Baba Levo ataja watu waliomsaidia wakati hana kitu. Amtaja Nature na Shilole. Alifukuzwa kwa kudokoa chakula kwenye friji

Baba Levo ataja watu waliomsaidia wakati hana kitu. Amtaja Nature na Shilole. Alifukuzwa kwa kudokoa chakula kwenye friji

Maghayo

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2014
Posts
20,307
Reaction score
47,210
Ebana wanajamvi inakuwaje?

Mjasiriamali, mwanasiasa, mchekeshaji na muhamasishaji nchini maarufu Baba Levo ametaja waliomsaidia wakati hana kitu.

Amesema kuna utitiri wa watu anaweza kuwashukuru kwa kumsaidia lakini atataja watano.

Watu ni wengi nilikuwa nalala sinza kwa jamaa anaitwa K Mazoba. Nilikuwa nadokoa msosi kwenye Friji hadi mke wa jamaa akamind ikawa sitonfahamu.

Nimeshawahi kulala Sinza kwa ghetto la jamaa anaitwa Sadi Yuda. Lilikuwa Ghetto la vibaka tulikuwa tunalala watu 15. Nilikuwa nalala uvunguni unakuta vibaka akipigwa huko anakuja kujificha uvunguni ninapolala huku damu zinamvuja nakutapakaa kwangu.

Anaendelea kusema ghetto lilikuwa na feni moja tu ile ya gari isiyozunguka ilikuwa inampuliza bosi tu.

Ukisema utaje list ya watu utataja list ya mamilion. Juma Kassim Kiroboto Nature alinikaribisha na kuniingiza TMK wanaume. Wakati huo inspector Haroun hawataki niingie kwenye kundi. Nature akawaambia ambae hawamtaki huyu dogo aache kundi.

Mimi njaa ilikuwa inanipiga duniani hamna mtu aliyekuwa ananisaidia kula kama Shilole Shishi food. Nilikuwa nakula hadi nikampa Jina kula jigaragaza. Tena bure pale kwake bila kutoa mia.

Hapo mbeleni nilikuwa nawabeza kuwadharau hawa kina mwijaku, baba levo na Dotto magari ila hawa jamaa wamepiti0a magumu nimetoka kuwakubali.

Pia imetokea kuwakubali sana Shilole na Juma Nature. Nature nilimchukiaga bure sana baada ya bifu na Mh. Temba ila kumbe jamaa poa sana. Nature na Shilole na wengine Mungu awabariki .

Sasa hivi Baba Levo na Mwijaku wako China wakiwakilisha vema Tanzania na kutangaza Silent Ocean Simba wa Bahari. Mungu awatangulie hawa miamba.

Screenshot_20240706-201009_Facebook.jpg
 
Pia jambo lingine la kusisimua ni yule producer wa marehemu wa Sam wa ukweli mwanamuziki wa Bongo Flavour. Jamaa alipokuwa anaumwa mahututi alikuwa anamsafisha kumuogesha nakumbadilisha diapers. Fikiria tu moyo wa jamaa ulivyo wa upendo. Kumbuka hata ndugu walikuwa hawajishughulishi. Alipokuwa kwenye msiba ndo hao kwa wingi. Kuna watu wachache duniani wameumbwa kipekee. Tujikumbushe na hiki kibao murua hapo chini. Endelea kulala salama Sam wa ukweli.


View: https://youtu.be/0my66XdpFJU?si=5B0ocU_RoIBkdYcy
 
Siamini inspector haroun ana roho mbaya kiasi hicho. Big up Juma Nature kwa moyo wa huruma kwa kumsaidia baba Levo.
 
Watu wenye mioyo hiyo huwa hatufanikiwi
Duniani wanyang'anyi hufanikiwa kwa sababu hujawa uchu wa kukusanya na kupata mali zaidi. Ila wenye nyoyo za kutoa huishia kutumika tu ndio maana usishangae hawa mastar au watu wakubwa, kuna watu wengi walifanyika daraja la mafanikio yao lakini wao kamwe hawafanikiwi kwa level ile ile.
 
Kumbe Ukiwa utumwa wa waarabu, hapo maisha umeshayaweza🤔
 
Duniani wanyang'anyi hufanikiwa kwa sababu hujawa uchu wa kukusanya na kupata mali zaidi. Ila wenye nyoyo za kutoa huishia kutumika tu ndio maana usishangae hawa mastar au watu wakubwa, kuna watu wengi walifanyika daraja la mafanikio yao lakini wao kamwe hawafanikiwi kwa level ile ile.
Nimekuelewa vizuri sana
 
Back
Top Bottom