Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Hafla hiyo ambayo imefanyika jana usiku nyumbani kwa balozi huyo golikipa namba moja nchini Aishi Manula alikabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Disemba wa klabu ya Simba.
Mbali na tuzo ya Manula wachezaji wengine walikabidhiwa medani za kuwa wachezaji bora wa mechi nne zilizopita ambao ni nahodha John Bocco ambaye aliibuka mchezaji bora wa mechi dhidi ya Ndanda FC.
Mwingine ni kiungo Said Ndemla aliibuka mchezaji bora wa mechi ya Simba SC dhidi ya Kagera Sugar iliyopigwa mkoani Kagera na Ndemla kufunga bao moja pamoja na kusaidia jingine moja kwenye ushindi wa mabao 2-0.
Hafla hiyo maalumu iliandaliwa na ubalozi wa Uturuki kwa ajili ya kujenga na kuimarisha uhusiano mzuri kati ya Klabu ya Simba na nchi ya Uturuki.