KERO Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Mzinga kuja Kongowe mpaka Kisemvule iboreshwe kabla ya kuleta maafa

KERO Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Mzinga kuja Kongowe mpaka Kisemvule iboreshwe kabla ya kuleta maafa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
Oct 7, 2024
Posts
9
Reaction score
10
Hii barabara ya Kilwa kipande cha kushuka hapa Kokoto kuja daraja la Mzinga mpaka Kongowe imeshakuwa kero kubwa sana kwa wakazi wa huku maana foleni haziishi sababu barabara ni nyembamba kiasi gari likiharibika hapo ni majanga inabidi mkae foleni mpaka either gari litolewe au askari wasimamishe na kuruhusu magari ya upande mmoja mmoja huku muda ukiendelea kupotea kwa sisi tunaotegemea kuitumia kila siku.

Barabara pia ina mashimo mengi mno na mkandarasi anaweka viraka tu tena kwa muda anaotaka yeye, kama hivi sasa amekata mashimo ya viraka kayatelekeza bila kujali kwamba yanasababisha usumbufu na ajali kwa watumiaji.

Pia daraja la mto Mzinga pale ni la chuma limepata kutu sana kutokana na kukaa muda mrefu, ukipita sehemu za watembea kwa miguu unaona lilivyoanza kumegeka ni hatari pia daraja ni jembamba sana ukilinganisha na aina na idadi ya magari yanayopita pale ambaye mengi yanasafirisha mizigo.

Soma Pia: Barabara ya Kilwa kipande cha Mzinga Kongowe kinatumaliza

Jamani mamlaka zinazohusika ziangalie barabara hii wasisubiri yatokee maafa ndio waje na salamu za kiunafiki wananchi tunaumia.

Naomba kuwasilisha
 
Hii barabara ya Kilwa kipande cha kushuka hapa Kokoto kuja daraja la Mzinga mpaka Kongowe imeshakuwa kero kubwa sana kwa wakazi wa huku maana foleni haziishi sababu barabara ni nyembamba kiasi gari likiharibika hapo ni majanga inabidi mkae foleni mpaka either gari litolewe au askari wasimamishe na kuruhusu magari ya upande mmoja mmoja huku muda ukiendelea kupotea kwa sisi tunaotegemea kuitumia kila siku.

Barabara pia ina mashimo mengi mno na mkandarasi anaweka viraka tu tena kwa muda anaotaka yeye, kama hivi sasa amekata mashimo ya viraka kayatelekeza bila kujali kwamba yanasababisha usumbufu na ajali kwa watumiaji.

Pia daraja la mto Mzinga pale ni la chuma limepata kutu sana kutokana na kukaa muda mrefu, ukipita sehemu za watembea kwa miguu unaona lilivyoanza kumegeka ni hatari pia daraja ni jembamba sana ukilinganisha na aina na idadi ya magari yanayopita pale ambaye mengi yanasafirisha mizigo.

Soma Pia: Barabara ya Kilwa kipande cha Mzinga Kongowe kinatumaliza

Jamani mamlaka zinazohusika ziangalie barabara hii wasisubiri yatokee maafa ndio waje na salamu za kiunafiki wananchi tunaumia.

Naomba kuwasilisha
Kwani huko Kuna chadema ? ,niliwahi kusikia chadema wanakwamisha maendeleo ..oohh kumbe huko ni kijani na mbunge wao ni waziri wa mifugo...sawa...kama wakijani pia wanateseka ni vizuri..

Barabara ya nini wakati mama anapiga mwingi...
 
Hicho kipande tayari kina maafa ya kutosha na mamlaka ziko kimya tuu
 
Hiki kipande kidogo kiondoke na uhai wangu,siwezi sahau ,lory break zilifail likawa linashuka linagonga magari,sisi tulipigwa tukasogea kwenye mtaro .Bahati nzuri kuna gari ilipigwa ikanasa kwenye trailer la lory moja lilikuwa linapanda uelekeo wa mbaga ,ndio ikaawa kama break ya lile lory liliokuwa linashuka
 
Back
Top Bottom