Barua ya wazi kwa Uhuru Kenyatta: Ungetatua kwanza mgogoro na Wananchi wako si Tanzania

Barua ya wazi kwa Uhuru Kenyatta: Ungetatua kwanza mgogoro na Wananchi wako si Tanzania

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2016
Posts
17,506
Reaction score
16,003
Ndugu yangu Uhuru aka Kamwana,

Kuna mambo umeyafanya ambayo yameleta ghadhabu wa wakenya sasa unataka kutupia lawama mataifa jirani kama ambavyo Trump anavyolaumu China kwa matatizo yake ya ndani.

Ushauri wangu tulia jifunze kutatua matatizo wa wanakenya kwa kutumia mikakati ya kimagharibi. Hili limekuwa tatizo kwenye nchi nyingi Afrika na inatokana zaidi na ukakasi wa viongozi wengi kukariri mitaala (curriculum) iliyotengenezwa kutatua changamoto za ulaya na Amerika. Hii imesababisha wafanya maamuzi wengi hasa wakurugenzi, makatibu wakuu badala ya kupata elimu wao hukazana kuzungumza Kiingereza kwa lafudhi (accent) ya wazungu huku akitingisha kichwa na kushika nywele kichwani ili naye aonekane Mzungu hapa ndipo wazungu hutushangaa wanachofanya ni kukusifia huku wakikuzodoa (dharau).

Mtu akitumia mbinu nzuri ambayo inafaa kwa mazingira husika usimchukie bali soma taratibu uchanganye na akili zako ili uweze kutafuta suluhisho sahihi kwa mazingira yako ili usiwaumize wananchi. Nikupe mfano pamoja na utajiri wa nchi za magharibu na uwezo wa kulipa wananchi wao ''walfare payments'' au malipo kwa wasio na ajira hili jambo halitekelezeki (unsastainable) kwa muda wa kati (short term) na muda mrefu (long-term). tusitatue changamoto za Africa kwa kutumia ''blue print'' za IMF, WB, WHO na kadhalika bali tusome hizo ''blue prints'' tuchague yanayotufaa na tuite wataalamu wetu wa nyanja mbalimbali ili kutatua tatizo.

Kwa mfano; ili kukabiliana na janga la Covid-19 inapasa viongozi wa Africa kusoma muongozo wa WHO (ambao kimsingi umejikita kwenye afya), lakini yatupasa kushirikisha wataalamu wa uchumi, biashara, miradi, kilimo, jamii na kadhalika ili kuja na mkakati wa jumla (Holistic approach) ambao utatekelezwa bila kuleta machungu sana kwa wananchi. Leo hii Ndugu Kenyatta ukitumia watu wako wa usalama wachunguze wanakenya wangapi wanakufa usishangae kuambiwa waliokufa na maradhi yanayosababishwa na njaa ikiwemo unyanyasaji ni wengi kuliko wanaokufa na Covid-19.

Nimeshangaa kusikia mmoja wa mawaziri waandamizi (CS)kwenye wizara ya Kilimo Bw.Munga akitangaza kuagiza chakula kutoka Ethiopia. Kama baraza la mawaziri lina waziri amabye hajui hali ya mavuno na chakula kwa nchi jirani lazima kuna tatizo la msingi. Ethipia hii ambayo miaka na mikaka ina tatizo la njaa, nzige, siasa zisizotulia (political instability leo wauie Kenya Chakula? Mh. Kenyatta hivi waziri wako hajui kuwa umoja wa ulaya umeahidi kuchangisha mamilioni ya euro kuisadia Ethiopia kupambana na baa la njaa (hunger)?

Kuhusu suala la madereva kusafirisha vitu mipakani linahitaji busara kubwa sana ili kuepuka malalamiko ya wananchi wa Afrika ya Mashariki. Ili kuepuka lawama kwamba madereva wa Tanzania ''wanaingiza Covid-19'' Kenya, Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro aliagiza kuwa mizigo yote inayoingia Kenya kupitia mipakani ishushwe kutoka magari ya Tanzania na kupakiwa kwenye magari ya Kenya yenye madereva wa Kenya ''wasioa na Covid-19'' ili kuzuia maambukizi na vilevile ile inayotoka Kenya ishushwe mpakan na kupakiwa kwenye magari yenye madereva wa Tanzania; mantiki ya hoja hii ni kama ifuatavyo;
  1. Ni jambo lisilowezakana madereva kuwa kila siku hauumwi unapimwa mfano kwa dereva anayeingia Kenya/Tanzania mara tano kwa mwezi atalazimika kupimwa mara kumi kwa mwezi, yaani mara tano 5 na mara tano Tanzania. Ni nani anaweza kuvumilia?
  2. Ucheleweshaji wa mizigo kusubiri vipimo umeharibu thamani ya bidhaa na mazao na pia kuongeza gharama ya biashara bila ulazima.
  3. Hii itapunguza lawama kuwa nchi fulani inapeleka magonjwa kwenye nchi nyigine.
Zaidi ya hayo Ndugu Kenyatta nikushauri tu kwenye taharuki na majanga ndipo wajanja hupiga hela kwa kutengeneza '' fancy models'' ili kuhalalisha zabuni za dharura (emergency tenders). Na kwa hili ni lazima baada ya hii taharuki kutagundulika kashfa za matumizi mabaya na wizi wa fedha za serikali (embelzement and frauds of public funds) wakati itakuwa mmeshachelewa mtabaki kulaumiana na kuharibiana hadhi kwenye jamii. Huu ni mtandao mkubwa unaohusisha hadi ''vigogo'' wa taasisi kubwa kama IMF na WB.

Ningependa nikutaarifu tu ya kwamba nimeona taarifa kupitia television ya CNN kuwa baada ya kudhibiti hali ya ugonjwa wa Covid-19 Marekani wataanza uchunguzi wa kina (scuitiny) kwa taasisi zake kwasababu inaonekana ni kama kuna mchezo unaendelea kwa sababu za siasa, biashara na uchumi wa kimataifa.

Nimeona kwa mfano; licha ya Northen coridor ya nchi nne za jumuiya ya Afrika Mashariki kukutana bila Tanzania na Burundi kumekuwa na ''billateral arrangements'' baina ya Uganda, Rwanda na Tanzania ili kuruhusu mambo yaende. Bado kuna nafasi ya Tanzania na Kenya kufanya ''billateral arrangements''. Kumbuka Bandari ya Mombasa inapitisha baadhi ya shehena za DRC na baadhi ya nchi nyingine ikiwamo Tanzania hususani maeneo ya kanda ya ziwa Victoria. Kama kutakuwa na usumbufu hii biashara ndogo utaikosa, kwani shehena kubwa ya nchi hizi hupitia Tanzania. Ndio maana nimesema ili kukabiliana na Covid-19, unapaswa kusoma muongozo wa WHO huku ukishirikisha wataalamu wa biashara, sheria, miradi, uchumi na kadhalika ili kupata suluishi la jumla (holistic approach. Kuna msemo wa kiswahili unasema ''la kuambiwa changanya na za kwako''

Mwisho nikukumbushe; Covid-19 bado ipo sana, haitaisha kwa kufungia watu ndani au kufunga biashara bali kwa kutoa elimu ya afya, kuondo hofu na kujifunza jinsi ya kuishi nayo huku jitihada za ugunduzi wa kinga na tiba ukiendelea.

Tusipuuze dawa zetu za asili hasa ikizingatia ugonjwa huu umeonekana kuwa wanaopona ni wengi sana huku asimilia ndogo inakufa (si jambo jema). Tungeweza kuwatenga wazee na wenye maradhi sugu ingesaidia kupunguza vifo. Zaidi ya yote Kenyatta, Mungu yupo! sisi ni waja wake tusichoke kumsihi atupe mbinu ya kupambana na maradhi haya ambayo madhara yake yamekuzwa (overrated) kuliko uhalisia.

Ni malize kwa kukutakia kazi njema Mh. Rais

Wakudadavuwa
Mwanajumuiya ya Afrika Mashariki Mwandamizi.
 
Ndugu yangu Uhuru aka kamwana,

Kuna mambo umeyafanya ambayo yameleta ghadhabu wa wakenya sasa unataka kutupia lawama mataifa jirani kama ambavyo Trump anavyolaumu China kwa matatizo yake ya ndani.

Ushauri wangu tulia jifunze kutatua matatizo wa wanakenya kwa kutumia mikakati ya kimagharibi. Hili limekuwa tatizo kwenye nchi nyingi Afrika na inatokana zaidi na ukakasi wa viongozi wengi kukariri mitaala (curriculum) iliyotengenezwa kutatua changamoto za ulaya na Amerika. Hii imesababisha wafanya maamuzi wengi hasa wakurugenzi, makatibu wakuu badala ya kupata elimu wao hukazana kuzungumza kiingereza kwa lafudhi (accent) ya wazungu huku akitingisha kichwa na kushika nywele kichwani ili naye aonekane Mzungu hapa ndipo wazungu hutushangaa wanachofanya ni kukusifia huku wakikuzodoa (dharau).
Wewe umelishwa propaganda ukashiba kweli kweli! Nyie ndo mnaskia stori vijiweni na mnazichukulia kweli. Hii simulizi ya nchi ya Kenya kuiga hatua za magharibi ni stori za vijiweni. Tupe mfano, curfew ya usiku iliopo Kenya imeigwa toka nchi gani ya magharibi? Cessation of movement kati ya mitaa ya Nairobi na Mombasa imeigwa toka nchi gani ya magharibi?

Usituletee infriority complex yako binafsi hapa, wanapoongea wakurugenzi na makatibu wakuu, badala ya kusikiliza na kuhoji point wewe unaangalia rafudhi na kuangalia anavotingisha kichwa na kushika nywele? Huo ni wivu ama ushoga!

Mtu akitumia mbinu nzuri ambayo inafaa kwa mazingira husika usimchukie bali soma taratibu uchanganye na akili zako ili uweze kutafuta suluhisho sahihi kwa mazingira yako ili usiwaumize wananchi.
Huoni kama hicho ndo alichofanya Uhuru Kenyatta? Ndo maana nchi nyingi zilifanya total lockdown ila yeye akafanya curfew na cessation of movement.

tusitatue changamoto za Africa kwa kutumia ''blue print'' za IMF, WB, WHO na kadhalika bali tusome hizo ''blue prints'' tuchague yanayotufaa na tuite wataalamu wetu wa nyanja mbalimbali ili kutatua tatizo.
Umesema "tutumie wataalam" nikacheka!
Unaonaje ukamshauri kwanza rais wako kabla ya kumshauri rais wa kenya, tumeona wataalam wakitenguliwa kwa kutoa mtazamo wa kitaalam.
Saivi shule zinafunguliwa na michezo inaruhusiwa, kabla la hilo tamko uliskia jopo la wataalam wa afya limekaa likajadili? Punguza unafki!

Kwa mfano; ili kukabiliana na janga la Covid-19 inapasa viongozi wa Africa kusoma muongozo wa WHO (ambao kimsingi umejikita kwenye afya), lakini yatupasa kushirikisha wataalamu wa uchumi, biashara, miradi, kilimo, jamii na kadhalika ili kuja na mkakati wa jumla (Holistic approach) ambao utatekelezwa bila kuleta machungu sana kwa wananchi. Leo hii Ndugu Kenyatta ukitumia watu wako wa usalama wachunguze wanakenya wangapi wanakufa usishangae kuambiwa waliokufa na maradhi yanayosababishwa na njaa ikiwemo unyanyasaji ni wengi kuliko wanaokufa na Covid-19.
Ni kweli covid-19 imeua watu wachache ukilinganisha na maradhi yanayosababishwa na njaa na hata mafuriko lakini uwezekano wa covid-19 kuua watu wengi zaidi kwa mda mfupi ni mkubwa zaidi. Kwa mfano, waziri Umi alituambia asilimia 9% (takriban watu millioni 5) ya watanzania wana kisukari, sasa tafiti zinaonyesha covid-19 inaua zaidi ya asilimia 20% ya hawa watu yani watu zaidi ya milioni (>1,00,000) ndani ya miezi michache tu na hapo hatujajumlisha watu wenye HIV, pumu, matatizo ya figo, sickle cell........ nadhani unapata picha. Kutokana na tafiti hizi, kila inayoweza kuchukuliwa ni muhimu ichukuliwe mapema.

Kuhusu suala la madereva kusafirisha vitu mipakani linahitaji busara kubwa sana ili kuepuka malalamiko ya wananchi wa Afrika ya Mashariki. Ili kuepuka lawama kwamba madereva wa Tanzania ''wanaingiza Covid-19'' Kenya, Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro aliagiza kuwa mizigo yote inayoingia Kenya kupitia mipakani ishushwe kutoka magari ya Tanzania na kupakiwa kwenye magari ya Kenya yenye madereva wa Kenya ''wasioa na Covid-19'' ili kuzuia maambukizi na vilevile ile inayotoka Kenya ishushwe mpakan na kupakiwa kwenye magari yenye madereva wa Tanzania;
Nilishangaa sana watanzania wengi walivyoshabikia hii pin head thinking! Mambo hayaendi kienyeji hivi... yale malori yanayosafirisha samaki uatafaulishaje? Container, tenki za mafuta na gesi? Ndo maana balozi wa Kenya alituambia tupunguze hisia. Tulichofanya ni kuchukulia vitu personal. Walichotaka ni madereva kupimwa ili kuzuia kuenea kwa maambukizi alafu eti tukazuia malori ya kenya kuingia tanzania. How stupid!
mwisho wa siku, tumekubaliana tutapima ila tusitangaze utaifa wa mgonjwa!!

  1. Ni jambo lisilowezakana madereva kuwa kila siku hauumwi unapimwa mfano kwa dereva anayeingia Kenya/Tanzania mara tano kwa mwezi atalazimika kupimwa mara kumi kwa mwezi, yaani mara tano 5 na mara tano Tanzania. Ni nani anaweza kuvumilia?

  1. Unapimwa kila baada ya siku 14. Punguza vijiwe na tumia mda mwingi kutafuta taarifa rasmi sio propaganda.

    [*]Ucheleweshaji wa mizigo kusubiri vipimo umeharibu thamani ya bidhaa na mazao na pia kuongeza gharama ya biashara bila ulazima.
    [*]Hii itapunguza lawama kuwa nchi fulani inapeleka magonjwa kwenye nchi nyigine.
Ndo maana marais wa Africa mashariki walifanya kikao kupitia mtandao kupanga mikakati ili kuepusha madhara kama haya, sisi hatukutaka kuhusishwa alafu tunaletewa propaganda za "northern corridor".

Zaidi ya hayo Ndugu Kenyatta nikushauri tu kwenye taharuki na majanga ndipo wajanja hupiga hela kwa kutengeneza '' fancy models'' ili kuhalalisha zabuni za dharura (emergency tenders). Na kwa hili ni lazima baada ya hii taharuki kutagundulika kashfa za matumizi mabaya na wizi wa fedha za serikali (embelzement and frauds of public funds) wakati itakuwa mmeshachelewa mtabaki kulaumiana na kuharibiana hadhi kwenye jamii. Huu ni mtandao mkubwa unaohusisha hadi ''vigogo'' wa taasisi kubwa kama IMF na WB.

Ningependa nikutaarifu tu ya kwamba nimeona taarifa kupitia television ya CNN kuwa baada ya kudhibiti hali ya ugonjwa wa Covid-19 Marekani wataanza uchunguzi wa kina (scuitiny) kwa taasisi zake kwasababu inaonekana ni kama kuna mchezo unaendelea kwa sababu za siasa, biashara na uchumi wa kimataifa.
Hiyo ni reality ya maisha, always kutakua na wanaotaka kufaidika haijalishi how noble unachokifanya always wapo wanaofaidika ama kupiga hela, angali RED CROSS, UNICEF, UNDP, hadi makanisani na misikitini watu wanapiga hela. Hutakiwa kuacha kutoa huduma kwa kuogopa watu kupiga hela, cha muhimu ni mfumo wa ufuatiliaji.

Mwisho nikukumbushe; Covid-19 bado ipo sana, haitaisha kwa kufungia watu ndani au kufunga biashara bali kwa kutoa elimu ya afya, kuondo hofu na kujifunza jinsi ya kuishi nayo huku jitihada za ugunduzi wa kinga na tiba ukiendelea.
Tafuta elimu kujua rationale behind lockdown/social distancing/kunawa mikono/curfew/barakoa/kusalimiana kwa mkono na hatua zinginezo coz naona unaongea from a very ignorant space!

Tusipuuze dawa zetu za asili hasa ikizingatia ugonjwa huu umeonekana kuwa wanaopona ni wengi sana huku asimilia ndogo inakufa (si jambo jema). Tungeweza kuwatenga wazee na wenye maradhi sugu ingesaidia kupunguza vifo. Zaidi ya yote Kenyatta, Mungu yupo! sisi ni waja wake tusichoke kumsihi atupe mbinu ya kupambana na maradhi haya ambayo madhara yake yamekuzwa (overrated) kuliko uhalisia.

Ni malize kwa kukutakia kazi njema Mh.Raisi.

Wakudadavuwa
Mwanajumuiya ya Afrika Mashariki Mwandamizi.
Zaidi zaidi tunatakiwa kuweka juhudi zaidi kwenye utafiti wa dawa za asili..... tatizo letu tunasoma ila hatuelimiki!

Unasema "tuwatenge wazee na wenye maradhi sugu"?! kwa mfano wazee Tanzania ni wangapi? Wenye HIV ni wangapi, kisukari? Idadi hiyo ya watu utawatenga kwa style ipi?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe umelishwa propaganda ukashiba kweli kweli! Nyie ndo mnaskia stori vijiweni na mnazichukulia kweli. Hii simulizi ya nchi ya Kenya kuiga hatua za magharibi ni stori za vijiweni. Tupe mfano, curfew ya usiku iliopo Kenya imeigwa toka nchi gani ya magharibi? Cessation of movement kati ya mitaa ya Nairobi na Mombasa imeigwa toka nchi gani ya magharibi?

Usituletee infriority complex yako binafsi hapa, wanapoongea wakurugenzi na makatibu wakuu, badala ya kusikiliza na kuhoji point wewe unaangalia rafudhi na kuangalia anavotingisha kichwa na kushika nywele? Huo ni wivu ama ushoga!

Huoni kama hicho ndo alichofanya Uhuru Kenyatta? Ndo maana nchi nyingi zilifanya total lockdown ila yeye akafanya curfew na cessation of movement.


Umesema "tutumie wataalam" nikacheka!
Unaonaje ukamshauri kwanza rais wako kabla ya kumshauri rais wa kenya, tumeona wataalam wakitenguliwa kwa kutoa mtazamo wa kitaalam.
Saivi shule zinafunguliwa na michezo inaruhusiwa, kabla la hilo tamko uliskia jopo la wataalam wa afya limekaa likajadili? Punguza unafki!


Ni kweli covid-19 imeua watu wachache ukilinganisha na maradhi yanayosababishwa na njaa na hata mafuriko lakini uwezekano wa covid-19 kuua watu wengi zaidi kwa mda mfupi ni mkubwa zaidi. Kwa mfano, waziri Umi alituambia asilimia 9% (takriban watu millioni 5) ya watanzania wana kisukari, sasa tafiti zinaonyesha covid-19 inaua zaidi ya asilimia 20% ya hawa watu yani watu zaidi ya milioni (>1,00,000) ndani ya miezi michache tu na hapo hatujajumlisha watu wenye HIV, pumu, matatizo ya figo, sickle cell........ nadhani unapata picha. Kutokana na tafiti hizi, kila inayoweza kuchukuliwa ni muhimu ichukuliwe mapema.

Nilishangaa sana watanzania wengi walivyoshabikia hii pin head thinking! Mambo hayaendi kienyeji hivi... yale malori yanayosafirisha samaki uatafaulishaje? Container, tenki za mafuta na gesi? Ndo maana balozi wa Kenya alituambia tupunguze hisia. Tulichofanya ni kuchukulia vitu personal. Walichotaka ni madereva kupimwa ili kuzuia kuenea kwa maambukizi alafu eti tukazuia malori ya kenya kuingia tanzania. How stupid!
mwisho wa siku, tumekubaliana tutapima ila tusitangaze utaifa wa mgonjwa!!


  1. Unapimwa kila baada ya siku 14. Punguza vijiwe na tumia mda mwingi kutafuta taarifa rasmi sio propaganda.
Ndo maana marais wa Africa mashariki walifanya kikao kupitia mtandao kupanga mikakati ili kuepusha madhara kama haya, sisi hatukutaka kuhusishwa alafu tunaletewa propaganda za "northern corridor".


Hiyo ni reality ya maisha, always kutakua na wanaotaka kufaidika haijalishi how noble unachokifanya always wapo wanaofaidika ama kupiga hela, angali RED CROSS, UNICEF, UNDP, hadi makanisani na misikitini watu wanapiga hela. Hutakiwa kuacha kutoa huduma kwa kuogopa watu kupiga hela, cha muhimu ni mfumo wa ufuatiliaji.

Tafuta elimu kujua rationale behind lockdown/social distancing/kunawa mikono/curfew/barakoa/kusalimiana kwa mkono na hatua zinginezo coz naona unaongea from a very ignorant space!


Zaidi zaidi tunatakiwa kuweka juhudi zaidi kwenye utafiti wa dawa za asili..... tatizo letu tunasoma ila hatuelimiki!

Unasema "tuwatenge wazee na wenye maradhi sugu"?! kwa mfano wazee Tanzania ni wangapi? Wenye HIV ni wangapi, kisukari? Idadi hiyo ya watu utawatenga kwa style ipi?



Sent using Jamii Forums mobile app
Hata kafyuu kwa Wakenya haifai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata kafyuu kwa wakenya haifai

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ni maneno yako,
Kwa mfano; ili kukabiliana na janga la Covid-19 inapasa viongozi wa Africa kusoma muongozo wa WHO (ambao kimsingi umejikita kwenye afya), lakini yatupasa kushirikisha wataalamu wa uchumi, biashara, miradi, kilimo, jamii na kadhalika ili kuja na mkakati wa jumla (Holistic approach).
Kutokana na ushauri wako, Kwaiyo we ni mtaalam wa uchumi, biashara, miradi, kilimo, jamii na kadhalika?

Pale unapokosa hoja jua kukaa kimya napo panahitaji maarifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakudadavuwa,
mmoja hivi muandika threads JF kama akina Wyatt Mathewson eti anamuelekeza Uhuru Kenyatta how to run Kenya?

Like really?

Kufunga mpaka na TZ kuna uhusiano gani na his performance kwa wananchi wake?

Kilichokupelekea wewe kuandika hii makala mamluki ni sababu ya kufunga mpaka wake na TZ kulinda watu wake?

Maana hapa EA,Tanzania ni kiwanda cha kuzalisha virus vya Covid-19,yeye kwa busara ya kulinda raia wake kafunga mpaka,then wewe unakuja kumuelekeza cha kufanya nchini kwake?

Kufunga mpaka wake na TZ hajaingilia TZ,kafunga upande wake,hoja yako eti kaingilia mambo ya TZ ni uongo!
 
Ahsante kwa maelezo na maelekezo.

Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana.


Cc: mahondaw
 
Mpuuzi mmoja hivi muandika threads JF kama akina Wyatt Mathewson eti anamuelekeza Uhuru Kenyatta how to run Kenya?????

Like really?

Kufunga mpaka na TZ kuna uhusiano gani na his performance kwa wananchi wake?

Kilichokupelekea wewe kuandika hii makala mamluki ni sababu ya kufunga mpaka wake na TZ kulinda watu wake?

Maana hapa EA,Tanzania ni kiwanda cha kuzalisha virus vya Covid-19,yeye kwa busara ya kulinda raia wake kafunga mpaka,then wewe unakuja kumuelekeza cha kufanya nchini kwake?

Kufunga mpaka wake na TZ hajaingilia TZ,kafunga upande wake,hoja yako eti kaingilia mambo ya TZ ni uongo!
Mwambie baada ya kuipigia magoti Tanzania sasa akampigie magoti Museveni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom