Baba atiwa mbaroni Songwe kwa tuhuma za kumuua mwanawe kisa chenji ya Sh9,000 baada ya kutumwa kununua chapati

Baba atiwa mbaroni Songwe kwa tuhuma za kumuua mwanawe kisa chenji ya Sh9,000 baada ya kutumwa kununua chapati

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe linamshikilia Festo Nzuki (39), mkazi wa Kitongoji cha Izyila, Kata ya Mlowo, Wilaya ya Mbozi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake, Jackson Nzuki (10) ambaye ni mwanafuzi wa darasa la sita, Shule ya Msingi Ivwanga kwa madai ya kutorudisha chenji ya Sh9,000 baada ya kutumwa kununua chapati.

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne, Januari 7, 2025 na kamanda wa polisi mkoa huo, Augustino Senga inaeleza kuwa, tukio hilo limetokea Januari 2, 2025 asubuhi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

Senga amedai kuwa, Desemba 30, 2024, Jackson alipigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na mtuhumiwa ambaye ni baba yake mzazi kwa kutumia fimbo, mateke na ngumi.

Amedai kuwa, baada ya kuona mtoto huyo amezidiwa saa moja usiku wa Januari mosi, 2025 aliamua kumpeleka Hospitali ya llasi kwa ajili ya matibabu na baadaye Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Songwe baada ya kuzidiwa.

Hata hivyo mtoto huyo alifariki akiwa anapatiwa matibabu.

"Uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha tukio hilo ni baada ya marehemu kutorudisha chenji Sh9,000 aliyopewa na mtuhumiwa baada ya kuagizwa kununua chapati. Uchunguzi wa tukio hili bado unaendelea na pindi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani," amesema Kamanda Senga.
 
Inasikitisha sana mkuu.

Hayo ni mauaji yaliyorepotiwa ,kuna mwingine kesi imeletwa Polisi kawe Bodaboda ameua muuza chips kisa ametembea na house girl wake.
 
Inasikitisha sana mkuu.

Hayo ni mauaji yaliyorepotiwa ,kuna mwingine kesi imeletwa Polisi kawe Bodaboda ameua muuza chips kisa ametembea na house girl wake.
Aisee....itakuwa alikuwa anamla huyo msaidizi wa kazi...haiwezekani
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe linamshikilia Festo Nzuki (39), mkazi wa Kitongoji cha Izyila, Kata ya Mlowo, Wilaya ya Mbozi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake, Jackson Nzuki (10) ambaye ni mwanafuzi wa darasa la sita, Shule ya Msingi Ivwanga kwa madai ya kutorudisha chenji ya Sh9,000 baada ya kutumwa kununua chapati.

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne, Januari 7, 2025 na kamanda wa polisi mkoa huo, Augustino Senga inaeleza kuwa, tukio hilo limetokea Januari 2, 2025 asubuhi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

Senga amedai kuwa, Desemba 30, 2024, Jackson alipigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na mtuhumiwa ambaye ni baba yake mzazi kwa kutumia fimbo, mateke na ngumi.

Amedai kuwa, baada ya kuona mtoto huyo amezidiwa saa moja usiku wa Januari mosi, 2025 aliamua kumpeleka Hospitali ya llasi kwa ajili ya matibabu na baadaye Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Songwe baada ya kuzidiwa.

Hata hivyo mtoto huyo alifariki akiwa anapatiwa matibabu.

"Uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha tukio hilo ni baada ya marehemu kutorudisha chenji Sh9,000 aliyopewa na mtuhumiwa baada ya kuagizwa kununua chapati. Uchunguzi wa tukio hili bado unaendelea na pindi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani," amesema Kamanda Senga.
View attachment 3195190
Umasikini ni shida sana.
Labda huyo mtoto hiyo hela amepoteza maana angekuwa nayo au ametumia kiasi angemrudishia huyo baba yake. Mtoto wa miaka kumi hawezi akatumia hiyo hela yote kwa muda mfupi.
 
Mzazi usimhadhibu mtoto wako ukiwa na hasira.
 
Back
Top Bottom