Barclays bank ni noma, msaada wa sheria haraka

wachome kwenye media na tafuta mwanasheria mzuri utafanikiwa.mpe pole!
 
Wana JF nashukuru kwa mchango wenu, nimewasiliana na ndugu yangu kuwa aandae vielelezo vyote kwa ajili ya kuwapeleka mahakamani, lakini sasa naomba kama kuna mwenye kumjua wakili mzuri asiye na tamaa na asiyecheza double dill, basi tufahamishane ili hatua zaidi ziendelee,ntakuwa nawapa hatua kwa hatua juu ya hii kesi, nilimhadithia rafiki yangu mmoja mholanzi, akashangaa sana akaniuliza, kwani huko tanzania mawakili huwa wanafanya kazi gani? au hakuna?. nikamwambia wapo lakini hawajui wajibu wao kazi yao ni kufunga tai na suti halafu wanapiga mizinga kwa machinga
 
Sheria inaweza ikawa upande wao kwenye hili, wewe uko responsible kwa cheque zote zinazodunda. Pesa inaweza kuingia hata siku hiyo hiyo kwenye account ila cheque inaweza kuchukua muda mrefu zaidi kudunda.

Sasa kwa vile walikuambia kuwa baada ya siku 21 uko salama hii inaweza ikabadilisha kesi, ila tatizo ni katika ushahidi, je utaweza kuprove kuwa uliambiwa siku 21 zinatosha, je alipata ahadi hiyo katika maandishi? Mkienda mahakamani mashahidi watasemaje? etc

Scam za aina hii ni very common, unatumiwa cheque, unaipeleka benki inaclear, kisha aliyekutumia anakuambia mtumie some % kwa wire transfer kisha kilichobaki ni chako, ukishafanya hivyo baada ya muda benki inakwambia cheque imedunda, inakula kwako.

Kwa kifupi kupokea cheque ni hatari sana.
 

Sasa maana ya wao kukaa na check siku 21 ni nini, mimi nilifikiri ni kwa wao kujiridhisha kuwa kila kitu kipo sawa, na tarehe check ilipoingia inaonyesha, na tarehe waliyoingiza pesa inaonyesha, ni siku ya 23 ndipo walipoingiza pesa, na baada ya kuona pesa kijana aka release mzigo wa watu, sasa hapo kuna kizunguzungu gani?
 
Major,
NimekuPM namba ya wakili anayefanya kazi benki ili aweze kukusaidia. Sidhani kama anaweza kukuchakachua.
 

ukipeleka cheque huwa wanarekodi siku ambayo wamepokea,
 

Pole sana! Nadhani majibu yaliyotolewa na baadhi ya wachangiaji yanaridisha. Nashangaa kwa nini vyombo vya dola havishughuliki na hii Barclays Bank Tanzania. Mimi nilichukua mkopo mdogo (shillingi milioni 10 Decemba 2007) na majrejesho wakawa wamesema miaka minne, ambayo nilitegemea mwisho iwe mwaka huu. Baada ya miezi sita, walinipigia simu wakasema kwa vile marejesho yangu so far ni mazuri wameona wani'ofe' TOP UP ya milioni 4 hivi. Nikaona itanisaidia kuendesha mambo yangu. Kwa bahati mbaya wakaniita niende kusaini karatasi kuonesha nimekubali.

Nami nikasaini na kwa vile nilidhani ni offer (nilichukulia kama bonus vile) na nilidhani huenda wakaongeza kiasi ninachorejesha kila mwezi maana nilikuwa narejesha laki na kumi na tano elfu hivi, ikafika hadi laki 3 na 45 elfu hivi. Sasa siku moja nilienda kuwaomba stamement ili nijue kama namaliza mwaka huu ni mwezi gani, nikakuta wameandika deni litaisha Desemba 26, 2014.

Nilitaka kuzimia! Niliuliza kwa nini? Wakasema TOP UP ni mika 6 na nilipaswa niambiwe kabla ya kusaini ile karatasi na kama sikuambiwa basi hakuna la kufanya ispokuwa kuendelea kulipa hilo deni hadi liishe. Nikawaambia "basi mko 'dishonest' kwa wateja wenu. Mnataka tu wasaini kitu bila kuwaelekeza nini masharti yake." Na mimi nakubaliana na wachangiaji wengine kwamba Barclays Tanzania ni matapeli na wameshaliza wateja wengi sana! Hata mimi nimeshamisha account yangu. Mshahara napokelea benki nyingine na nawapelekea tu kiasi ninachorejesha kwa kuzidisha kidogo tu.
 
Major,
NimekuPM namba ya wakili anayefanya kazi benki ili aweze kukusaidia. Sidhani kama anaweza kukuchakachua.

Thanks, careen, nimeshamtumia e mail, kumwelezea kilichotokea, nitaondoka na ndege ya saa nne usiku kuelekea nairobi i hope nikifika nitampigia tuongee zaidi, ningependa hii pesa ipatikane as soon, na nakupromiss caren ikitoka nitakuita arusha december maana nitakuwa huko tukale bata,sasa hivi niko baiyung air port china,
 

Umeongeza siku zangu za kuishi..
 
ukipeleka cheque huwa wanarekodi siku ambayo wamepokea,

Tatizo sio siku waliyopokea wala siku waliyoweka pesa benki. Wewe kama mtu uliyepeleka cheque benki uko responsible kwa ile cheque yaani majukumu yote kuhusu uhalali wa ile cheque yako juu yako, na kuingia kwa hela kwenye account yako haimaanishi kuwa ile cheque ni halali.

Sasa kama walimhakikishia siku 21 zinatosha basi anaweza akawa na kesi,tatizo litakuwa kwenye kupata ushahidi kuwa walimhakikishia.

Yaani fikiria, kama majukumu yote yangekuwa ya Benki watu kibao wangeandika cheque zinazodunda kisha hela ikiingia wanazitumbua zote, Benki zingepata hasara sana.
 
Kwa hiyo kama ni hivyo, basi kila anayelipwa kwa check anakuwa hajalipwa, kwa maana aliyekulipa anaweza kudil na watu wa benki halafu akarudishiwa pesa wakati wewe unakuwa umesha-delever bidhaa, nijuavyo mimi kama check imebaunzi, wanatakiwa wakurudishie check yako kabla hawajakulipa, ili upate ushahidi wa kumdai aliyekupa check, sasa huyu ndugu yangu,ameomba wamrudishie check yake, lakini wanasema check hawana, huu ni wizi
 
There must be something missing here guys.

Mbona kama hii case iko simple hivi haihitaji hata Lawyer!!

Unaacha milioni 30, inashikiliwa Benki kwa miezi nane leo ndo uje uombe msaada wa kisheria?

Great thinkers please think greatly.
 
barclays bank (T) , sidhani kama inakidhi viwango vya kibenki ni wakati umefika sasa wahusika waitolee macho , malalamiko yametosha .
 

Benki wanapotoa muda kwa hundi ku-clear ni utaratibu waliojiwekea ili kuweza kuchunguza uhalali wa hundi hiyo pamoja na kuwasiliana na benki inayohusika kama mlipaji ana pesa kwenye account yake. Ndio maana huweka siku 3 za kazi kwa hundi za hapa nchini na siku 21 kwa hundi za nje....Isitoshe, kwa hundi za nje mteja hutozwa ada fulani kwa ajili ya gharama za mawasiliano na benki za huko nje n.k.

Ni jukumu la benki kujiridhisha kwanza kama hundi ni halali au la kabla hawajamlipa mteja...siku wanazotoa kwa amteja kusubiri zinatosha kabisa kuwasiliana na benki husika kama hundi hiyo ni halali na kama mlipaji ana kiasi cha kutosha kwenye account yake. Ikitokea kama hundi ina matatizo basi wanatakiwa kumrudishia mteja wao ili akapambane na huyo mdeni wake.

Kwenye hii issue ya Barclays lazima kuna uzembe fulani ulifanyika ndani ya benki yenyewe kwa kushindwa kufanya uhakiki unaotakiwa kabla ya kumwekea pesa huyo jamaa...
 

Ni sawa kabisa mkuu, sasa unatoa ushauri gani?
 
Kwa aina ya Shughuli zangu nimekua niki-deal na Banks karibia zote kila siku.
Asikuambie mtu, kwa utapeli wa kuibiana tu, Barclays wanaongoza.
Yaani kuna vijana wako pale wao kazi zao ni "kupiga" tu,
Mtu kamaliza chuo mwaka uliopita, kwa Net ya say laki 6 tu anataka kua na Bangaloo, Mkoko, Ndoa ya Kifahari n.k.
Pili bado sijaelewa iweje mtu alete cheki kutoka nchi ingine na ui-deposit under normal procedure, sijawahi kusikia hii kitu.
Kwa navyofahamu, ilitakiwa hao wacomoro wafanye "telegraphic transfer", tena ambayo ingechukua maximum 3days kuonekana.
Lakin pia kama hiyo cheki ilionekana kwenye statement ya jamaa, ikapewa value date ya hizo siku 21, na jamaa aka-trade nao AFTER hiyo value date basi hiyo statement ni ushahidi tosha wa yeye kuwashtaki.
Ila kama ali-trade nao WITHIN value date, ahesabie maumivu tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…