Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Habari,
Licha ya kuwepo Malalamiko ya mara kwa mara kuhusu adha ya ubovu wa barabara Maeneo ya kuanzia Juu kidogo kwa Mpalange mpaka Kituo Cha Mwisho Mwanagati lakini hakuna hatua zinachukuliwa. Soma malalamiko Hapa
Barabara ya Maeneo haya imekuwa shida kubwa na haipitiki kwa urahisi kiasi ambacho daladala, bajaji na pikipiki wanalazimika kupandisha nauli kama fidia ya vyombo vyao vya usafiri.
Barabara hii imekuwa mbovu kwa kiasi ambacho sehemu unayoweza kusafiki dakika kumi unalazimika kusafiki muda zaidi kwa sababu magari yanalazimika kutembea taratibu sana.
Imekuwa kawaida kukuta magari na bajaji zimekwama kwenye madimbwi makubwa ya maji. Pia, imekuwa kawaida vyombo vya usafiri kukwepa njia Kuu kuingia mitaani mwa watu Ili kuyaepuka madimbwi hayo.
Mbunge wetu Jerry Silaa huoni jambo hili kweli? Mbona umekuwa unashughulikia migogoro ya ardhi lakini tatizo kubwa kama hili kwenye Jimbo lako hutaki kulitatua.
Wakazi wa Mwanagati nasi tunalipa Kodi tunaomba mtuboreshee barabara hii tuache kulalamika kila Leo.
Jamiiforums tunaomba mtusaidie kupaza sauti hii ujumbe ufike.
Hizi hapa Chini ni baadhi ya picha nilizopiga Leo. Imagine hapa mvua haijanyesha Pako hivi. Mvua ikipiga hapatamaniki zaidi.
UPDATE
- Baada ya malalamiko mengi hatimaye barabara ya Mwanagati imemwagwa vifusi na kusawazishwa
Licha ya kuwepo Malalamiko ya mara kwa mara kuhusu adha ya ubovu wa barabara Maeneo ya kuanzia Juu kidogo kwa Mpalange mpaka Kituo Cha Mwisho Mwanagati lakini hakuna hatua zinachukuliwa. Soma malalamiko Hapa
Barabara ya Maeneo haya imekuwa shida kubwa na haipitiki kwa urahisi kiasi ambacho daladala, bajaji na pikipiki wanalazimika kupandisha nauli kama fidia ya vyombo vyao vya usafiri.
Barabara hii imekuwa mbovu kwa kiasi ambacho sehemu unayoweza kusafiki dakika kumi unalazimika kusafiki muda zaidi kwa sababu magari yanalazimika kutembea taratibu sana.
Imekuwa kawaida kukuta magari na bajaji zimekwama kwenye madimbwi makubwa ya maji. Pia, imekuwa kawaida vyombo vya usafiri kukwepa njia Kuu kuingia mitaani mwa watu Ili kuyaepuka madimbwi hayo.
Mbunge wetu Jerry Silaa huoni jambo hili kweli? Mbona umekuwa unashughulikia migogoro ya ardhi lakini tatizo kubwa kama hili kwenye Jimbo lako hutaki kulitatua.
Wakazi wa Mwanagati nasi tunalipa Kodi tunaomba mtuboreshee barabara hii tuache kulalamika kila Leo.
Jamiiforums tunaomba mtusaidie kupaza sauti hii ujumbe ufike.
Hizi hapa Chini ni baadhi ya picha nilizopiga Leo. Imagine hapa mvua haijanyesha Pako hivi. Mvua ikipiga hapatamaniki zaidi.
UPDATE
- Baada ya malalamiko mengi hatimaye barabara ya Mwanagati imemwagwa vifusi na kusawazishwa