Mpendanchi-2
JF-Expert Member
- Apr 4, 2009
- 304
- 38
mkuu pundamilia inaonekana una bahati sana au unafahamika, suala la bandarini lina mauzauza mengi kwenye utoaji wa mizigo, tena iwe wewe ni mchukia rushwa (haupo tayari kutoa rushwa) ndio utalijua jiji, kwakweli kwa bongo gharama ya kutoa gari ni kubwa zaidi ya ile uliyonunulia na kusafirisha,
nina jamaa yangu alitaka kuiacha gari yake bandarini, kwa gharama alizoambiwa, mpaka alipolazimika kutoa chochote ndio wakamshushia gharama, sijui kama wamejirekebisha jana au juzi nikiwa namaana hii 2009!!
Tatizo bado lipo pale pale, tumekupa njia zinazotakiwa na mifano ya sisi tuliowahi kufanya hivyo . Ni kwamba ukifuata taratibu kama zilivyo bila ku forge chochote na kutomsikiliza the so called agent kwenye mawazo yake ya kutaka kukushauri kufanya forgery, Utafanikisha within no time.
Hata kama utakuta kumefanyiwa Uplifting ya price kama kweli ndiyo gharama halisi uliyonunulia wana kitengo pale unakwenda unatoa malalamiko yako, watakuuliza upeleke document zote original ulizoanza mawasiliano, email zote, na pay slip uliyotuma pesa!! Hapo ndipo huwa kimbembe kwa wale walio forge kwani pay slip ina gharama ingine na document zina gharama ingine. Hivyo mtu kama huyo akitoka hapo lazima atabaki kutukana na kulalamika, Lakini hatasema tatizo ni yeye.