Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 144
na Khadija Kalili
MKURUGENZI wa Kampuni ya African Stars Entertainment (ASET), Asha Baraka, ametoa wito kwa wadau wa muziki nchini kumsaidia mwanamuziki mahiri, Ramadhani Masanja Banza Stone aliyelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika Hospitali ya Mwananyamala jana, Asha alitoa wito kwa kila mdau kuguswa na matatizo yaliyomkuta msanii huyo, ambayo yangeweza kumkuta yeyote.
Asha aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Banza Stone kabla ya msanii huyo kujiunga na bendi ya Bambino Sound, alisema kwa sasa msanii huyo anahitaji msaada mkubwa katika kupigania uhai.
Alisema, mara kadhaa msanii huyo alipoumwa, ASET ndiyo iliyokuwa ikigharamia matibabu yake katika Hospitali ya Burhani ya jijini Dar es Salaam, hivyo anahitaji kusaidiwa.
Alisema, kwa mazingira na tabia ya Banza Stone, anastahili kupata usimamizi wa karibu katika ufuatiliaji wa tiba, kula na udhibiti wa utumiaji wa bangi, vitu ambavyo vinazidi kumuathiri.
Alisema, wakati akiwa chini yake, alikuwa akijitahidi kumdhibiti, lakini baada ya kuondoka, Banza Stone amekosa usimamizi wa karibu.
Aidha, mkurugenzi huyo alisema kwa matatizo ya msanii huyo, hastahili kulaumiwa kwa sababu wanaotakiwa kumsaidia kwa sasa ni Bambino Sound, si ASET.
Viongozi wa Bambino Sound ndio wa kulaumiwa, kwani walimchukua kwa ahadi ya kumtibu nchini Ujerumani, lakini hadi sasa ndiyo hivyo, alisema Asha.
Asha alisema, pamoja na hayo, kamwe hawezi kumtupa Banza Stone, kwani hata msanii huyo analijua hilo na ndiyo maana akiwa nje, aliwahi kumtumia tiketi ya ndege kurejea nchini.
Kuna wakati nilikuwa namgharamia matibabu, lakini leo hii watu wanasema tumemtupa, hii siyo kweli, kwani hata Kapteni John Komba aliwahi kutaka kutoa msaada wa kumhamishia Hospitali ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Lugalo, lakini mgonjwa mwenyewe alikataa, alisema.
Alisema baada ya Banza Stone kurejea nchini, alionekana kudhoofika, hivyo ASET wakampeleka Muhimbili kwa vipimo na kubainika anakabiliwa na ugonjwa wa kifua kikuu (TB), kwa kumjali, Asha alikuwa akienda kumchukulia dawa za ugonjwa huo katika hospitali ya kitengo hicho, iliyoko mkabala na Kituo Kikuu cha Polisi.
Msanii amaelazwa katika wodi namba tano ya hospitali ya Mw'nyamala.
MKURUGENZI wa Kampuni ya African Stars Entertainment (ASET), Asha Baraka, ametoa wito kwa wadau wa muziki nchini kumsaidia mwanamuziki mahiri, Ramadhani Masanja Banza Stone aliyelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika Hospitali ya Mwananyamala jana, Asha alitoa wito kwa kila mdau kuguswa na matatizo yaliyomkuta msanii huyo, ambayo yangeweza kumkuta yeyote.
Asha aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Banza Stone kabla ya msanii huyo kujiunga na bendi ya Bambino Sound, alisema kwa sasa msanii huyo anahitaji msaada mkubwa katika kupigania uhai.
Alisema, mara kadhaa msanii huyo alipoumwa, ASET ndiyo iliyokuwa ikigharamia matibabu yake katika Hospitali ya Burhani ya jijini Dar es Salaam, hivyo anahitaji kusaidiwa.
Alisema, kwa mazingira na tabia ya Banza Stone, anastahili kupata usimamizi wa karibu katika ufuatiliaji wa tiba, kula na udhibiti wa utumiaji wa bangi, vitu ambavyo vinazidi kumuathiri.
Alisema, wakati akiwa chini yake, alikuwa akijitahidi kumdhibiti, lakini baada ya kuondoka, Banza Stone amekosa usimamizi wa karibu.
Aidha, mkurugenzi huyo alisema kwa matatizo ya msanii huyo, hastahili kulaumiwa kwa sababu wanaotakiwa kumsaidia kwa sasa ni Bambino Sound, si ASET.
Viongozi wa Bambino Sound ndio wa kulaumiwa, kwani walimchukua kwa ahadi ya kumtibu nchini Ujerumani, lakini hadi sasa ndiyo hivyo, alisema Asha.
Asha alisema, pamoja na hayo, kamwe hawezi kumtupa Banza Stone, kwani hata msanii huyo analijua hilo na ndiyo maana akiwa nje, aliwahi kumtumia tiketi ya ndege kurejea nchini.
Kuna wakati nilikuwa namgharamia matibabu, lakini leo hii watu wanasema tumemtupa, hii siyo kweli, kwani hata Kapteni John Komba aliwahi kutaka kutoa msaada wa kumhamishia Hospitali ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Lugalo, lakini mgonjwa mwenyewe alikataa, alisema.
Alisema baada ya Banza Stone kurejea nchini, alionekana kudhoofika, hivyo ASET wakampeleka Muhimbili kwa vipimo na kubainika anakabiliwa na ugonjwa wa kifua kikuu (TB), kwa kumjali, Asha alikuwa akienda kumchukulia dawa za ugonjwa huo katika hospitali ya kitengo hicho, iliyoko mkabala na Kituo Kikuu cha Polisi.
Msanii amaelazwa katika wodi namba tano ya hospitali ya Mw'nyamala.