji mkubwa mfano upasuaji wa mifupa, uzazi wakati wa kujifungua au upasuaji wa viungo.

Kinachopona ni jeraha la juu ila ndani bado misuli inakuwa bado haijaunga vema na kipindi cha baridi hutokea contractions au mkazo wa misuli ambapo hufanya zile sehemu ambazo bado hazijaungana tena kukaza na hatimae maumivu kwa mbali humpata muhusika.
 
Ni kweli kuna jamaa yangu mmoja ilikuwa tukitoka mishe hasa usiku kuna sehemu kuna uwazi na upepo tukipita tu maumivu humuanza na anaweza akasimama kwa muda na baadae maumivu hupotea.Alifanyiwa upasuaji wa mgongo.Siku hizi yuko fiti.
 
Sio mishono ya tumbo tu, hata vidonda sugu vya sehemu nyingine za mwili hupata maumivu au mikazo katika wakati wa baridi.
 
Hata waliotahiriwa ?.
Hapana, ingekuwa hivyo basi mimi na wewe wote tungekuwa wahanga wa hayo maumivu.

Makovu yatokanayo na upasuaji ndyo huleta maumivu wakati wa baridi, mfano hata watu walio vunjika miguu au mikono na kushonwa, pia huhisi maumivu wakati wa baridi.
 
Hiyo ni kweli na huwakuta wale watu waliofanyiwa upasuaji mkubwa mfano upasuaji wa mifupa, uzazi wakati wa kujifungua au upasuaji wa viungo...
Mkuu umeeleza vyema.

Je, wale ambao tayari wanaishi kwenye mazingira ya baridi wakati wote huwa wanahisi maumivu muda wote ama inakuaje?
 
Back
Top Bottom