Ms Billionaire
JF-Expert Member
- Jul 18, 2020
- 2,452
- 4,955
Habari ya leo wadau.
Salamu kwa Rais Samia.
Mimi ni Mwanachi wako mkazi wa Goba mwaka wa 12 huu. naleta malalamiko kuhusu njia ya Tegeta A iliyoungana na Kulangwa Nimeishi huku miaka mingi na changamoto yetu kubwa ni barabara.
Nilileta malalamiko yangu miezi michache iliyopita kuhusu barabara za Tegeta A na Kulangwa ila changamoto tunayoihofia ni kipindi cha mvua hatuna CARAVAT inayoeleweka tegeta A karibu na KITUO CHA AFYA cha ST YOHANE.
Goba kuna shule nyingi sana kama Victory Adonai, Victory Christian Center na nyingine nyingi, school bus nyingi sana zinapita kwenye hili caravat ninalo lilalamikia asubuhi na jioni, ni hatari kwa schoolbus za watoto wetu hata kipindi hiki ambacho sio cha mvua ni hatarishi vipi pakizidisha unyevu na udongo ukamomonyoka?
Serikali tunaomba itusaidie KUTANUA hili daraja na waweke caravat imara na lenye upana ili watoto wetu wapite vizuri bila hofu matukio ni mengi na kinga ni bora kuliko tiba msije sema hatukuwaambia mapema.
Rais Samia tunaomba utusaidie kuwakumbusha viongozi uhai wa watoto wetu ni muhimu sana hii ni hatari na hatuna njia nyingine ya kupitisha watoto wetu. Ikiwezekana hii njia ichongwe hadi mwishoni kule kanisa la Roman Catholic Tegeta A karibu na hiyo shule ya Victory Christian.
Soma Pia: Changamoto ya barabara mbovu Goba Kulangwa/Tegeta a Serikali inapuuza?
Siku nimeenda shuleni kwa mwanangu nimepita kwenye hilo caravat moyo ulitetemeka nikasema watoto zaidi ya mia wanapita hapa kwenye schoolbus tofauti kwanini hatuwekei uzito wa hili caravat kutengenezwa? Kwasababu mimi nakaa upande wa kulangwa lakini watoto wanasoma Tegeta A lazima nitetee haki ya wote hata kama mimi situmii hiyo njia. Watoto watasemewa na nani?
Iliwahi kutokea changamoto ya school Bus ya watoto kunusurika kuleta maafa. Ila maafa ya hili caravat ni mabaya kuliko kawaida tunaomba litengenezwe upya.
Hatutaweza kuvumilia kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa muongelee mambo mengine wakati hatari kama hizi hamzi solve.
Rais Samia kwa maelekezo mazuri tu nikuelezee watoto wetu na school bus zinapopita kwenye caravat mbovu ni ile njia ya Goba Kulangwa/Tegeta A inachepua kushoto kabla ya skymart supermarket kama umetokea njia nne ile njia inayoenda St Yohanne Health center na Victoria Adonai school inanyooka hadi makanisa ya Anglikana na katoliki kuelekea madawa.
Tunaomba msaada ile njia ichongwe vizuri maana hiyo ndo njia yenye caravat bovu lipo karibu na kituo cha afya ya ST Yohanne hata ukituma watu wako wanaweza kwenda kuliona. Ni hatari mno kwa watoto wetu.
Jengeni daraja kubwa wekeni na kingo pembeni.
Nawasalisha
Salamu kwa Rais Samia.
Mimi ni Mwanachi wako mkazi wa Goba mwaka wa 12 huu. naleta malalamiko kuhusu njia ya Tegeta A iliyoungana na Kulangwa Nimeishi huku miaka mingi na changamoto yetu kubwa ni barabara.
Nilileta malalamiko yangu miezi michache iliyopita kuhusu barabara za Tegeta A na Kulangwa ila changamoto tunayoihofia ni kipindi cha mvua hatuna CARAVAT inayoeleweka tegeta A karibu na KITUO CHA AFYA cha ST YOHANE.
Goba kuna shule nyingi sana kama Victory Adonai, Victory Christian Center na nyingine nyingi, school bus nyingi sana zinapita kwenye hili caravat ninalo lilalamikia asubuhi na jioni, ni hatari kwa schoolbus za watoto wetu hata kipindi hiki ambacho sio cha mvua ni hatarishi vipi pakizidisha unyevu na udongo ukamomonyoka?
Serikali tunaomba itusaidie KUTANUA hili daraja na waweke caravat imara na lenye upana ili watoto wetu wapite vizuri bila hofu matukio ni mengi na kinga ni bora kuliko tiba msije sema hatukuwaambia mapema.
Rais Samia tunaomba utusaidie kuwakumbusha viongozi uhai wa watoto wetu ni muhimu sana hii ni hatari na hatuna njia nyingine ya kupitisha watoto wetu. Ikiwezekana hii njia ichongwe hadi mwishoni kule kanisa la Roman Catholic Tegeta A karibu na hiyo shule ya Victory Christian.
Soma Pia: Changamoto ya barabara mbovu Goba Kulangwa/Tegeta a Serikali inapuuza?
Siku nimeenda shuleni kwa mwanangu nimepita kwenye hilo caravat moyo ulitetemeka nikasema watoto zaidi ya mia wanapita hapa kwenye schoolbus tofauti kwanini hatuwekei uzito wa hili caravat kutengenezwa? Kwasababu mimi nakaa upande wa kulangwa lakini watoto wanasoma Tegeta A lazima nitetee haki ya wote hata kama mimi situmii hiyo njia. Watoto watasemewa na nani?
Hatutaweza kuvumilia kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa muongelee mambo mengine wakati hatari kama hizi hamzi solve.
Rais Samia kwa maelekezo mazuri tu nikuelezee watoto wetu na school bus zinapopita kwenye caravat mbovu ni ile njia ya Goba Kulangwa/Tegeta A inachepua kushoto kabla ya skymart supermarket kama umetokea njia nne ile njia inayoenda St Yohanne Health center na Victoria Adonai school inanyooka hadi makanisa ya Anglikana na katoliki kuelekea madawa.
Tunaomba msaada ile njia ichongwe vizuri maana hiyo ndo njia yenye caravat bovu lipo karibu na kituo cha afya ya ST Yohanne hata ukituma watu wako wanaweza kwenda kuliona. Ni hatari mno kwa watoto wetu.
Jengeni daraja kubwa wekeni na kingo pembeni.
Nawasalisha