Ballon d'or vs FIFA best player of the year

Astej

Member
Joined
Apr 2, 2018
Posts
22
Reaction score
6
Habari wadau. Hivi kuna tofauti gani kati ya tournaments mbili hapo juu?
 
Habari wadau. Hivi kuna tofauti gani kati ya tournaments mbili hapo juu?
Mkuu zamani kabla enzi za kina Messi na Ronaldo kulikuwa na Tuzo mbili za mpira, FIFA Best Men player of the year na Baloon D or.

Tuzo ya FIFA ilikuwa inamilikiwa na FIFA Wenyewe na Baloon D or inamilikiwa na shirikisho la ufaransa.

Baadae mwaka 2010 Kama sijakosea wakaunganisha hizi tuzo ikawa Tuzo moja inaitwa FIFA Baloon D or.

Mwaka 2016 zikatenganishwa Tena kutokana na FIFA kutaka kuongeza mahusiano Yao na Uingereza, hivyo ufaransa wakaendelea na Baloon D or Yao na FIFA nao wakaendelea na Best player Yao.

Sema FIFA Best player of the year ya Sasa Ni tofauti na ya zamani, maana nao wanapiga kura, hivyo jina halisi inatakiwa iitwe FIFA Popular player of the year na sio Best player of the year, maana hata ukicheza vizuri kiasi gani Kama sio maarufu huwezi shinda hii tuzo.
 

Mkuu Fifa wanapiga kura tokea uasili wake. Na wanaopiga kura ni makocha wa timu za taifa pamoja na macaptain. Na baloon D'or wanaopiga kura ni waandishi wa habari.

Hizi zote ni Popular awards tu, Ushindi hauhusiani na ubora bali umashuhuri. Lakini nashindwa kuwafahamu walimwengu wanaopima ubora kwa kupitia hizi tunzo.

Just imargine mpaka hii leo bado marcello unamkuta ndani ya eleven ya Dunia ya kila mwaka. Na Alves nahisi amekosekana mwaka huu tu.
 
Sasa Hivi waomeongeza na wadau wengine wa soka yaani Mashabiki, kila kundi kura zake zinachangia asilimia 25 yaani makocha, wachezaji (macaptain), waandishi wa habari za michezo na Mashabiki.

Hio ya Mashabiki kuingizwa Ni mpya imeanzishwa 2016 zamani haikuwepo, na pia zamani waandishi wa michezo waliohusishwa Ni wachache Sana wale wenye hadhi, siku hizi mpaka vijarida vya uchochoroni vinapiga kura.
 
Asante sana chief! Kwa maana hiyo basi, FIFA Best Men player ina value kubwa kuliko Ballon d'or!
 
Habari wadau. Hivi kuna tofauti gani kati ya tournaments mbili hapo juu?


Pole sana kamanda...Fifa na ballon ni vitu viwili tofauti...kama unasubiri Cr7 au vidjik apewe imekula kwako kamanda...haki ya mtu haipotei bure bure...


Mara nyingi kujadili na waswahili ni kupoteza muda tu, mswahili anajiona anajuwa kila kitu kuhusu tuzo hizi, baada ya Messi kuwagaragaza wenzie povu limewatoka utafkiri ndio mara yake ya kwanza kuchukua tuzo hizi...alafu inakuja hapa kuilalamikia fifa eti haiwatendei haki wachezaji utafkiri wao ndio wapiga kura 😀😀 sometimes elimu inamtoa mtu ujinga..
 
hii ni tuzo ya kwanza ya messi ya Fifa toka irudishwe hajawahi kuchukuwa,
 
Asante sana chief! Kwa maana hiyo basi, FIFA Best Men player ina value kubwa kuliko Ballon d'or!
kwa zamani ndio ilikuwa na hadhi kuliko Baloon d or, ila kwa sasa Baloon d or ni maarufu zaidi.
 
kwa zamani ndio ilikuwa na hadhi kuliko Baloon d or, ila kwa sasa Baloon d or ni maarufu zaidi.

Mkuu Fifa haijawahi kuwa na hadhi zaidi ya ballon, Tunzo yenye ya Fifa ilianzishwa 1991 wakati Ballonipo tokea 60's huko.
 
Mkuu Fifa haijawahi kuwa na hadhi zaidi ya ballon, Tunzo yenye ya Fifa ilianzishwa 1991 wakati Ballonipo tokea 60's huko.
It doesn't matter mkuu, tuzo Bora ya mchezaji wa Dunia ilikuwa Ni Ya FIFA na sio Baloon D or.

Kama huufahamu Baloon D or ilikuwa haijumishi Dunia nzima ndio maana Maradona, Pelle etc hawana Baloon D or, ili ushinde Baloon D or ilikuwa Ni lazima utoke ulaya na uwe unachezea ulaya.

Mwaka 1995 ndio kwa Mara ya kwanza Baloon D or ikajumuisha Dunia nzima ambapo kipindi hicho tayari FIFA Ina miaka 4 ya tuzo.

Leo ukisikia Zidane ana uchezaji Bora Mara 3, Ronaldo de Lima Mara 3 sio Baloon D or zile Ni tuzo za FIFA.

Na hata angalia washindi wa Baloon D or wa zamani sio actual wachezaji Bora wa kipindi hicho, mfano Kipindi Madrid inatawala na wachezaji wa Dunia Wanatoka kwao Hawa Ni washindi wa FIFA vs Baloon D or.

Mwaka 2001 mshindi wa FIFA Ni Luis Figo wakati Baloon D or Ni Michael Owen ambaye hajashinda ligi Wala Uefa.

Then Zidane alivyochukua 2003 kwa kukichafua champions league na ligi ya Spain Baloon d or alibeba Pavel Nedved.

Wakati ronaldinho anakiwasha 2004 Barcelona Dunia nzima tunamjua Kama Ni Bora na anapewa tuzo ya Uchezaji Bora wa FIFA Baloon D or anashinda Andrei schevchenko na wa Pili Deco

Mkuu hio mifano mitatu inatosha kuonesha Baloon d or ilikuwa Ni Tuzo ya ajabu toka zamani na haikuwa maarufu kuliko FIFA na siku zote ilikuwa Ni popularity contest, hii tuzo imepata Umaarufu zaidi baada ya kumerge na ya FIFA, Ila zamani ya FIFA ilikuwa Ni maarufu zaidi.
 

Upo Bongo halafu unaizungumza Dunia nzima. Ndoto za wachezaji wote Ulaya ni kushinda Ballon D'or na si FiFa. Fifa walishindwa moja kwa moja kuiangusha tunzo ya Ballon D'or kihadhi na ndio walipotumia kila mbinu mpaka wakaimeza. Na baada ya Blatter kupotea tu tu Ballon wakafanikiwa kujimegua.

Mkuu Dunia ya Football ipo Ulaya, Unapokua mchezaji bora wa ulaya maana yake ndio Dunia nzima. Kigezo cha kua haikujumuisha wachezaji wa nje ya ulaya pre 95 sio hoja nzito kabisa, Bado Fifa wanabakia kua wameanzisha tunzo 1991 na ni juzi tu.

Na Ballon D'or walishatangaza washindi wapya wanyuma wamiaka yote ambaye tunzo zilikua kwa wachezaji wa ulaya tu.

Halafu mkuu punguza mihemko, Zidane 2003 alikichafua nini? Unaukumbuka huo mwaka vizuri lakini? Hebu niambie kati ya Zidane na Nedved nani alikichafua?
 
Mbona Hili linajulikana Sana Tu, mwaka Jana pia Modric alipewa kura feki kibao, Kuna jarida limefungwa toka 2012 na website Yao IPO offline lilipiga kura, Kuna jamaa wa Trinidad and Tobago pia kura zake zinaonesha amempigia Modric wakati mwenyewe anakataa.

Mimi japo Siwapendi Liverpool lakini Mane anadesrve atleast top 3 misimu yote hii miwili. Na mwaka Huu bila Shaka van Djik alitakiwa apewe tuzo.
 

Siungi mkono ushindi wa Messi kwa VVD lakini, Mane na Alison walideserve more kuliko VVD
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…