Balozi wa Marekani awapongeza polisi kwa kuhitimisha kifo cha muuaji katili

Balozi wa Marekani awapongeza polisi kwa kuhitimisha kifo cha muuaji katili

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
US.PNG

Naomba kuungana na Balozi wa Marekani Nchini kwa pongezi alizotoa kwa jeshi letu, kweli walifanya kazi stahiki kwa wakati.

Zipo clip zinadai askari mmoja aliyevaa kiraia nusura ashambuliwe na wenziwe, niwapongeze wananchi waliopaza sauti kuzuia polisi kushambuliana.

Lakini pia niwapongeze wananchi kwa kuweza kuzuia msafara uliokuwa unaelekea eneo la tukio, naamini tukiwekeza kukuza imani ya wananchi kwa ujasiri wao waliofanya eneo la tukio wa kuzuia vyombo vya dola baadhi ya action, lakini pia wamekuwa wepesi Sana kuweka kumbukumbu za tukio hilo kwa ujasiri mkubwa kwa ushirikiano huu tutailinda Tanzania.

Mhe. Rais hongeza juhusi kwenye community police, elekeza kufutwa kwa kesi zinazoligawa Taifa viongozi muishi kwa ushirikiano kama wanavyoishi wananchi. Ujachelewa, tumia tukio hili kuwekeza kwenye police jamii huku ukiruhusu Uhuru wa siasa na usimamizi wa haki itasaidia Sana ufichuaji wahalifu.

Otherwise niwapongeze Askari wote walioshiriki tukio like wameonyesha Dunia kwamba Tanzania tunaweza kurespond na kufanya kazi. Mhe. Rais Waite Hawa vijana wape zawadi ikiwezekana ya vyeo kutoa motisha kwa wengine, waombee nafasi za mafunzo nje waimarike zaidi na kujifunza ni hazina kwa Taifa
 
Ndugu tuendelee kusubiri habari au? maana kichwa cha Habari Juu ya Wamarekani kupongeza haviendani na habari yenyewe! Wapi amepongeza huyo balozi wa America?
 
Mungu awabariki wote waliojitoa kusaidia kuntuliza muhalifu na pia awalaze marehemu wote mahala pema peponi Amen.
 
Wakati tunatoa pole na rambirambi kwa Jeshi la polisi na ndugu wa askari waliofariki katika tukio la jana. Lakini Jeshi letu la polisi, lijitakari, liongeze umakini na weledi kazini,haingii akilini,raia mmoja awanyang'anye silaha askari wawili, waliziweka wapi?

Silaha huruhusiwa kuiacha hovyohovyo. Askari wenye weledi wanapokuwa kazini wanakuwa wangalifu na makini, lakini siku hizi, unaweza kuona askari wanaongea na simu za mikononi au wanachat wakati wa kazi,tusipokuwa makini, kitatekwa kituo cha polisi siku moja.
 
Pamoja na pongezi hizo,

Mi naona kulikuwa na mapungufu kidogo KWA Askari wetu.

Mtuhumiwa alikuwa mmoja,Amefanikiwaje kuua Askari wengi kiasi hicho?

Amefanikiwaje kudumu KWA MUDA mrefu akitawala eneo Hilo bila kushughulikiwa KWA upole?

Na kwanini hawakumlenga miguu ili akamatwe akiwa hai ili baadaye wambembeleze KWA upole kutoa maelezo vzr ikiwemo kuwataja wenzake na kumpima AKILI ili tujue mbivu na mbichi?

USHAURI: Polis wawe wanahudhuria mafunzo ya kulenga shabaha Mara KWA Mara.Mafunzo ya kutumia silaha iwe ndo chai yao ya asubuhi.

Dunia ya Leo imebadilika.Watu wamekuwa makatili na roho mbaya.

Zamani Askari mmoja alikuwa na uwezo wa kukamata wahalifu Hata kumi na akawaamrisha wafungane mashati wenyewe KWA wenyewe.

LAKINI Leo mtuhumiwa mmoja anapambana na Askari Hata wakiwa Askari wawili LAKINI anagoma kukamatwa.Watu mioyo yao imekengeuka.

LINGINE,Askari wetu wanapokuwa na silaha wawe makini na watu wanaopita karibu yao.Huyu muuaji sijajua aliwataimu vipi hao Askari Hadi akawaua wote hao pasipo yeye kuvunjwa miguu?

NA LA NWISHO, Askari wapate MUDA wa kumpumzika.wasikae MUDA mrefu na silaha bila kuja kubadilishwa. Wakikalishwa Kwenye lindo MUDA mrefu na silaha Ni hatari MWISHO wa SIKU wanachoka wanaweza Hata kusinzia wale nao Ni binadamu Kama sisi.Usingizi hauna shujaa.

MWISHO,Uchunguzi ufanywe KWA umakini mkubwa KWA kuanza na kutrack Simu ya mtuhumiwa ,Historia ya mtuhumiwa,Rekodi zake hospitalini,Aina ya marafiki zake,Mke au mvhumba wake, Alifikaje hapo Kwenye tukio? CCTV Camera za maeneo hayo Polisi wachunguze , Silaha aliipataje? AU alikuja nayo? Alikuwa anaimiliki kihalali au kimazingaombwe TU?
Mtuhumiwa anaonekana Ana asili KAMA ya kisomali Je uraia wake ukoje?

ZAIDI YA YOTE,MSAKO NCHI NZIMA RAIA WOTE WA KIGENI WAKAGULIWE UHALALI WA URAIA WAO.WAONESHE VIBALI VYAO NA WAPO NCHINI KWA SHUGHULI ZIPI.

MSAKO KWA WANAOMILIKI SILAHA NAO WAKAGULIWE UHALALI WA UMILIKI WA HIZO SILAHA NA IKIWEZEKANA WAWE WANAPIMWA AKILI KILA BAADA YA MWEZI AU MUDA FULANI.HUYU ALIYEUA ASKARI WETU HAKUNA ANAYEJUA ALICHANGANYIKIWA AU ILIKUWAJE? PENGINE UCHUNGUZI UTAKUJA NA MAJIBU MAZURI ILA NI VZR WAMILIKI WA SILAHA WAWE WANAPIMWA AKILI MARA KWA MARA.

Tuwaombee Askari wetu Mungu awalaze mahali pema peponi Amina.Poleni wafiwa .Msiba huu Ni wetu sote watanzania Wala Siyo was Askari peke yao.Tuendeshe ibada kuwaombea Askari wetu hawa pamoja na RAIA waliouawa bila hatia yoyote.

Raha za milele uwape we bwana na mwanamke was milele uwaangazie wapumzike KWA amani
Amina.
 
Wakati tunatoa pole na rambirambi kwa Jeshi la polisi na ndugu wa askari waliofariki katika tukio la jana. Lakini Jeshi letu la polisi,lijitakari,liongeze umakini na weledi kazini,haingii akilini,raia mmoja awanyang'anye silaha askari wawili, waliziweka wapi? Silaha huruhusiwa kuiacha hovyohovyo .Askari wenye weledi wanapokuwa kazini wanakuwa wangalifu na makini,lakini siku hizi,unaweza kuona askari wanaongea na simu za mikononi au wanachat wakati wa kazi,tusipokuwa makini,kitatekwa kituo cha polisi siku moja.
Ni kweli,Wajitahidi kuongeza umakini .

Mafunzo ya shabaha iwe ndo chai yao asubuhi.

Wasikalishwe na silaha MUDA mrefu bila kubadilishwa.

WAMILIKI wasilaha wawe wanakahuliwa VIBALI VYAO Mara KWA Mara.

WAMILIKI was silaha wapimwe AKILI Mara KWA Mara.

WAMILIKI was silaha wafuatiliwe nyendo zao Mara KWA Mara.
 
Back
Top Bottom