Bahati mbaya hatuna Tony Olumelu wa kwetu, angetupunguzia umbeya miongoni mwa vijana

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Nigeria wanaye tajiri mmoja anaitwa Tony Olumelu. Huyu bwana anao mradi maalum (foundation) kwa ajili ya vijana wa kiafrika wenye mawazo mazuri ya kibiashara (entrepreneurship).

Kwa miaka kadhaa amekuwa akihamasisha ujasiriamali miongoni mwa vijana wa bara la Afrika. Waafrika wa mataifa ambayo yameshajitambua kama vila Ethiopia wamekuwa wakifaidika sana na foundation ya Olumelu.

Nimetamani sana jambo kama hili lingekuwa linafanyika nchini mwetu kwa kasi kubwa, ukizingatia kuwa mazingira ya kibiashara ni rafiki licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali zinazohusiana na mazingira ya uwekezaji.

Taasisi ya Olumelu inaandaa wajasiriamali vijana wa kiafrika, inawapa changamoto nzuri sana.

Inakera sana kuwaona vijana wa kiethiopia wakiwa kwenye harakati za kuwa wajasiriamali wa kimataifa halafu vijana wa kitanzania wanakalia kununua simu za mikononi kwa ajili ya umbeya wa facebook na instagram.

Inachukiza sana kuwaona vijana wa afrika ya magharibi wakijiunda kwenye vikundi ili waweze kupata mikopo mikubwa kutokana na mawazo yao ya kibiashara, halafu vijana wa kitanzania wamekalia majungu ya kina Mange Kimambi na wengine wasio na adabu.

Vijana wa kitanzania wanasubiri matukio ya wanasiasa ili wapate cha kuongea na kujadili kwenye makundi wa whatsapp wakati huo huko Nigeria vijana wa rika lao wanaumiza vichwa ili waingie kwenye kundi la wajasiriamali wa kesho wa bara la Afrika.

Ni kweli tunao kina Mohamed Dewji, Reginald Mengi na Mzee Bakhresa, lakini hawa bado hawajawa na msukumo mkubwa kwa kundi la vijana ambalo halioni aibu kuishia kwenye mijadala ya kisiasa badala ya kuhangaikia ubunifu wa kwenye ujasiriamali.

Wakati sisi watanzania tunaendekeza kejeli za kitoto kuhusiana na dunia ya viwanda, huko Nigeria watu wanaumiza vichwa ili kufaidika na teknolojia inayobadilika kila kukicha.

Hizi kejeli za mitandaoni na upuuzi mwingine wa kitoto, ni vitu ambavyo haviwezi kuwasaidia vijana wa Tanzania.
 
vijana wa hapa nyumbani hatupendi kazi wala wanaotuambia tufanye kazi. tunaota utajiri wa kuibuka kama uyoga ambao huo haupo hapa duniani.
 
Mange anawaumiza sana watawala, na bado. Hukuwezi kuwa na ujasiriamali ktk utawala unarudisha maisha watu nyuma kwa kuwabomolea nyumba zao, kwa kodi kubwa na za kukomoana, kwa vitisho kwa wawekezaji ( rejea kilio cha Dangote), wakubwa kibiashara wanalia je hao wa kuinukia je!?

Lazima msemwe ili muache uonevu ndio tufanye biashara
 
Na pia sisi wenyewe vijana tuna majungu balaa.
ontario kuna kipindi fulani alikuwa anaelezea alivyopambana hadi akafanikiwa kama kijana lakini angalia Majungu hayo.
Juzi hapa kaleta fursa ya forex ndo balaa tupu watu wamezidisha majungu
 
Mkuu akili zako ndio zile zile za walalamikaji. Unataka kuniambia vijana wanafaidika na mradi wa ujasiriamali wa Olumelu wanatoka kwenye nchi zinazoongozwa na malaika?.

Ukiwa mtu wa kuhesabu vikwazo pasipo kuangalia fursa zilizomo ndani ya vikwazo hivyo, basi tegemea kufa ukiwa masikini mwenye kipaji cha kulalamika.
 
vijana wa hapa nyumbani hatupendi kazi wala wanaotuambia tufanye kazi. tunaota utajiri wa kuibuka kama uyoga ambao huo haupo hapa duniani.
Matokeo yake uvivu wetu unakuwa ukituambia kwamba chanzo cha umaskini wetu ni mtu fulani aliye madarakani.

Katika hali kama hii, kila rais atakayekuwa pale magogoni atabebeshwa zigo la lawama.
 
Ni TONY ELUMELU ** INfact jamaa yuko vizuri sema hata vijana wa hapa kwetu tusiwalaumu sana mkuu Philip Kwakuwa hata Taasisi zetu za Elimu somo la Entrepreneurship ni ndoto ndio maana vijana wanakosa morali.
 
Tatizo lenu mmebakia kufanya mambo Kwa mdomo na syo watendaji

Ova
 
Hivi vijana wa Nigeria sio ndo walikuwa wameanzisha movement ya kumtaka Raisi wao aachie madaraka kwa lazima au vijana gani wa Magharibi unazmgmzia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…