Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,278
- 797
Balozi wa Tanzania Nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Precision Bw. Patrick Mwanri ambapo wamezungumzia namna bora ya kuongeza wigo wa usafiri wa anga baina ya Tanzania na Visiwa vya Comoro.
Katika mazungumzo hayo Balozi Yakubu ambaye anajiandaa kwenda kuanza kazi katika eneo hilo la uwakilishi alipokea maelezo ya safari za anga ambazo Shirika la Precision hufanya baina ya Visiwa hivyo na Tanzania mara mbili kwa wiki na pia fursa ambazo bado zipo katika sekta hiyo hasa kwa kuwa Tanzania na Comoro ni washirika wakubwa wa kibiashara.
Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Bw. Christian Shirima, Meneja miradi wa huduma kwa wateja.
🗓️ 08 Mei, 2024
Katika mazungumzo hayo Balozi Yakubu ambaye anajiandaa kwenda kuanza kazi katika eneo hilo la uwakilishi alipokea maelezo ya safari za anga ambazo Shirika la Precision hufanya baina ya Visiwa hivyo na Tanzania mara mbili kwa wiki na pia fursa ambazo bado zipo katika sekta hiyo hasa kwa kuwa Tanzania na Comoro ni washirika wakubwa wa kibiashara.
Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Bw. Christian Shirima, Meneja miradi wa huduma kwa wateja.
🗓️ 08 Mei, 2024