Kuna aina 2 za mikopo zinazotolewa bank,moja mkopo wenye dhamana ya vitu na pili usio na dhamana ya vitu lakini kazi yako ndo inakuwa ni dhamana,katika hii aina ya pili kuna namna 2,aidha mwajiri anakata moja kwa moja kisha yeye ndo anapeleka bank au mshahara unapitia bank husika kisha wao bank ndo wanakata chao.
Ili uweze kupata mkopo yapo mambo mbalimbali yanazingatiwa mojawapo ni kupata taarifa ya kibank kutoka bank nyingine hasa kama umekuwa kwenye bank B chini ya miezi 6,na hii hufanyika kwa kumuomba mteja alete bank statement ya atleast six month toka bank A.
Na ikionekana kama amedefault sana basi mkopo ule utakuwa declined katika bank B.
Katika bank kuna system moja ya kucheki blacklist person aidha ni gaidi,jambazi,au mhalifu yoyote ambaye kimataifa amekuwa noted,lakini katika nchi yetu kuwaangalia wahalifu au wadeni sugu wa ndani ya nchi si sana labda wale ambao wanajulikana sana kitaifa,lakin hii system iko mbion kuanzishwa kwmb taarifa za mtu zitamjulishwa kiasi kwmb katika kila sekta itakuwa rahisi kupata taarifa mfano leseni ya udereva,bank,tra n.k
Kuna ujanja mwingi unafanyika kati ya loan officer na mteja,TZ kitu hakishindwi kuna watu wanajua kuzitengeza hizo bank statement acha! Wana mihuri ya kila bank,wanajua kufoji sahihi za branch managers mpka basi!!! Hivyo yawezekana jamaa yako naye alifanya hako kampango.