Bagamoyo au kigamboni?

Angalau leo ndugu yake Munawar umeandika kwa kiswahili.
Hakuna website yenye maelezo hovyo kama yenu aisee,sijawahi kuona.Yaani full ujanja,no details za kutosha,hamtaki dalali wakati nyie wenyewe ni madalali au mashanta kwa lugha za mjini

Tunawalaumu watu humu tu kumbe kuna wengine hadi wanamiliki mitandao na viingereza vingi kumbe hovyo kabisaaa.

Najuta kuifungua
 


Wasalaam,
Tunakiri huenda hatujakidhi mahitaji yako, taasisi zote zinaendeshwa kwa hali ya kupenda kujiboresha. Kwa uungwana na unyenyekevu wa dhati kabisa, tungefurahi kufahamu taarifa ulizozitarijia lakini hukuwa umezipata. Pia tunapenda kukufahamisha ya kwamba, katika uuzwaji wa mali hapo mtandaoni, hatuhusiki katika mauzo kwa vyevyote vile, madalali na wenye mali ni sehemu ya wateja wetu, tukiwa na jukumu kuu la kuwawekea jukwaa la hao watajwa kujitangaza na kuwakutanisha na wahitaji kiurahisi zaidi.
Mtandao wetu umesheheni makala mbalimbali ambazo kwa idadi zinafika walau 100, tumeweka taarifa, miswada na matamko ya serikali ili kuhabarisha umma, wadau na wawekezaji wa ndani na nje, tunatangaza mali zilizopo zaidi ya mataifa 120 duniani.

Tunakushukuru kwa kututembelea tunatarijia ushirikiano wako wa dhati kati uboreshaji wa huduma zetu.

Wako katika ujenzi,

Afisa habari.
 

Aaleykum Salaam.
Mie mwanzo nilijua hujui kiswahili,maana kila ukiingia humu kizungu,kumbe mkipelekana kiswahili kinakuja.

Haya,hembu tuambie bei kiasi gani,ukubwa kiasi gani,vipo umbali gani na barabara au pwani nk.

Hapo utakuwa umesaidia wengi.Maana kuna watu bundle zao ndogo,sasa umwambie afungue JF na website yako ndio apate maelezo utakuwa unamzonga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…