BAKWATA yawataka Watanzania kukataa ndoa za jinsia moja, Mufti ashangazwa wanaume kulawitiana ilhali wanawake wa kuolewa wapo

BAKWATA yawataka Watanzania kukataa ndoa za jinsia moja, Mufti ashangazwa wanaume kulawitiana ilhali wanawake wa kuolewa wapo

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mufti wa Tanzania, Abubakar Zuberi ameshangazwa na watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja kutokemewa lakini badala yake wanalindwa na kutafutiwa uhalali wa ndoa akiwataka Watanzania wote kulaani na kukataa ndoa za jinsia moja nchini. Mufti alitoa hadithi ya nabii Lut ambapo jamii yake ilishiriki vitendo vya jinsia moja na miji yao kupinduliwa juu chini.

Mufti amesikitishwa na wanaume kuingilia wanaume wenzao ilhali wanawake wapo akidai ni muujiza mkubwa watu hao leo kupewa nafasi na kuwa huru ikionekana jambo la kawaida. Mufti anasema si sawa vitendo hivyo kufundishwa mashuleni.

 
Warumi 1:24
Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.

Warumi 1:25
Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.

Warumi 1:26
Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

Warumi 1:27
wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

Warumi 1:28
Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

Warumi 1:32
ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.
 
Sheria za kijinga za ubakaji zinazo tungwa na tamwa na bunge letu ndiyo zina sababisha athari za kisaikolojia kwa watoto na kuamuq kufanyiana ushoga wakiume wao kwa wao
 
Sheria za kijinga za ubakaji zinazo tungwa na tamwa na bunge letu ndiyo zina sababisha athari za kisaikolojia kwa watoto na kuamuq kufanyiana ushoga wakiume wao kwa wao
TAMWA huwa wanakurupuka tu, ni waharibifu wa maadili ya ndoa
 
Kakurupuka, anatoa taarifa kana kwamba jambo hili limeibuka ghafla wakati lipo kitambo tu, too late wamechelewa. Ulawiti na ufiraji uliipuuzwa kufundishwa wakati maandiko yapo wazi kukemea watu wakawa wanajiwekea mistari yao kufarijiana na kuhubiriana baraka tu kwenye maliturijia yao waliyopanga yafundishwe nchi nzima mstari mmoja tu
 
TAMWA huwa wanakurupuka tu, ni waharibifu wa maadili ya ndoa
Mara mume kumbaka mke wanataka kupora mali za waumezao kwanjia ya kuwafunga maisha badala ya njia ya kuwaua maana wamegundua ina wa cost sana, sasa wanataka kuwe na ubakaji baina ya wanandoa ili kufikia tamaa zao za mali....hii ndiyo ina sababisha watu kukataa ndoa na harakati za hivyo na ushoga
Tena walivyo wapumbavu hao tamwa wanadhani hizo sheria wanazo zisukuma zita waacha wao na watoto wao salama ...maana watoto wao wakiume ndiyo watakao fungwa jela na wake zao waovu kwa tamaa za mali
 
Haya majimama kwa usomi wao na kuishi bila waume wana impose ujinga na kuporomosha maadili ya ndoa. Kwanza yenyewe yanazaa watoto na kulea wenyewe bila baba matokeo yake ndiyo haya madhara ya watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili. Hawa wasomi wanakosa agenda za maana wanaanza kuingilia mambo nyeti ya kijamii kama ndoa kwa kubomoa misingi yake. Wameharibu mila na desturi za jamii zilizojiwekea kulinda maadili yao ya ndoa kwa kuendesha kampeni za ajabuajabu na kusabisha kutungwa kwa sheria za aibu. Leo mambo yameharibika hawana pa kujificha wamebaki kutatapa na kutafuta wa kumtupia lawama
 
Namaanisha huko hivi vitendo vimekithiri sana
Nashangaa umenishambulia

Kikawaida Jambo lolote liwe zuri ama baya mara nyingi huanzia maeneo ya mijini na baadae kusambaa maeneo mingine. Kwa TZ haliwezi pingika kuwa Maeneo ya Pwani ndio maeneo yaliyotangulia ustaarabu na maendeleo kiujumla, Kwa hiyo hata adoption za mambo mabaya ni wazi yataanzia huko. Hilo halina mahusiano yoyote na Uarabu wala Uzungu bali ni athari za utandawazi.
 
Back
Top Bottom