Baba wa Taifa aliwahi kukiri hivi

Baba wa Taifa aliwahi kukiri hivi

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Katika kuangaza macho kwenye media nilikutana na hotuba/mahojiano ya Nyerere na akakiri kwamba wao kama wapigania uhuru hawakuwahi kuleta jambo jipya liwalo lolote katika nchi hii.

Kama ni mipaka waliikuta. Kama ni jina la nchi walilikuta, kama ni taifa walilikuta, kama ni watu waliwakuta. Nyerere anakiri wazi kuwa jambo pekee walilofanikisha wao ni kuiunganisha Tanganyika na Zanzibar. Hii yaweza kuwa kigezo cha kuutetea Muungano?

Viongozi wa sasa hawampendi Mwalimu, lakini wanajaribu kutetea Muungano kwa kadri wawezavyo. Najiuliza, ili kufanya kitu kipya nje ya wakoloni ilikuwa ni lazima kufanya Muungano? Ambapo Muungano wenyewe una nyufa na viraka hadi basi.

Leo Muungano ukifa, sisi kama Taifa tutakuwa na lipi la kujivunia?
 
Katika kuangaza macho kwenye media nilikutana na hotuba/mahojiano ya Nyerere na akakiri kwamba wao kama wapigania uhuru hawakuwahi kuleta jambo jipya liwalo lolote katika nchi hii. Kama ni mipaka waliikuta. Kama ni jina la nchi walilikuta, kama ni taifa walilikuta, kama ni watu waliwakuta. Nyerere anakiri wazi kuwa jambo pekee walilofanikisha wao ni kuiunganisha Tanganyika na Zanzibar. Hii yaweza kuwa kigezo cha kuutetea Muungano? Viongozi wa sasa hawampendi Mwalimu, lakini wanajaribu kutetea Muungano kwa kadri wawezavyo. Najiuliza, ili kufanya kitu kipya nje ya wakoloni ilikuwa ni lazima kufanya Muungano? Ambapo Muungano wenyewe una nyufa na viraka hadi basi. Leo Muungano ukifa, sisi kama Taifa tutakuwa na lipi la kujivunia?

Raia Fulani;

Kwani Ethiopia na Eritrea wanaishi kwa masikitiko? Muungano ukifa kila mtu atabakia katika nchi yake na atajifunia sehemu yake.
 
Raia Fulani;

Kwani Ethiopia na Eritrea wanaishi kwa masikitiko? Muungano ukifa kila mtu atabakia katika nchi yake na atajifunia sehemu yake.
Hata Sudan zote wanaishi japo kwa amani sasa. Binafsi siamini kuwa Muungano ukifa tutatikisika. Sijajua siri ya ccm hadi leo kubembelezea Muungano ni nini hasa. Na kwa mujibu wa marehemu Baba wa Taifa Muungano ukifa hakuna jipya ambalo sisi kama watanganyika tumelifanya jipya tangu kuweko kwa nchi hii.
 
Hata Sudan zote wanaishi japo kwa amani sasa. Binafsi siamini kuwa Muungano ukifa tutatikisika. Sijajua siri ya ccm hadi leo kubembelezea Muungano ni nini hasa. Na kwa mujibu wa marehemu Baba wa Taifa Muungano ukifa hakuna jipya ambalo sisi kama watanganyika tumelifanya jipya tangu kuweko kwa nchi hii.

Raia Fulani;

Tatizo ni kuwa Nyerere alikuwa anatoa mawazo yake kwa watu wasiofikiri au kumuuliza maswali ya udadisi. Kitendo cha kuvunja muungano ni tukio jipya kwa sababu kutatokea nchi mbili zenye katiba, muundo wa kiserikali na mifumo mingine iliyo tofauti kabisa na hile ya 1964. Hivyo hoja ya Nyerere haina msingi.

Kwa kuongezea, watanganyika, wazanzibar, au watanzania kwa ujumla wanatakiwa kuangalia jinsi ya kuboresha maisha yao. Kuangalia umefanya nini kipya wakati unaishi maisha duni hakuna mpango wowote.
 
Ndugu mtoa hoja,
nitangulie kusema kua (kwa mawazo yangu) muungano uwepo ama usiwepo bado maisha ya Watanganyika na Wazanzibari yataendelea kuwepo. Kwa hiyo nje ya muungano matatizo tuliyonayo yataendelea kuwepo hali kadhalika pia ndani ya muungano bado matatizo tuliyonayo yataendelea kuwepo. nasema hivi kwa maana kua matatizo yanayotukabili kwa sasa (binafsi kwa mtazamo wangu) hayasababishwi na muungano bali kiini hasa cha matatizo ni viongozi kukosa sifa za uongozi.

Katika hali isiyokua ya kawaida utamkuta mtu anataka kuwa kiongozi, labda katika ngazi ya kijiji/mtaa (mwenyekiti), kata (diwani), jimbo (mbunge) au hata nchi (rais), cha ajabu utakuta mtu huyo ukimwuliza swali kua kwa nini anataka kua kiongozi jibu lake litakua jepesi sana eti anataka kuleta maendeleo ktk eneo husika. Kiuhalisia kazi ya kiongozi ni kuwaongoza watu wake waweze kufikia malengo yao waliyojiwekea. Sasa mbunge anaposema ataniletea maendeleo (sawa sikatai ila) nashangaa sana kwa sababu leo namchagua kuwa mbunge wangu lakini baada tu ya uchaguzi haonekani jimboni mpaka baada ya miaka mi5 kupita, sasa atapata wapi mawazo yangu ili aweze kuniongoza kufikia malengo yangu? (KUMRADHI MTOA HOJA, NIMETOKA NJE YA MUKTADHA ILI NIWEZE KUELEWEKA).

Nikirudi kwenye hoja ya msingi (kama nilivyoielewa mimi) ni kwamba watu wanataka kuwa viongozi ili waweze kutajirika kwa haraka kupitia rasilimali za taifa pamoja na jasho la wavuja jasho. hapa ndipo matatizo mengi ya sisi Watanzania (au hata Waafrika na sehemu zingine kwa ujumla) yanapoanzia, kisa nini? (eti siasa inalipa). Watu wanaacha taaluma zao ili wapewe vyeo vya kisiasa (wakuu wa wilaya kwa mfano kutoka uandishi wa habari, uhandisi, ualimu wa shule au chuo, nk.).

Niseme tu kwamba tusiumize vichwa kukomalia kuwa na muungano ama la, cha msingi tukomae na viongozi wetu japo wapunguze uroho wa madaraka. Hili tutalifanikisha kwa kuanza mchujo mkali ngazi ya mtaa na kuendelea, yaani tuanze kuwahoji hao wanaotaka kutuongoza kama wako tayari kutuongoza kweli. Na kama wako tayari kutuongoza basi tuwekeane utaratibu (sijui kama upo kwenye katiba) wa kuwatathmini hao viongozi kila baada ya muda fulani (mfano kwa mwenyekiti wa mtaa/kijiji kila baada ya miezi miwili au mitatu). Tathmini hii inaweza kufanyika kupitia (kwa mfano) kusomewa mapato na matumizi au kupewa taarifa za muhimu kuhusu utekelezaji wa mipango yetu pamoja na kutoa mapendekezo palipo na mapungufu. Tukiweza ngazi za chini hata huko kwenye ubunge na urais tutafanikiwa pia.

Nasisitiza tena kua haya masuala ya muungano (kuudumisha au kuuvunja) tuachane nayo wala hayatusaidii asilani. 'Nasikia' siku hizi tumeongeza na mambo mengine kama (mfano tu lakini) umakonde na unyakyusa, ufreemason na umizimu, ubara na uvisiwani, na mengineyo mengi ya kufanana na hayo. Vyote hivi ni kama mbwa kutupiwa mfupa halafu mwizi anaingia ndani na kufanya mambo yake bila bughudha yoyote.

Mwisho, kumradhi kama nimetoka nje ya mada husika.
 
Raia Fulani;

Kwani Ethiopia na Eritrea wanaishi kwa masikitiko? Muungano ukifa kila mtu atabakia katika nchi yake na atajifunia sehemu yake.
Ethiopia kuna part inapigania kujitenga ambayo ina wasomali wengi kuna kikundi kinapigania kujitenga.
 
Hii ishu ya muungano kwa kweli inaumiza kichwa, mpaka sasa najiuliza kwa nini Mwalimu alikuwa anautetea sana. Kwa mtazamo wangu ni wakati muafaka wa kujadiliana kama taifa kuhusu hatma ya huu muungano.
 
Kwa kweli, nikijaribu kuangaza huu muungano,bado naona watanganyika na wazanzibar wanatukuza utaifa wao kuliko utanzania.

Kwa kweli, watanganyika wanahesabu Tanganyika kwanza, TANZANIA baadaye; hali kadhalika wazanzibar!
Hivyo,sitarajii maajabu yoyote kutokea pale muungano utakapo vunjika.
 
Back
Top Bottom