BAKWATA ifuate mfano wa KKKT

Katika Taasisi zenye kuwarudisha nyuma waislamu katika azma yao ya kupata usawa katika jamii hii ni BAKWATA.

Viongozi wakubwa wa BAKWATA wakishapata vimaslahi vichache kutoka kwa watawala basi hawajali kabisa mustakbali mpana wa waumini wa dini yao nchini.

BAKWATA kazi wanayoifanya ni kuwapa watawala moral authority hata pale wanapopaswa kunyooshewa vidole kwa matendo ya udhalimu
 
Mliongea nao lini tarehe ngapi na wapi hao waumini wao? Minute ziko was za kikao na za majina ya waliohudhuria hicho kikao Cha kuwaunga mkono? Mwenyekiti wa kikao alikuwa Nani na katibu alikuwa Nani?

Hao waumini wa kushukiwa akili na viongozi wako wapi miaka hii?
 
Mohamed Said anasemaje juu ya kadhia hii?
Hatua gani amechukua?

cc. Mohamed Said
 
Ndie baba wa Taifa na alilenga kudumisha uzalendo kama ilivyo China, Russia au suudia dini zote zinadhibitiwa kwa maslahi mapana ya Taifa. Huyo binti uliyemuweka ktk avatar Anamengi kisa ni kushindwa kudhibiti hizi dini
Kudhibiti akili za watu sio sawa na kudhibiti mifugo
 
Mliongea nao lini tarehe ngapi na wapi hao waumini wao? Minute ziko was za kikao na za majina ya waliohudhuria hicho kikao Cha kuwaunga mkono? Mwenyekiti wa kikao alikuwa Nani na katibu alikuwa Nani?
Viongozi wao ni wanufaika waumini si wanufaika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…