Baba mkwe kakataa mahari... kuku!

Baba mkwe kakataa mahari... kuku!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Kabla hujaamua kupeleka mahali kwa watu hasa kwa wale wasio wa kabila lako husisha watu kwanza...

Kijana mmoja chakaramu alimpenda binti kutoka mojawapo ya makabila yanayofuga ng'ombe sana maeneo ya kanda ya ziwa. Bila kumuuliza mpenzi wake jamaa akaamua kufunga safari kwenda kijijini kwa wazazi wa binti kujitambulisha. Alipofika huko akajitambulisha na kuleta zawadi za kuku kama kianzio cha mahari...mambo yalikuwa hivi:

Mzee: Karibu kijana habari za wapi?
Kijana: Miye natoka mjini mzee na nimekuja kuleta ujumbe wangu wa kujitambulisha
Mzee: Ah kujitambulisha nini?
Kijana: Mzee mimi na binti yako tunaishi pamoja na nimekuja kuomba baraka zako ili nimuoe
Mzee: Umekuja kunini!!? kwa tahamaki mzee aliuliza.
Kijana: Kuomba baraka zako.

Mzee alikaa kimya kwa sekunde kidogo.

Mzee: Na hilo tenga la kuku?
Kijana: Mzee ni kifunga uchumba!
Mzee: Baba una wazazi wewe?
Kijana: Hapana mzee wazazi wangu walishafariki
Mzee: Una wazee huko kwenu?
Kijana: Wazee wa nini tena baba?
Mzee: Kijana umenitusi na kunitukana kwa namna za ajabu kabisa. Naomba uondoke hapa.


To cut the long story short...


Miaka 25 baadaye kijana (sasa mzee) anaishi na binti wa wote; wamezaa watoto na hawajafunga ndoa na hajaonana na baba mkwe tangu siku ile.
 
Asante kwa hadithi hadithi!.

Ila haijatulia kwa sababu its too good to be true!.

Muoaji toka kabila la wafugaji kwenda na kifungauchumba cha kuku?!.

Binti unaishi nae asikueleze mahitaji ya kwao?!.

Baada ya ba mkwe kususa life ikaendelea miaka 25!. Msuso wa wazazi hata mwaka tuu ni karne, ndio itakuwa miaka 25!.

All and all hadithi ni hadithi,

Thanks.

Pasco
 
Asante kwa hadithi hadithi!.

Ila haijatulia kwa sababu its too good to be true!.

Muoaji toka kabila la wafugaji kwenda na kifungauchumba cha kuku?!.

Binti unaishi nae asikueleze mahitaji ya kwao?!.

Baada ya ba mkwe kususa life ikaendelea miaka 25!. Msuso wa wazazi hata mwaka tuu ni karne, ndio itakuwa miaka 25!.

All and all hadithi ni hadithi,

Thanks.

Pasco


well ni kweli kwa kila details ukiondoa "pakacha"; walikuwa kuku lakini.
 
Kuna mambo ya washenga, huendi peleka uchumba bila kuwa na mshenga. Huyo jamaa alikosea kwa hilo!


Chengine sidhani kama kwenye sehemu za kufunga ndoa wanauliza kama baba na mama wameridhika au mmpata baraka zao. Wangapi wameoana bila ya kupata muafaka wa wazee wao, kama wameamua kuishi pamoja bila baraka za wazee sioni tatizo la kutofunga ndoa, it doesn't make different to me.
 
Hay MM naona umeamua utembelee jukwaa hili kwa staili ya kishigongo shigongo,karibu mwanafyale
 
Back
Top Bottom