Ballon d'Or 2019: Lionel Messi ashinda tuzo ya sita ya Ballon d'Or awabwaga Virgil Van Dijk na Cristiano Ronaldo

Mchezaji Lionel Messi amfanikiwa kunyakua tuzo ya sita ya Ballon D' or zilizofanyika usiku huu Jijini Paris, nafasi ya pili kinyang'anyiro hicho imeenda kwa mchezaji Van Dijk, huku mchezaji Cristiano Ronaldo akishikilia namba tatu.

Aidha katika tuzo hizo mchezaji Matthijs de Light ameibuka mshindi wa tuzo ya mchezaji bora kijana huku Jadon Sancho akishika nafasi ya pili na Joao Felix akishika nafasi ya tatu.

kwa upande wa tuzo ya kipa bora imeenda kwa Allison Becker anayekipiga kunako timu ya Liverpool huku nafasi ya pili ikienda kwa Ter Stegen na nafasi ya yatu ikienda kwa Ederson.

aidha, Ballon D or kwa upande wa wanawake imeenda kwa mchezaji Megan Rapinoe ambaye ni raia wa Marekani.

Je, wamestahili?
 
Reactions: PNC
Mchezaji wa kipekee wa soka wa Argentina na Klabu ya Barcelona Lionel Messi aka La Pulga ametwaa tuzo yake ya sita ya Ballon d'Or na kuweka rekodi mpya ya dunia.

Messi anakuwa mchezaji wa kwanza tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kugunduliwa kwa mchezo wa soka na tuzo zake kutwaa tuzo sita za Ballon. Messi amewabwaga Dijk,Ronaldo na Sadio Mane.

King Messi tena...viva La Pulga!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…