Bahlul na harun kwenda kuoga pamoja

Bahlul na harun kwenda kuoga pamoja

KABAVAKO

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
229
Reaction score
32
Ilitokea siku moja Bahlul na Harun Rashid kukutana katika bafu. Khalifa alimfanyia mzaha kumwuliza Bahlul: "Je iwapo ningalikuwa mtumwa, ningalikuwa na thamani gani?" Bahlul alimjibu: "Dinar hamsini." Harun Rashid katika kughadhabika alisema: "Ewe Mwehu! itawezekanaje hivyo? Mavazi yangu tu yamezidi thamani hiyo!” Hapo Bahlul alimwambia: "Kwa hakika mimi nimesema kuwa hiyo ni thamani ya nguo zako tu ama Khalifa hana thamani yoyote!"
 
Back
Top Bottom