Baba achinjwa na mwanae

frem zero

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
595
Reaction score
875
Jamani mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Hapa jirani kuna baba mmoja ambae ana watoto wawili wa kiume. Baba huyu inasemekana ni jambazi wa kutupwa. Aliwafundisha watoto wake ujambazi na namna ya kuua watu. Mtoto wake mmoja yupo gerezani huu mwaka wa 15, na huyu mwingine kamaliza kifungo miezi miwili iliyopita.
Sasa hapo juzi ulitokea ugomvi kati yake na mwanae alietoka gerezani. Mtoto kaamua kumchinja baba yake kisha kumchimbia shimo ili kupoteza ushahidi. Kabla hajatimiza azma yake watu wakatokea na ndipo uovu wake ukawa hadharani. Kijana huyo sasa yupo mahabusu, na taratibu za mazishi zinaendelea.

NB: wazazi waleeni watoto katika njia ipendezayo machoni pa Mungu nao hawataiaacha hadi uzeeni kwao.
 
Hii habari yako mbona n copyright na ile habari ya Ruvuma last wk.....?? Manake hujatutajia jina la eneo yalipotokea mauaji, jina la marehemu maana n jirani yako, jina la mtuhumiwa na lini tukio limetokea muda na mahali...... Vinginevyo nahisi kama fiction story with intention to teach others
 
Sasa nikitaja hadi sehemu si utaelewa nilipo na unaweza kunitambua? Nashukuru ujumbe umefika na kila mtu atakuwa mzazi mwema kwa mwanae. Hili ni somo kubwa sana kwa wazazi na wanaotarajiwa kuwa wazazi baadae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…