BahariPesa: Matumizi Mabaya ya Taarifa za Watu na Lugha za Matusi

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,497
Reaction score
4,775
Kwa muda mrefu sasa,Kampuni ya Ukopeshaji Pesa ya Mtandaoni ijulikanayo kama BahariPesa imekuwa na Tabia ya Kutoa siri za wateja wao hasa wale wanaodaiwa na kutuma taarifa zao kupitia namba za watu wengine bila kuwahusisha watu hao pindi wanapotumiwa taarifa hizo. Pamoja na BahariPesa licha ya kuwa inachakata taarifa za watu na kudhalilisha wale wanaowadai,lakini pia imekuwa ikitoa lugha chafu na za matusi na za kudhalilisha pindi watu waopokea meseji za wadaiwa wanapotaka kuhoji juu ta matumizi ya namba zao kwa kampuni hiyo.

Kampuni ya BahariPesa mbali na kutumia lugha za hovyo kwa watu wanaohoji juu ya uhalali wa wao wa kama kampuni kuchakata taarifa za watu kinyume na taratibu na makubaliano ya wahusika, kampuni imekuwa kimya bila ya kujibu malalamiko wa watu.

Nimeambatanisha hapa record ya sauti ya mtu kutoka katika kampuni hiyo ya ukopeshaji ambae inatumia application za plastore kuwakopesha na kisha kumwaga siri za wateja wao hadharani.
Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu,lakini pia serikali iwapige marufuku kampuni hiyo kututumia ujumbe wa watu wanaowadai.

Tumechoka matusi yao.
 

Attachments

  • baharipesa.mp4
    3.9 MB
Huwajui hawa? Walinisumbua sana hawa kima wana namba hapo walipo kama 300 hivi. Na kila dakika 5 wanakuendea hewani wewe au ndugu zako. Kwa nn mnawakopa hawa?
 
Huwajui hawa? Walinisumbua sana hawa kima wana namba hapo walipo kama 300 hivi. Na kila dakika 5 wanakuendea hewani wewe au ndugu zako. Kwa nn mnawakopa hawa?
Mtu mwingine anaweza kukopa,lakini wao bado wakakutumia meseji,wakijua kuwa wakati wakikopeshana na mtu huyo hawakukushirikisha
 
Bila hawa watu kukamatwa, huu upuuzi hautaisha. Law enforcement hakuna kabisa.
 
Maxence Melo
 
Anakopeshwa mwingine,
Kurudisha mkopo anasumbuliwa mwingine!!
Na wanavyozidi kuachwa ndivyo wanavyozidi kujiona wao ndio wao,utafikiri nchi ya kwao peke yao, na taasisi za fedha zipotu zinawatazama
 
Bila hawa watu kukamatwa, huu upuuzi hautaisha. Law enforcement hakuna kabisa.
Wanalalamika kila siku,lakini mamlaka zinawatazama,ni muda sasa hata hiyo App yao kufungiwa.
 
Wanakopesha shingapi kwa mara ya kwanza kabisa niwaendee juu kwa juu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…