Dah huko Kenya kuna nini tena, huyu kijana mwanasiasa Babu Owino amemshoot mtu yaani bila hata huruma na mabody guard wanamburuza nje kama gunia huyo aliyetunguliwa.
Serikali ya Kenya hapo itabidi msifumbie macho hili jambo hakuna kiongozi yupo juu ya sheria yaani nashangaa Wakenya mpo kimya hili jambo lingekuwa Marekani ingekuwa top in CNN na BBC.
Wakenya mtujuze zaidi. Video hii hapa (CCTV footage ) ila naona mtu ameshaiweka watermark ya jina lake.
Raia wanaruhusiwa kumiliki silaha bora upate leseni kutoka polisi. Babu mwenyewe alikuwa na leseni ila ametumia silaha kinyume na sheria. Wacha ale maharagwe huko rumande.