BAKWATA, huu utaratibu gani? Dodoma kuna Sheikh wa Mkoa, kwanini Sheikh wa Mkoa wa DSM anatuingilia kuja kupiga dua hafla za Serikali?

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Ninajua Sheikh wa Mkoa was Dar es Salaam alizoea kualikwa katika hafla mbalimbali za kitaifa na pengine alikuwa anafaidika kinamna fulani, sasa anaelekea kuvuka mipaka.

Mamlaka yake yanaishia Dar es Salaam lakini inaonekana uamuzi was kuhamia Dodoma ulimuumiza sana sasa kaamua kuvamia hafla za Viongozi /Serikali hapa Dodoma. Ina maana Dodoma hakuna Sheikh wa mkoa? Kwa nini huyu was Dar es salaam aje Dodoma?

Hizi ni chokochoko, tunaomba BAKWATA Dodoma wakatae, kama ni posho wote tunazitaka, was DSM mlizila sana kipindi serikali iko DSM, sasa ni zamu yetu

N.B

Alhaji Mussa leo yuko Dodoma katika hafla ya siku ya mazingira Duniani
 
Kusoma Duwaa kwani kunakulipwa?

Mnalumbana kwa sababu ya Kusoma Duwaa!!

Punguzeni maneno maneno yasiyofaida
 
HUYO JAMAA WA DAR KIUKWELI AMETUKWAZA SANA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ILOPITA,Alikuwa katibu mwenezi wa CCM badala ya kukemea.
Yupo na yule MALASUSA hawakusimama kiimani Bali walikuwa kimaslahi ya chama.
Umewahi kujiuliza Kwa nini huwa wanaenda kupiga Kura?
 
Hukusikia akijiita Shee Mkuu wa Mkoa...!!!
 
Huyo ni sheh mkuu wa mikoa yote basi

Ova
 
Huyo shekhe wa Dar anapenda sana kuhudhuria hafla ili ale ubwabwa. Ndiyo maana akabatizwa jina la "shekhe ubwabwa".

Ana kinywa kichafu utadhani siyo mtumishi wa Mungu. Unakumbuka maneno ya shombo aliyomtwmkia shekhe Mohamed wa channel ten??
 
Huyo shehe dili la kuimba kwaya na kuandaa makongamano ya kumtukuza jiwe kwa malipo ya bahasha ya kaki limekufa.Hivyo ni lzm abuni njia nyingine
 
Atusikii tena viongozi wa dini wakiandaa makongamano kulikoni tena
 
Hizi ni chokochoko, tunaomba BAKWATA Dodoma wakatae, kama ni posho wote tunazitaka, was DSM mlizila sana kipindi serikali iko DSM, sasa ni zamu yetu
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜‹
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…