habari wanayanga wote.
huu ujumbe nitashukuru sana tukiutoa kwa pamoja kwa kuweka maoni yetu kwa timu yetu pendwa..
najua wengi tunaona yanayotokea kwa timu yetu.. mishahara ya wachezaji, gharama za usafiri na mengi yamekuwa kitendawili kisa tajiri wetu mpendwa.. mwanayanga mwenzetu manji amekaa pembeni..
Huwa nawaza sana hali hii ya kumtegemea mtu mmoja au kikundi cha watu wachache matajiri kuzamini na kuendesha timu itaisha lini ? nawaza tu siku manji akifariki, je tutaenda kumlilia mke wake kumuomba hela za mishahara hata kama yeye haipendi yanga au hapendi mpira?
ningependa sana kuona timu inaondoka huu mfumo wa kumtegemea mtu mmoja au wachache kiholela..
Maoni yangu mimi ni haya..
1. Yanga haifanikiwi na ni maskini sababu ya vipaumbele vya pesa na matumizi mabovu
hapa namaanisha timu ambayo haina kipato kikubwa imeajiri watu wengi sana ambao wanalipwa mishahara na posho ila role zao au majukumu yao hayana ulazima.. vyeo kama msemaji wa timu etc vingefutwa kupunguza gharama za mishahara msemaji wa timu anabaki kocha tu.. kama ulaya vile..
wangeitwa wataalamu , makampuni ya taaluma kama pwc, kpmg, delloite etc waje wathaminishe majukumu ya kila cheo.. kisha washauri role gani ziunganishwe na role gani zifutwe baada ya hapo kuwe na redundancy ya wasio na ulazima, na pia mishahara ipangwe kwa uhalisia..
2. Yanga haifanikiwi sababu ina poor marketing policy
hapa namaaisha yanga haijatangazi inavyotakiwa,, haitumii jina lake na mtaji wake wa mashabiki mamilioni kutengeneza pesa zake yenyewe.. mfano haina strong website, social network accounts, online tv etc... yanga ina uwezo wa kuwa na tv yake hata online tu kama millard hayo ambayo ingeendeshwa kisasa ingepata matangazo yake kama vodacom, tbl na makampuni binafsi, na bado kula hela za adsense ambazo zingeongeza mapato ya timu.. strong instagram accounts zingepost matangazo pia kama WCB wanavyofanya.. sitaki amini diamond ni smart than yanga management
3. ufatiliaji wa matumizi mabaya ya nembo na mauzo ya jezi feki ni mbovu
Hapa namaanisha mashabiki wengi wa yanga tunavaa jezi feki.. jezi zimejaa kariakoo na nchi nzima zina nembo za yanga ila ni feki... yanga haipati hata mia mauzo ya zile jezi feki.. unaenda taifa unakuta mashabiki wa yanga tumejaa kibao na njano na kijani zetu.. ila karibu wote tumevaa jezi feki ambazo club haijapata hata mia... kuwe na watu wa kufatilia wauzaji wa jezi feki na kuwashtaki na kwa kushirikiana na jeshi la polisi hii inawezekana kabisa ikiwekwa mfumo mzuri.. mauzo ya jezi yaifaidishe club..
4. Matumizi mabovu ya michango ya wanachama nayo ni sababu ya timu kulia ukata
wanachama tunalipia kadi kila mwaka, ila hela hizo hazieleweki zinaenda wapi... dunia ya sasa hela zinavunja uaminifu.. kuwe na mfumo rasmi wa kucontrol hela.. kila hela itoke kwa sababu.. hata kama ni 1000 tu au mia tano itoke kwa mbinde baada ya kuidhinishwa na ma signatories kibao...
hela ikiwa inatunzwa vizuri hii itashawishi hata mashabiki tukichangishwa tunatoa kwa moyo.. kuna wamachinga, wauza chips, boda boda, mama lishe wengi tu hawana kipato kikubwa ila wanaipenda sana yanga yetu,, kwamba ukimwambia arushe 1000 tigo pesa kuchangia timu yake yanga anatoa kwa amani kabisa.. ila sababu anajua kwa sasa hata nikitoa inaliwa na wezi viongozi na kulipana maposho hawezi kutoa kiurahisi...
mwenyekiti manji aliwahi kusema idadi ya mashabiki wa yanga ni kama milioni 35.. sina uhakika kama ni sahihi
Eti Yanga ina mashabiki 35 milioni!
sasa timu yenye mashabiki wengi hivyo inalia njaa.. si zaidi ya uchizi
timu yenye mashabiki wengi hivyo haijawai fika hata nusu fainali ya caf champions league.. kweli ujamaa umetulemaza.. yanga ni kubwa kuliko mazembe, kubwa kuliko enyimba, kubwa kuliko zanaco, kubwa kuliko APR sijui tumelogwa na nani
wanayanga wengine mnaruhusiwi kutoa maoni yenu.. Tunakosea wapi
Mimi yanga kwa jinsi navyoipenda hata kwa kukopa sishindwi ichangia buku buku kila mwezi.. kama tukiamua wanayanga tulipe mishahara ya wachezaji wenyewe kwa kuchanga.. ila sitachanga bila kuona mfumo rasmi wa kuzitunza hizi pesa za michango
by freshman aka Adam mwanayanga tawi la yanga Mabibo Hostel
huu ujumbe nitashukuru sana tukiutoa kwa pamoja kwa kuweka maoni yetu kwa timu yetu pendwa..
najua wengi tunaona yanayotokea kwa timu yetu.. mishahara ya wachezaji, gharama za usafiri na mengi yamekuwa kitendawili kisa tajiri wetu mpendwa.. mwanayanga mwenzetu manji amekaa pembeni..
Huwa nawaza sana hali hii ya kumtegemea mtu mmoja au kikundi cha watu wachache matajiri kuzamini na kuendesha timu itaisha lini ? nawaza tu siku manji akifariki, je tutaenda kumlilia mke wake kumuomba hela za mishahara hata kama yeye haipendi yanga au hapendi mpira?
ningependa sana kuona timu inaondoka huu mfumo wa kumtegemea mtu mmoja au wachache kiholela..
Maoni yangu mimi ni haya..
1. Yanga haifanikiwi na ni maskini sababu ya vipaumbele vya pesa na matumizi mabovu
hapa namaanisha timu ambayo haina kipato kikubwa imeajiri watu wengi sana ambao wanalipwa mishahara na posho ila role zao au majukumu yao hayana ulazima.. vyeo kama msemaji wa timu etc vingefutwa kupunguza gharama za mishahara msemaji wa timu anabaki kocha tu.. kama ulaya vile..
wangeitwa wataalamu , makampuni ya taaluma kama pwc, kpmg, delloite etc waje wathaminishe majukumu ya kila cheo.. kisha washauri role gani ziunganishwe na role gani zifutwe baada ya hapo kuwe na redundancy ya wasio na ulazima, na pia mishahara ipangwe kwa uhalisia..
2. Yanga haifanikiwi sababu ina poor marketing policy
hapa namaaisha yanga haijatangazi inavyotakiwa,, haitumii jina lake na mtaji wake wa mashabiki mamilioni kutengeneza pesa zake yenyewe.. mfano haina strong website, social network accounts, online tv etc... yanga ina uwezo wa kuwa na tv yake hata online tu kama millard hayo ambayo ingeendeshwa kisasa ingepata matangazo yake kama vodacom, tbl na makampuni binafsi, na bado kula hela za adsense ambazo zingeongeza mapato ya timu.. strong instagram accounts zingepost matangazo pia kama WCB wanavyofanya.. sitaki amini diamond ni smart than yanga management
3. ufatiliaji wa matumizi mabaya ya nembo na mauzo ya jezi feki ni mbovu
Hapa namaanisha mashabiki wengi wa yanga tunavaa jezi feki.. jezi zimejaa kariakoo na nchi nzima zina nembo za yanga ila ni feki... yanga haipati hata mia mauzo ya zile jezi feki.. unaenda taifa unakuta mashabiki wa yanga tumejaa kibao na njano na kijani zetu.. ila karibu wote tumevaa jezi feki ambazo club haijapata hata mia... kuwe na watu wa kufatilia wauzaji wa jezi feki na kuwashtaki na kwa kushirikiana na jeshi la polisi hii inawezekana kabisa ikiwekwa mfumo mzuri.. mauzo ya jezi yaifaidishe club..
4. Matumizi mabovu ya michango ya wanachama nayo ni sababu ya timu kulia ukata
wanachama tunalipia kadi kila mwaka, ila hela hizo hazieleweki zinaenda wapi... dunia ya sasa hela zinavunja uaminifu.. kuwe na mfumo rasmi wa kucontrol hela.. kila hela itoke kwa sababu.. hata kama ni 1000 tu au mia tano itoke kwa mbinde baada ya kuidhinishwa na ma signatories kibao...
hela ikiwa inatunzwa vizuri hii itashawishi hata mashabiki tukichangishwa tunatoa kwa moyo.. kuna wamachinga, wauza chips, boda boda, mama lishe wengi tu hawana kipato kikubwa ila wanaipenda sana yanga yetu,, kwamba ukimwambia arushe 1000 tigo pesa kuchangia timu yake yanga anatoa kwa amani kabisa.. ila sababu anajua kwa sasa hata nikitoa inaliwa na wezi viongozi na kulipana maposho hawezi kutoa kiurahisi...
mwenyekiti manji aliwahi kusema idadi ya mashabiki wa yanga ni kama milioni 35.. sina uhakika kama ni sahihi
Eti Yanga ina mashabiki 35 milioni!
sasa timu yenye mashabiki wengi hivyo inalia njaa.. si zaidi ya uchizi
timu yenye mashabiki wengi hivyo haijawai fika hata nusu fainali ya caf champions league.. kweli ujamaa umetulemaza.. yanga ni kubwa kuliko mazembe, kubwa kuliko enyimba, kubwa kuliko zanaco, kubwa kuliko APR sijui tumelogwa na nani
wanayanga wengine mnaruhusiwi kutoa maoni yenu.. Tunakosea wapi
Mimi yanga kwa jinsi navyoipenda hata kwa kukopa sishindwi ichangia buku buku kila mwezi.. kama tukiamua wanayanga tulipe mishahara ya wachezaji wenyewe kwa kuchanga.. ila sitachanga bila kuona mfumo rasmi wa kuzitunza hizi pesa za michango
by freshman aka Adam mwanayanga tawi la yanga Mabibo Hostel