Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,925
Matajiri wakubwa nchini ambao ni Rostam Azizi, Regnald Mengi, Mo na Bakhresa, katika kusoma historia ya maisha yao na jinsi walivyoanza kutajirika naelekea kuvutiwa zaidi na huyu Bakhresa ambaye kwa kweli ni sawa na kuanzia umachinga baada ya kuacha shule akiwa na umri wa miaka 14, na kwa umri huu dhahiri ni kama kiwango cha elimu ya msingi.
Mtaji wa kuuza Mbatata
Kwa umri aliokuwa nao wa miaka 14 kuamua kuacha shule na kufanya biashara ya kununua viazi vitamu kwa wakulima huko njiani na kupakia kwenye magari kidogokidogo kuleta kuuza Kariakoo na maeneo mengi ni jambo ambalo limo ndani ya uwezo wa walio wengi kati yetu. Hatua iliyofuata ya kuanzisha mgahawa dhahiri alifanikiwa kukuza mtaji huo wa kuuza mbatata, hatua ambayo ilisaidia kuwa na mapato zaidi yaliyomsaidia kufikia uamuzi wa kununua vinu vya kusaga nafaka vya kawaida tu kama wengi wafanyavyo. Serikali ilipokuwa bin taabani kushikilia mashirika ya umma, iliamua kulegeza kamba kuruhusu wazawa kuyanunua, ndipo Bakhresa alipoamua kununua vinu vya shirika la National Milling Corporation mradi mbao aliuendesha kwa ufanisi mkubwa hadi kufikia hatua ya kuwa na mitambo ya utengenezaji ice cream, pipi, vinywaji baridi, biasha ya madini nk. Hatua nyingine umiliki wa timu ya mpira ligi kuu taifa jambo la pekee katika nchi yetu ingawa ni jambo la kawaida katika nchi zilizoendelea kwa kampuni iliyopiga hatua kubwa kiuchumu. Kati ya matajiri wakuu wanne hawa, yeye pekee ndiye anayetoa ajira kubwa kwa vijana nchini.
Kwa kuangalia historia hii ya huyu Bakhresa dhahiri wengi tunaweza kujifunza kwake, kwano MO ametajirishwa na urithi wa wazazi wake, Mengi kazi ya uhasibu aliyofanya UK na Tanzania na hivyo kuna na upenyo wa kufikia alipo, na Aziz sina cha kuongeza kwani mengi yalishaandikwa hapa yanajulikana.
Njia za huyu Bakhresa nasema pametulia naweza kujifunza na kujaribu bahati yangu.