Baadhi ya watumishi wa umma Dar kufanyia kazi nyumbani Januari 27 na 28, 2025 sababu ya Mkutano wa Nishati Afrika

Baadhi ya watumishi wa umma Dar kufanyia kazi nyumbani Januari 27 na 28, 2025 sababu ya Mkutano wa Nishati Afrika

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

TAARIFA KWA UMMA

Tanzania imepata fursa na heshima ya kuwa nchi mwenyeji wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika Kuhusu Nishati (Africa Energy Summit) utakaofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 27-28 Januari, 2025.

Mkutano huo unaandaliwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Tanzania, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan; Marais wa Nchi za Afrika 24; wawakilishi wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika 21; Wakuu wa Taasisi za Kimataifa sita (6) wakiwemo Rais wa Benki ya Dunia, Rais wa Benki ya Afrika na Rais wa Taasisi ya Rockefeller; na Washirika wa Maendeleo watano (5) watashiriki Mkutano huo.

Aidha, jumla ya washiriki wengine 2,600 wa ndani na nje ya Tanzania wamejisajili kwa ajili ya Mkutano huo.

Kufuatia ugeni huu mkubwa, baadhi ya barabara muhimu za Jiji la Dar es Salaam zitafungwa kama ilivyotangazwa na Jeshi la Polisi.

Hivyo, ili kuepuka usumbufu ambao unaweza kusababishwa na kufungwa kwa barabara hizo, Serikali inaelekeza kuwa tarehe 27 na 28 Januari, 2025 watumishi wa umma katika Mkoa wa Dar es Salaam wafanyie kazi nyumbani isipokuwa wale ambao mazingira yao ya kazi yanawataka kuwepo katika vituo vya kazi kama vile watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, sekta ya afya na sekta ya usafiri na usafirishaji.

Vilevile, Benki hazitafungwa na biashara katika Soko la Kariakoo zitaendelea kufanyika. Hoteli na migahawa nayo haitafungwa.

Pia soma: DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika

Aidha, waajiri katika sekta binafsi wanashauriwa kuruhusu watumishi wao katika Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi nyumbani au kuweka utaratibu ambao hautasababisha changamoto ya usafiri kutokana na kufungwa kwa barabara hizo.

Imetolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi

Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka
KATIBU MKUU KIONGOZI
26 Januari, 2025

1737891342570.png
 
Wakuu,

TAARIFA KWA UMMA

Tanzania imepata fursa na heshima ya kuwa nchi mwenyeji wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika Kuhusu Nishati (Africa Energy Summit) utakaofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 27-28 Januari, 2025. Mkutano huo unaandaliwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Tanzania, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan; Marais wa Nchi za Afrika 24; wawakilishi wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika 21; Wakuu wa Taasisi za Kimataifa sita (6) wakiwemo Rais wa Benki ya Dunia, Rais wa Benki ya Afrika na Rais wa Taasisi ya Rockefeller; na Washirika wa Maendeleo watano (5) watashiriki Mkutano huo. Aidha, jumla ya washiriki wengine 2,600 wa ndani na nje ya Tanzania wamejisajili kwa ajili ya Mkutano huo.

Kufuatia ugeni huu mkubwa, baadhi ya barabara muhimu za Jiji la Dar es Salaam zitafungwa kama ilivyotangazwa na Jeshi la Polisi. Hivyo, ili kuepuka usumbufu ambao unaweza kusababishwa na kufungwa kwa barabara hizo, Serikali inaelekeza kuwa tarehe 27 na 28 Januari, 2025 watumishi wa umma katika Mkoa wa Dar es Salaam wafanyie kazi nyumbani isipokuwa wale ambao mazingira yao ya kazi yanawataka kuwepo katika vituo vya kazi kama vile watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, sekta ya afya na sekta ya usafiri na usafirishaji. Vilevile, Benki hazitafungwa na biashara katika Soko la Kariakoo zitaendelea kufanyika. Hoteli na migahawa nayo haitafungwa.

Pia soma: DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika

Aidha, waajiri katika sekta binafsi wanashauriwa kuruhusu watumishi wao katika Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi nyumbani au kuweka utaratibu ambao hautasababisha changamoto ya usafiri kutokana na kufungwa kwa barabara hizo.

Imetolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi

Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka
KATIBU MKUU KIONGOZI
26 Januari, 2025

View attachment 3214755
Serikali ijitahidi kutengeneza miundombinu wezeshi ili ikitokea mikutano mikubwa kama hii kazi za uzalishaji pia ziendelee kama kawaida..
Imagine ingekuwa mkutano wa madola sasa si ndo dar yote ingefungwa kabisa..
 
Mm babantilie nifanye kazi nyumbani ya kuwauzia chakula majirani zangu au sio
 
Serikali ijitahidi kutengeneza miundombinu wezeshi ili ikitokea mikutano mikubwa kama hii kazi za uzalishaji pia ziendelee kama kawaida..
Imagine ingekuwa mkutano wa madola sasa si ndo dar yote ingefungwa kabisa..
Waende dodoma, au wameona dodoma hakuna hotel za kuweza ku walaza wageni hao
 
Wakuu,

TAARIFA KWA UMMA

Tanzania imepata fursa na heshima ya kuwa nchi mwenyeji wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika Kuhusu Nishati (Africa Energy Summit) utakaofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 27-28 Januari, 2025.

Mkutano huo unaandaliwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Tanzania, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan; Marais wa Nchi za Afrika 24; wawakilishi wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika 21; Wakuu wa Taasisi za Kimataifa sita (6) wakiwemo Rais wa Benki ya Dunia, Rais wa Benki ya Afrika na Rais wa Taasisi ya Rockefeller; na Washirika wa Maendeleo watano (5) watashiriki Mkutano huo.

Aidha, jumla ya washiriki wengine 2,600 wa ndani na nje ya Tanzania wamejisajili kwa ajili ya Mkutano huo.

Kufuatia ugeni huu mkubwa, baadhi ya barabara muhimu za Jiji la Dar es Salaam zitafungwa kama ilivyotangazwa na Jeshi la Polisi.

Hivyo, ili kuepuka usumbufu ambao unaweza kusababishwa na kufungwa kwa barabara hizo, Serikali inaelekeza kuwa tarehe 27 na 28 Januari, 2025 watumishi wa umma katika Mkoa wa Dar es Salaam wafanyie kazi nyumbani isipokuwa wale ambao mazingira yao ya kazi yanawataka kuwepo katika vituo vya kazi kama vile watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, sekta ya afya na sekta ya usafiri na usafirishaji.

Vilevile, Benki hazitafungwa na biashara katika Soko la Kariakoo zitaendelea kufanyika. Hoteli na migahawa nayo haitafungwa.

Pia soma: DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika

Aidha, waajiri katika sekta binafsi wanashauriwa kuruhusu watumishi wao katika Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi nyumbani au kuweka utaratibu ambao hautasababisha changamoto ya usafiri kutokana na kufungwa kwa barabara hizo.

Imetolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi

Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka
KATIBU MKUU KIONGOZI
26 Januari, 2025

View attachment 3214755
Waajiri wa sekta binafsi wameshauriwa kufanyia kazi nyumbani. Je watumishi wa umma wao watapewa ndege za kuendea kazini?
 
Sio hao tu, kuna madaktari na manes; mapailot na waongozaji wao n.k.
Tangazo liko wazi mbona? Wale watoa huduma za lazima ni lazima waende mf. Watu wa usalama, afya, usafirishaji n.k. Soko la Kariakoo litakuwa open na biashara zingine zitaendelea kama kawaida ...
 
Nani yupo sahihi?
Waziri wa Ujenzi anasema barabara za DART zitatumika kwa wageni na wananchi tutaendelea kutumia barabara za pembezoni. RPC Kanda Maalumu anasema barabara kadhaa zitafungwa kwa muda. NANI YUPO SAHIHI TUMFUATE?
 
Nani yupo sahihi?
Waziri wa Ujenzi anasema barabara za DART zitatumika kwa wageni na wananchi tutaendelea kutumia barabara za pembezoni. RPC Kanda Maalumu anasema barabara kadhaa zitafungwa kwa muda. NANI YUPO SAHIHI TUMFUATE?
Kuna ukurupukaji wa hali ya juu.

Kila mtu anatoa kauli zake.
 
Nani yupo sahihi?
Waziri wa Ujenzi anasema barabara za DART zitatumika kwa wageni na wananchi tutaendelea kutumia barabara za pembezoni. RPC Kanda Maalumu anasema barabara kadhaa zitafungwa kwa muda. NANI YUPO SAHIHI TUMFUATE?
Miscommunications au Kujitutumua, subir tuone.
 
Back
Top Bottom