Badala ya serikali tatu iwe majimbo

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Muungano wa serikali mbili (muungano na Zan.) bila ya kuwepo kwa Tanganyika ni vigumu kukubalika hasa kwa watu wenye akili njema. Nadhani hata Nyerere hakumaanisha serikali mbili, haikuwa mwisho wake wa kufikiri na kutenda juu ya muungano huu bali alikuwa na mpango wa kuwa na muungano wa serikali moja pole pole kadri siku na fursa zilivyokuwa zinatokea. Kuwa na serikali tatu ni jambo ambalo halitekelezi sana kwa sababu ya tofauti ya ukubwa na udogo wa Tanganyika na Zanzibar hasa kwenye kuchangia gharama za muungano. Nyerere nadhani hata yeye alilijua hili. Kuunganisha TANU na ASP kuwa CCM ulikuwa mchakato wa kuelekea serikali moja. Nyerere kaondoka kabla ya ndoto yake ya serikali moja haijatimia, je viongozi mliomfuata Nyerer mna ajenda gani? kuirudisha ASP na TANU tena au kuifuta serikali ya Zanzibar kama ilivyo ya Tanganyika? Kama kufuta mama (ASP) kuliwezeka kwanini kufuta toto lake (SMZ) kushindikane? Inavyoonekana kufuta SMZ kuko mbali sana katika zama hizi ambazo matoto ya wale waarabu waliopinduliwa (CUF) wanashirikiana na matoto ya waliopindua (ASP/CCM). Ndoto ya CUF ni kujitenga kama sio kwa Zanzibar basi angalau kwa Pemba ili kuwaalika babu zao.

Kama selikali moja imeshindikana basi njia muafaka wa kuunusuru muungano na kuwaridhisha watanganyika pia ni kuendesha nchi kwa njia ya majimbo. majimbo yanayojiendesha yenyewe japo kwa asilimia 60 yatafanana na SMZ. Ni upuuzi mkubwa kuona Zanzibar yenye watu 1m iwe na idadi sawa ya wajumbe na Tanganyika yenye watu 44m kwenye tume ya madadiliko ya katiba kwa kisingizio kwamba Zan ni nchi kamili. Kama Zan ni nchi kamili kwanini watu wa Zan wahodhi ardhi kwenye nchi nyingine (Tanganyika) bila hata ya mashariti yoyote? Kama Zan ni nchi kamili kwanini isilipe gharama sawa na Tanganyika katika serikali ya Muungano? Kama Tanganyika itakuwa na majimbo yenye angalau watu milioni 5 kila jimbo basi kelele za muungano na Zanzibar zitapungua kama sio kwisha kabisa. Tuachane na serikali mbili au tatu zinazotuumiza vichwa.
 
sio lazima wazanzibar kuungana tukutane kwenye africa mashariki
 
Kama selikali moja imeshindikana basi njia muafaka wa kuunusuru muungano na kuwaridhisha watanganyika pia ni kuendesha nchi kwa njia ya majimbo.

Mkuu kavulata

Kwa nini iwe 'kuunusuru' muungano? Kwani huo muungano ni so imperative hadi izungumzwe kuunusuru? Kumbuka hapa unazungumzia nchi mbili tofauti ambazo kwa wakati fulani(as of 1964) zilikubaliana na kuridhiana katika mambo kadha wa kadha yaliyozaa huo muungano. Kama ilivyokuwa kwa wakati ule, hata leo nchi hizi kila moja kwa status yake inayohaki ya kutoka katika makubaliano na maridhiano hayo kuamua it's own fate.

Halafu kwa nini iwe kuwaridhisha watanganyika na siyo wazanzibari ama watanzania? What's your point here? Huwezi kuzungumzia hatima ya muungano huku ukizungumzia hatima ya mdau mmoja tu wa muungano unless unazungumzia kitu kingine hapa.

Unazungumzia mfumo wa serikali wa JMT kwa kukana serikali tatu huku ukipendekeza majimbo kwa base ya gharama, umefanya cost analysis na kuona utofauti wa gharama baina ya mambo haya mawili? Vipi mfumo huo utakuwa effected? Halafu unafikiri ni Tanganyika pekee ndiyo ya kuamua juu ya muundo huo? Absolutely wrong. As far as unazungumzia muungano ujue si jambo rahisi la kutafuta ridhaa ya Tanganyika tu, hiyo itahusu ridhaa ya Zanzibar pia.
 
Last edited by a moderator:
Muungano wa nini? una faida gani kwako, uwe wa Serikali moja, mbili, tatu au kumi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…