DOKEZO Baadhi ya Watumishi Kituo cha Afya Rusumo (Kagera) hawana lugha nzuri na hawatoi huduma nzuri pia kwa Wagonjwa

DOKEZO Baadhi ya Watumishi Kituo cha Afya Rusumo (Kagera) hawana lugha nzuri na hawatoi huduma nzuri pia kwa Wagonjwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
Screenshot_20241230_173435_Chrome.jpg

Wana JF kuna Kero moja ambayo imekuwa ikitutafuna sisi wakazi wa Kijiji cha Mshikamano, Kata ya Rusumo ambayo ni wahudumu wa Kituo cha Afya cha Rusumo kilichopo Wilayani Ngara mkoani Kagera.

Hiki kituo kilijengwa mahususi kwaajili ya kurahisisha huduma za afya kwa wakazi wa kijiji hicho na vingine vya jirani ndiyo maana kilijengwa Rusumo jirani na Boda ya Tanzania na Rwanda.

Cha ajabu ni kwamba baadhi ya Watumishi wa kituo wamekuwa wakilalamikiwa na Wagonjwa kwamba wanawatukana wagonjwa pale wanapohoji baadhi ya mambo ambayo yanaihusu hospitali hiyo, mimi pia nimethibitisha hilo mara kadhaa.

Kibaya zaidi ni kwamba, wale wahudumu wa afya ikifika siku ya Jumapili, huwa hawafanyi kazi wakati kituo wanachofanyia kazi kinaweza kuwa na hadhi ya Hospitali ya Wilaya kutokana na usanifu wa majengo yake na miundombinu iliyowekwa.

Kuna wakati nilipeleka mgonjwa pale akatolewa lugha chafu baada ya kuhoji kuhusu huduma baada ya kuweka muda mrefu bila kuhudumiwa.

Jambo lingine ni kuwa kuna tabia ya uzembe kwa baadhi ya Wahudumu wake kiasi kwamba kuna wakati wanaopeleka wagonjwa hapo huwa wanatamani kuwahamisha kwenda kwenye hospitali zingine.

Wahudumu wenye tabia hizo inadaiwa wameshawahi kuonywa kuhusu huduma mbovu wanazotoa lakini hawasikii maana mtindo huu umekuwa wa kujirudiarudia, ukifika Mapokezi, mhusika wa hapo anaweza kuendelea kuongea na simu hata kama kuna mgonjwa wa dharura, wala hashtuki hata kidogo.

Ipo haja kwa mamlaka kutoa onyo kali kwa wale Watumishi ili huduma za afya zitolewe kwa watu kama inavyokusudiwa sio kutuchezea maana kuna ndugu zetu kadhaa wameumizwa na matendo hayo.

Nategemea kuona mabadiliko kwenye hili kwakweli lasivyo hali itakuwa mbaya...

Screenshot_20241230_173513_Chrome.jpg
 

Attachments

  • Screenshot_20241230_173435_Chrome.jpg
    Screenshot_20241230_173435_Chrome.jpg
    290.5 KB · Views: 6
Wana JF kuna Kero moja ambayo imekuwa ikitutafuna sisi wakazi wa Kijiji cha Mshikamano, Kata ya Rusumo ambayo ni wahudumu wa kituo cha Afya cha Rusumo kilichopo Wilayani Ngara mkoani Kagera.

Hii hospitali ilijengwa mahususi kwaajili ya kurahisisha huduma za afya kwa wakazi wa kijiji cha Mshikamano na vijiji vingine vya jirani ndiyo maana kilijengwa Rusumo jirani na Boda ya Tanzania na Rwanda.

Cha ajabu ni kwamba watumishi wa hiki kituo wamekuwa wakilalamikiwa na wagonjwa kwamba wanatukana wagonjwa pale wanapohoji baadhi ya mambo ambayo yanaihusu hospitali hiyo na mimi nimethibitisha hilo mara kadhaa.

Kibaya zaidi ni kwamba, wale wahudumu wa afya ikifika siku ya jumapili, huwa hawafanyi kazi wakati kituo wanachofanyia kazi kinaweza kuwa na hadhi ya Hospitali ya Wilaya kutokana na usanifu wa majengo yake na miundombinu iliyowekwa kwenye hospitali hii ambayo sisi tunaita kituo cha Afya.

Kuna wakati nilipeleka mgonjwa pale Akatukanwa kwamba "Mjinga nini" baada ya kungojea kwa muda mrefu akahoji kuzorota kwa huduma kwenye hicho cha Afya., hilo moja jingine ni kwamba kuna uzembe uliopitiliza sana kwenye hiki kituo kwa wahudumu wake kiasi kwamba kuna wakati wanaoleta wagonjwa hapa huwa wanatamani kuhamisha wagonja kwenda kwenye hospitali zingine.

Wahudumu wale wa kituo hiki cha Afya wameshawahi kuonywa kuhusu huduma mbovu wanazotoa lakini hawasikii maana mtindo huu umekuwa wa kujirudiarudia maana ukifika Mapokezi, anayekuwa hapo anakuwa anaongea na simu hata kama kuna mgonjwa wa dharula wala hashtuki hata kidogo.

Ipo haja kwa mamlaka kutoa onyo kali kwa wale watumishi ili huduma za afya zitolewe kwa watu kama inavyokusudiwa sio kutuchezea maana kuna ndugu zetu kadhaa wamewahi kupoteza maisha hapa mzaha huu ukiendelea tutapoteza ndugu wengi kwa uzembe wa watu wachache.

Nategemea kuona mabadiliko kwenye hili kwakweli lasivyo hali itakuwa mbaya...

View attachment 3189455


Poleni sana! Naamini wahusika watasuluhisha.

OR TAMISEMI
 
Swali jepesi kituo kina watumishi wangapi? Tukishajua idadi ya watumishi ndio tutoe mchanganuo...manesi wangapi na madaktari wangapi,unaweza kuwa una lawama nyingi kumbe clinician wako chin ya 5 pekee kituo kizima tena wanafanya na upasuaji wa kina mama na watoto licha ya uhaba wao na manesi pia wodi zote hata 10 hawafiki na hio ni health center ikimaanisha inafanya kazi 24/7 ,

Tatizo siasi zikiingilia huduma za afya zinazidisha kuzorotesha huduma.

Ukitaka mtu ashughulikiwe WEKA USHAHIDI,CHUKUA VIDEO TUONESHE MUHISIKA ALIYEGOMA KUKUPA HUDUMA, mambo kwa ushahidi....Onyesha kadi yako umeandikiwa then ukakosa huduma

Kwa kufanya hivyo huyo mtu au watu wanaozorotesha huduma watapewa onyo au kushughulikiwa ipasavyo ila hii ya kuja kutafuta huruma bila ushahidi acha.

Leta ushahidi ili tudeal na wanaotuharibia huduma, ila vinginevyo acha siasi.

Vituo vyote vya afya nchi nzima vinafunguliwa masaa 24 ,sasa wew unsyesems jumapili hawafanyi kazi hapo tayari umetufunga kamba,jitathimini na uache chuki.

Pia kama mpenda maendeleo ya afya cha kwanza,ungemtafuta mganga mkuu wa wilaya hio ,lakin watu kama wew huwezi ...acha siasa kwenye vitu vya taaluma.

Sasa kama watu wanalalamikia JKCI yenye wahudumu wa kutosha sitashangaa wewe,
 
Mpaka nalalama maana ake kuna changamoto, hebu zifanyiwe kazi. Ushahidi kwani hapa ni Mahakama? Ujumbe wangu ufike kwa walengwa👊👊👊
Swali jepesi kituo kina watumishi wangapi? Tukishajua idadi ya watumishi ndio tutoe mchanganuo...manesi wangapi na madaktari wangapi,unaweza kuwa una lawama nyingi kumbe clinician wako chin ya 5 pekee kituo kizima tena wanafanya na upasuaji wa kina mama na watoto licha ya uhaba wao na manesi pia wodi zote hata 10 hawafiki na hio ni health center ikimaanisha inafanya kazi 24/7 ,

Tatizo siasi zikiingilia huduma za afya zinazidisha kuzorotesha huduma.

Ukitaka mtu ashughulikiwe WEKA USHAHIDI,CHUKUA VIDEO TUONESHE MUHISIKA ALIYEGOMA KUKUPA HUDUMA, mambo kwa ushahidi....Onyesha kadi yako umeandikiwa then ukakosa huduma

Kwa kufanya hivyo huyo mtu au watu wanaozorotesha huduma watapewa onyo au kushughulikiwa ipasavyo ila hii ya kuja kutafuta huruma bila ushahidi acha.

Leta ushahidi ili tudeal na wanaotuharibia huduma, ila vinginevyo acha siasi.

Vituo vyote vya afya nchi nzima vinafunguliwa masaa 24 ,sasa wew unsyesems jumapili hawafanyi kazi hapo tayari umetufunga kamba,jitathimini na uache chuki.

Pia kama mpenda maendeleo ya afya cha kwanza,ungemtafuta mganga mkuu wa wilaya hio ,lakin watu kama wew huwezi ...acha siasa kwenye vitu vya taaluma.

Sasa kama watu wanalalamikia JKCI yenye wahudumu wa kutosha sitashangaa wewe,
 
Mpaka nalalama maana ake kuna changamoto, hebu zifanyiwe kazi. Ushahidi kwani hapa ni Mahakama? Ujumbe wangu ufike kwa walengwa👊👊👊
Swali jepesi kituo kina watumishi wangapi? Tukishajua idadi ya watumishi ndio tutoe mchanganuo...manesi wangapi na madaktari wangapi,unaweza kuwa una lawama nyingi kumbe clinician wako chin ya 5 pekee kituo kizima tena wanafanya na upasuaji wa kina mama na watoto licha ya uhaba wao na manesi pia wodi zote hata 10 hawafiki na hio ni health center ikimaanisha inafanya kazi 24/7 ,

Tatizo siasi zikiingilia huduma za afya zinazidisha kuzorotesha huduma.

Ukitaka mtu ashughulikiwe WEKA USHAHIDI,CHUKUA VIDEO TUONESHE MUHISIKA ALIYEGOMA KUKUPA HUDUMA, mambo kwa ushahidi....Onyesha kadi yako umeandikiwa then ukakosa huduma

Kwa kufanya hivyo huyo mtu au watu wanaozorotesha huduma watapewa onyo au kushughulikiwa ipasavyo ila hii ya kuja kutafuta huruma bila ushahidi acha.

Leta ushahidi ili tudeal na wanaotuharibia huduma, ila vinginevyo acha siasi.

Vituo vyote vya afya nchi nzima vinafunguliwa masaa 24 ,sasa wew unsyesems jumapili hawafanyi kazi hapo tayari umetufunga kamba,jitathimini na uache chuki.

Pia kama mpenda maendeleo ya afya cha kwanza,ungemtafuta mganga mkuu wa wilaya hio ,lakin watu kama wew huwezi ...acha siasa kwenye vitu vya taaluma.

Sasa kama watu wanalalamikia JKCI yenye wahudumu wa kutosha sitashangaa wewe,
 
Mpaka nalalama maana ake kuna changamoto, hebu zifanyiwe kazi. Ushahidi kwani hapa ni Mahakama? Ujumbe wangu ufike kwa walengwa👊👊👊
Tatizo ukilalama bila kuweka facts hakuna msaada utao pata,

Ushahid ni mzuri ila watu wawajibishwe vinginevyo inaonekana ni drama, chuki n.k

Mtag DMO wa hiyo wilaya ili changamoto ifanyiwe kazi vinginevyo ni kutwanga maji kwenye kinu.....
 
Back
Top Bottom