Baloteli aiweka kileleni Nice Ligue 1

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Mshambuliaji wa kiitaliano Mario Baloteli aka Super Mario jana alifunga mara mbili na kuisaidia timu yake ya Nice kukwaa kileleni mwa Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) kwa kufikisha alama 14 katika michezo 6. Nice inafuatiwa na PSG yenye alama 13.

Nice ilipata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Monaco wanaoshikilia nafasi ya 3 wakiwa na alama 13. Wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wa Allianz Riviera, Nice waliwapoteza Monaco katia kila idara. Baloteli alifunga mabao yake katika dakika za 30 na 69 za mchezo huo.
 
Akianza kung'aa wazungu wanamchukua wanaenda kumkalisha benchi kiwango kinatulia
 
Balloteli ni mchezaji mzuri sana, ila baadhi ya makocha hawataki kumuelewa na hivyo kumtreat kama mtoto kitu ambacho hakipendi. Anaweza akafanya vizuri sana mwaka huu pale Nice timu za EPL au hata La Liga zikaanza tena kummezea mate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…