Bar ya Aunty Ezekiel yafungwa

warumi

R I P
Joined
May 6, 2013
Posts
16,218
Reaction score
18,440
Wanazengo, leo nimepita Mikocheni kwa Aunty Ezekiel nikaona wamefunga bar yake na wamebandika na bango kabisa “Bar imefungwa kuanzia tarehe 30/10”.

Sasa mmbea mie nikajiuliza ni mtaji umekata baada ya kufanya party ya kufa mtu au ndio sponsor kakasirika baada ya Aunty kurudiana na Moze Iyobo. Au majirani watakuwa wamekasirika makelele ya jumapili wameenda kumreport?

Ebu tujadilini wambea wenzangu maana jamani sio kwa mkosi huu, bar si kafungua tu juzi jamani, mimi nimeumia mwenzenu, pole Aunty.
 
Huyo alianziaga karibia ya kona ya kuelekea mwqnanyamala hosp akaifunga.... Mara akahamia mitaa ya kwamakoma akaifunga
Ndy Sasa hpo mitaa ya Regent karibu na kairuki napo we mmbea unasema pamefungwa....
Biashara zinawenyeweeeeee hizoooo

Ova
 
Tatizo anakunywa mwenyewe na mashosti zake,pesa za bata anachota kwenye biashara
Huyo alianziaga karibia ya kona ya kuelekea mwqnanyamala hosp akaifunga.... Mara akahamia mitaa ya kwamakoma akaifunga
Ndy Sasa hpo mitaa ya Regent karibu na kairuki napo we mmbea unasema pamefungwa....
Biashara zinawenyeweeeeee hizoooo

Ova
 
Mama Biskuti alimpora huyo danga kwa yule muogea maziwa na yy akaona afunguliwe biashara sare sare na mwenzie ..Ndo chanzo yy na binti wa balozi wasialikwe kwenye uzinduz wa reality show juz kati hapa,Sasa juzi sponsa kadhamin birthday mama biskuti kaenda kulambanalambana na Iyobo. Sponsa kajionea mapicha picha kaamua kuchukua vyake.
 
Msiojua biashara ni nini mtamcheka Aunt Ezekiel! Nadhani Wafanyabiashara mnaelewa Hustle ambazo huwa mnapitia hadi biasha isimame! Kuna muda kwenye Biashara Utapigwa matukio hadi utamani kuua mtaa mzimaa lakini unapiga moyo konde! Kuna Muda kwenye Biashara Unafilisika mara 10 lakini ukikata tamaa ndio umekwisha japo waaulimwengu hawawezi kosa Sababu!

Nachokijua Hawa wafanya biashara wakubwaa duniani hakuna aliefanikiwa chini ya Miaka 15 karibia wote wame hustle zaidi ya Miaka 15 hadi biashara zao kuja kusimama na kuendelea! Ninacho kiona hapa ni kwasababu Aunt Ezekiel ni Mtu anae fahamika ndio shida ila huko mtaani biashara nyingi tuu zinakufa na kuzaliwa hadi mtu atakapo kuja kufanikiwa! Ukichanganya na Masharti Ya Serikalii Biashara Tanzania Ni Ngumu sanaa hadi kufanikiwaa Unaweza kuta mtajii wote unaishia kwenye kutafuta Vibali! Ndio maana Wanasema Enterpreniuer yoyote lazima Uwe mbabe ili ufanikiwe! Usione Hizi hospital mnaenda kutibiwa mnapona Jua ameshafungiwa mara kadhaa ameshapigwa vita vya kila aina,Msione hizi bar mnaenda mnalewa mkazani zimeibuka tuu! Vitu ni Vingi! Watu Wenye Makanisa Tuu Wanapata Tabu Sembuse Bar? Kifupi Biashara ni Ngumu na inahitaji ujasiri na uvumilivu.

Ukiona Mtu amefunga biashara yake Usimchekee nenda kajifunze kwake itakusaidia! Sio kazi nyepesi! Huwa napenda sana kujifunza kupitia waliofanikiwa kujua changamoto kifupi changamoto ni nyingi usipo funga biashara yako basi polisi utaendaa either kwa kushtakiwa au kwa kushtaki!

Hakuna Mafanikio yanayo kuja by Chance! Kila kitu ni kupambana nikoona mwanamke kama Aunt anapambana namuheshimu sanaaa Nakumbuka Mama Angu alipambana kunilea kwa kuuza Nyasi za Kuezekea Nyumba! Mwisho wa Siku Maisha yailienda Jabo hiyo biashara pia alipigaa vita vilevile! Tumseme Mtu kwa Yote Kuhusu biashara acheni kama ilivyoo! Ukiona Umeanza leo kuuza nguo na kusema umefanikiwa ndani ya Wiki 1 jua biashara yako haitakuwa Kamwee!! Kuna Watu wanaacha Kazi maofisini wanalipwa millioni 5 lakini wanaenda kwenye biashara zinakufa mara kadhaa lakini wanasimama imara

Kwenye biashara mataifa haya nayapenda sana INDIA,ETHIOPIA,ZIMBABWE yaani Mmoja Akiwa Na Duka Atafanya kila namna amelete Mwenziee nae afanikiwe kwa njia yoyote ile ILA SIO TANZANIA akifanikiwa anataka afanikiwe yeye tuu ili amcheke mwenzie

AUNTY WAKUCHEKE,WAKUSEME USIKATE TAMAAA PAMBANAA HADI DAKIKA YA MWISHO IKIWEZEKANA ACHA KUIGIZAAA SIMAMIA BIASHARA YAKO.
 
Kumbe wamerudiana na king of dance Iyobo?

Kaona nn baada ya mikashfa yote ile kwa mzazi mwenzake?
 
Huyo alianziaga karibia ya kona ya kuelekea mwqnanyamala hosp akaifunga.... Mara akahamia mitaa ya kwamakoma akaifunga
Ndy Sasa hpo mitaa ya Regent karibu na kairuki napo we mmbea unasema pamefungwa....
Biashara zinawenyeweeeeee hizoooo

Ova
Bar iko mikocheni mkuu kalibu na nyumba za watu wa geti jeusi
 
Umeeleza vizuri kwa kweli
 
Bar yenyewe mbona hakuna parking kabisa??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…