Saint Anne
JF-Expert Member
- Aug 19, 2018
- 76,039
- 230,142
Habari
Najua unapitishwa katika magumu, mazito na maumivu ni makali hayastahimiliki lakini nakuomba mno usivunjike moyo.
Usiwaze kunywa sumu
Kunywa sumu si suluhisho,wapo watu wengi sana nyuma yako wanakutegemea. Kunywa sumu hakutatatua Shida unazopitia.
Usiwaze kuacha kufanya
Inawezekana kabisa umeshajaribu mara nyingi kufanya lakini umejikuta umeishia kushindwa. Usiache kujaribu tena..ipo siku utaweza.
Usiwaze kufunga biashara
Hata kama wateja hawaonekani na kila siku unaishia kupata hasara. Ukiwatazama wenzio wanaofanya biashara Kama yako wanafanikiwa lakini kwako ni tofauti...Ipo siku utafanikiwa.
Usiende kwa mganga,usikubali kabisa shetani akakudanganya,Endelea kumuomba Mungu naye atatenda.
Bado lipo tumaini,bado unayo nafasi,Mungu analo kusudi na Wewe.
-Unayo nafasi ya kurekebisha makosa yako.
-Unayo nafasi ya kujipanga upya.
-Bado unayo nafasi ya kufanya vizuri zaidi.
Mungu amekuamini kwamba unaweza na Ndiyo maana bado Amekupa huo uzima.
Usikubali kuishia njiani,
Hakikisha unafanya zaidi ya ulivyofanya Jana.
Be blessed
Najua unapitishwa katika magumu, mazito na maumivu ni makali hayastahimiliki lakini nakuomba mno usivunjike moyo.
Usiwaze kunywa sumu
Kunywa sumu si suluhisho,wapo watu wengi sana nyuma yako wanakutegemea. Kunywa sumu hakutatatua Shida unazopitia.
Usiwaze kuacha kufanya
Inawezekana kabisa umeshajaribu mara nyingi kufanya lakini umejikuta umeishia kushindwa. Usiache kujaribu tena..ipo siku utaweza.
Usiwaze kufunga biashara
Hata kama wateja hawaonekani na kila siku unaishia kupata hasara. Ukiwatazama wenzio wanaofanya biashara Kama yako wanafanikiwa lakini kwako ni tofauti...Ipo siku utafanikiwa.
Usiende kwa mganga,usikubali kabisa shetani akakudanganya,Endelea kumuomba Mungu naye atatenda.
Bado lipo tumaini,bado unayo nafasi,Mungu analo kusudi na Wewe.
-Unayo nafasi ya kurekebisha makosa yako.
-Unayo nafasi ya kujipanga upya.
-Bado unayo nafasi ya kufanya vizuri zaidi.
Mungu amekuamini kwamba unaweza na Ndiyo maana bado Amekupa huo uzima.
Usikubali kuishia njiani,
Hakikisha unafanya zaidi ya ulivyofanya Jana.
Be blessed