Mwaka huu baraza la Mitihani lilitoa utaratibu wa kuripia mitihani kwa njia tatu, ambazo ni Posta, M-Pesa an Selcom. Lakini imeonekana kuna tatizo la mfumo wa malipo. Mimi nilituma ada ya mtihani kwa njia ya M-pesa, lakini juzi nilipata msg ya kunitaka nikaripie mitihani kabla ya tarehe 1 mwezi wa nne. Hapa najiuliza tatizo ni nini? Je mfumo hauwezi kutambua malipo ambayo Vodacom wameyathibitish? Naomba baraza litusaidie kwa hili kwani kulipa mara mbili ni kutuumiza walala hoi wa Tanzania. Pia naomba baraza lituambie hatma ya pesa ambayo imetumwa kwao kwa njia ya M-pesa.Je itarudishwa?