Barabara za mwendokasi (BRT) zinatumiwa zaidi na magari ya vigogo wa serikali na gari za ST kuliko mabasi kwa ajili ya wananchi wa kawaida!

Barabara za mwendokasi (BRT) zinatumiwa zaidi na magari ya vigogo wa serikali na gari za ST kuliko mabasi kwa ajili ya wananchi wa kawaida!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Naanza kuamini kwamba mwendokasi ulikuwa uongo mwingine wa wanasiasa, kwamba wanataka kuondoa kero za usafiri jijini kwa ajili ya wananchi. Hizi barabara zilitengenezwa kwa ajili yao kukwepa bugudha za barabara za kawaida.

Nimeona kwamba barabara za mwekasi zinatumiwa zaidi na magari ya setikali kuliko mabasi yaliyokusudiwa kusaidia wananchi.

Labda ukweli ni kwamba kuna viongozi wa serikali wanafanya makusudi kutoweka mabasi ya mwendokasi barabarani ili barabara hizi wazitumie wao na magari yao ya ST na kadhalika.

Ni kama wanajua ikiwa mabasi ya mwendokasi yatakuwa mengi, hawataweza tena kutumia barabara hizi, na hivyo kunakuwa na jitihada za makusudi kuhakikisha hakuna uendelevu wa huduma ya mabasi ya mwendokasi

Sintashangaa siku moja nikisikia serikali imetoa tamko rasmi kwamba gari za serikali sasa ni rasmi kuruhusiwa kupita barabara za mwendokasi!
 
Leo maeneo ya Magomeni kumetokea kosa kosa kwenye barabara STM kwenye barabara ya mwendokasi!
 
Naanza kuamini kwamba mwendokasi ulikuwa uongo mwingine wa wanasiasa, kwamba wanataka kuondoa kero za usafiri jijini kwa ajili ya wananchi. Hizi barabara zilitengenezwa kwa ajili yao kukwepa bugudha za barabara za kawaida.

Nimeona kwamba barabara za mwekasi zinatumiwa zaidi na magari ya setikali kuliko mabasi yaliyokusudiwa kusaidia wananchi.

Labda ukweli ni kwamba kuna viongozi wa serikali wanafanya makusudi kutoweka mabasi ya mwendokasi barabarani ili barabara hizi wazitumie wao na magari yao ya ST na kadhalika.

Ni kama wanajua ikiwa mabasi ya mwendokasi yatakuwa mengi, hawataweza tena kutumia barabara hizi, na hivyo kunakuwa na jitihada za makusudi kuhakikisha hakuna uendelevu wa huduma ya mabasi ya mwendokasi

Sintashangaa siku moja nikisikia serikali imetoa tamko rasmi kwamba gari za serikali sasa ni rasmi kuruhusiwa kupita barabara za mwendokasi!
Mabasi si yameharibika
 
Mie sion shida kwa gari za serikal kutumia hiyo barabara.

Au mtoa mada kuna shida gani hizo gari zikipita humo?
 
Useme serikali imeacha yaharibike ili watumie barabara za mwendokasi!😀

Lakini habari njema ni kwamba wameongeza basi 100. Sasa tuone hizi zitadumu kwa muda gani
Mkuu kwa nini hawataki kuyafanyia Servise?
Waziri mkuu aliwatembelea na alichoka kabisa alichokikuta
 
Mkuu kwa nini hawataki kuyafanyia Servise?
Waziri mkuu aliwatembelea na alichoka kabisa alichokikuta
Tanzania hii ni ya ajabu sana. Watu wanasema kuna hujuma za makusudi. Mwendo kasi inaua biashara ya taksi, daladala, bajaji na bodaboda. Na pia kuna suala la watu wanaotaka wapewe tenda ya ku-service na ku-supply mabasi, wakitajwa vigogo wakuu sana.

Sasa maswali yanayofuata ni kwamba, baada ya SGR kuonekana ina demand kubwa sana, na itapunguza sana biashara ya usafirishaji kwa barabara, tutaona treni nazo zina park kwa kuharibika na kukosa service? Kwenye SGR pia kuna interest TRC ionekane inafeli watu binafsi wakamate
 
Tanzania hii ni ya ajabu sana. Watu wanasema kuna hujuma za makusudi. Mwendo kasi inaua biashara ya taksi, daladala, bajaji na bodaboda. Na pia kuna suala la watu wanaotaka wapewe tenda ya ku-service na ku-supply mabasi, wakitajwa vigogo wakuu sana.

Sasa maswali yanayofuata ni kwamba, baada ya SGR kuonekana ina demand kubwa sana, na itapunguza sana biashara ya usafirishaji kwa barabara, tutaona treni nazo zina park kwa kuharibika na kukosa service? Kwenye SGR pia kuna interest TRC ionekane inafeli watu binafsi wakamate
Tena hio SGR utakufa kama TRC.
Hata usipoteze muda wako na nguvu kuwafikiria.
Its just matter of time
 
Tena hio SGR utakufa kama TRC.
Hata usipoteze muda wako na nguvu kuwafikiria.
Its just matter of time
Viongozi wakiiacha SGR ikafa basi itakuwa wazi Tanzania inahitaji uongozi mbadala wa nchi, na usio wa kisiasa!
 
Back
Top Bottom