Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), limesema Sikukuu ya Eid el Adh’haa itakuwa Jumatatu Juni 17 na swala yake itaswaliwa katika msikiti wa Mohamed VI uliopo makao makuu ya baraza hilo Kinondoni.
Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Juni 8, 2024 na Katibu Mkuu wa Bakwata, Alhaji Nuhu Mruma swala ya Eid itaanza saa moja asubuhi ikifuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika pia katika msikiti huo.
“Kwa niaba ya Bakwata, Mufti na Sheikh mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir anawatakia maandalizi mema ya sikukuu hiyo,” amesema Alhaj Mruma katika taarifa hiyo.
Eid El Adh’haa ni sikukuu inayoadhimishwa baada ya waumini wa Kiislamu kukamilisha ibada ya Hijja ambayo ni nguzo ya tano katika nguzo za dini.
Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Juni 8, 2024 na Katibu Mkuu wa Bakwata, Alhaji Nuhu Mruma swala ya Eid itaanza saa moja asubuhi ikifuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika pia katika msikiti huo.
“Kwa niaba ya Bakwata, Mufti na Sheikh mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir anawatakia maandalizi mema ya sikukuu hiyo,” amesema Alhaj Mruma katika taarifa hiyo.
Eid El Adh’haa ni sikukuu inayoadhimishwa baada ya waumini wa Kiislamu kukamilisha ibada ya Hijja ambayo ni nguzo ya tano katika nguzo za dini.