Barabara ya kumbukumbu kutoka Usukumani hadi Kariakoo

Barabara ya kumbukumbu kutoka Usukumani hadi Kariakoo

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
TUTEMBEE KWENYE BARABARA YA KUMBUKUMBU KUTOKA USUKUMANI KWA CHIEF MAKWAIA MOHAMED MWANDU (1905 - 1945) HADI KARIAKOO KWA ABDULWAHID KLEIST SYKES (1924 -1968)

Chief Makwaia Mohamed Mwandu ndiye baba yake Chief David Kidaha Makwaia.

Mtoto wa Chief Makwaia, Chief Kidaha (1922 - 2007) alifikiriwa kuongoza TAA mwaka 1951na waunde TANU mwaka unaofuatia yaani 1952 lakini haikuwa.

Hiki ni kisa kisichofahamika na wengi.

Chief Kidaha alikuwa chaguo la Abdul Sykes lakini Hamza Mwapachu (1913 - 1962) yeye alimtaka Julius Nyerere.

Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) Mufti wa Tanganyika alisimama bega kwa bega na Nyerere akiitangaza TANU misikitini na kuuza kadi za chama katika darsa zake hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.

Nani leo anaejua historia za wazalendo hawa?

Leo inapozungumzwa kumtanguliza Mungu ni muhimu sana kuwakumbuka masheikh wazalendo waliouza kadi za TANU misikitini na kufungua mikutano ya TANU tena ya hadhara kwa kusoma Qur'an.

Je, tunae kiongozi wa dini, mzalendo mfano wa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir?

Imekuwaje hatajwi katika historia?

Screenshot_20210326-170112_Facebook.jpg


Screenshot_20210327-071651_Facebook.jpg
 
Ka Nyerere kalikuwa kajanja sana. Kasomi haka ka elimu duniya kametoka zake Butiama huko na kuwaingilia akina Sykes mpaka wakakaunga mkono huko Pwani.

Umewatendea haki na kuwapigania sana wazee wako hawa ili nao wapewe nafasi wanayostahili katika historia ya Tanzania. Endelea kuwapambania kwa sababu sidhani kama kuna andiko lako ambalo kwa namna moja au nyingine halimtaji Sykes.
 
Ka Nyerere kalikuwa kajanja sana. Kasomi haka ka elimu duniya kametoka zake Butiama huko na kuwaingilia akina Sykes mpaka wakakaunga mkono huko Pwani.

Umewatendea haki na kuwapigania sana wazee wako hawa ili nao wapewe nafasi wanayostahili katika historia ya Tanzania. Endelea kuwapambania kwa sababu sidhani kama kuna andiko lako ambalo kwa namna moja au nyingine halimtaji Sykes...
Shimba,

Ikiwa historia ni kuhusu African Association, Tanganyika African Association (TAA), TANU, uhuru wa Tanganyika na Julius Nyerere huwezi kuiandika historia hiyo bila kuwemo akina Sykes.

Wamejaribu kuwafuta akina Sykes katika historia ya TANU matokeo yake ndiyo haya.

Huwezi kuandika historia ya Azimio la Arusha na Vijiji Vya Ujamaa bila kumtaja Nyerere.

Mwandishi hataeleweka.
 


Jamii ya Marastafari ni wafuasi wazuri wa historia na mashujaa wetu.

Mfumo wetu wa elimu umewaondoa mashujaa wetu wengi kwenye historia.

Mzee Wangu Mohamed Said, naomba kama inawezekana, jamii ya Marastafari ipewe vitabu vinavyowahusu mashujaa wetu, wavisome na wavielewe, wao ndio watu pekee wanaoenzi utamaduni wetu, wengine wako na dini za melikebu, hao hata Mkwawa kwao wanamuona snitch tu sababu alipigana na wazungu walioleta dini.
 
Ka Nyerere kalikuwa kajanja sana. Kasomi haka ka elimu duniya kametoka zake Butiama huko na kuwaingilia akina Sykes mpaka wakakaunga mkono huko Pwani.

Umewatendea haki na kuwapigania sana wazee wako hawa ili nao wapewe nafasi wanayostahili katika historia ya Tanzania. Endelea kuwapambania kwa sababu sidhani kama kuna andiko lako ambalo kwa namna moja au nyingine halimtaji Sykes...

Kwa kusema ' Ka Nyerere ' umelenga nini hasa Ndugu? Dhihaka kwa Marehemu tena waliopambana kwa Uhuru na Ustawi wako na wangu hivi sasa si sahihi.
 
Back
Top Bottom