kichwaones
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 399
- 49
kama kuna uwezekano wa kujiajiri inakuwa bora zaidi kuliko kutafuta vibarua ofisini kwa watu
nampa pole sana huyo dada kama hii stori ni kweli!Habari zenu ndugu watanzania wenzangu. Katika hali isiyo ya kawaida, jana nilipokuwa ofisini kwangu mida ya saa tano na nusu asubuhi alikuja dada mmoja ambaye ni graduate, alikuwa anaonekana amechoka na kweli anashida ya kazi. Alitela barua yake ya maombi ya kazi then akaikabidhi kwa ofisi ya human resources ambayo tumetenganishwa na partition za vioo, hivyo mnaweza kuona kinachoendelea ofisi nyingine. Baada ya yule dada kukabidhi ile barua kwa HR na kuondoka, barua ile ilichanwa muda ule ule bila wao kufahamu kama nilikuwa ninawaona. Na inasemekana nafasi ile ya assistant accountant tayari mtoto wa dada yake huyu HR manager wetu hapa ofisini tayari ameshachukuliwa. Poleni sana graduates mnaohangaika kutafuta kazi, haya ndio yanayowakuta ambayo mlikuwa hamyafahamu!
futa kauli yako! mkuuhr wengi wapuzi sana
futa kauli yako! mkuu
hizo taaluma za watu kama ilivyo yako
mimi kuna kipindi niliitwa kwenye interview nilivyoingia nikaulizwa "what is your good name?"nikajibu.nikaambiwa basi subiri nje tutakuita interview ya pili.baadae wakatoka wakaita watu watatu.sisi tuliobakia tukawa tumeshindwa interview.nilishangaa lakini pia nilicheka sana.Duh! Tutatoboa kweli kwa mtindo huu
inaonekana uliwapaga wakakumegaga alafu kazi hawakukupaga!Afute kwnn?
Kweli ni wapuuzi!na ndo maana most of them they die na mdudu coz of rushwa ya ngono
utakuwa ni wewe wewe! koma, shame on u!
asante kwa kutujuza yanayotokea ofisinii kwenu...Ingawa mgeni Jamvini siku nyingine ukiingia piga hodi
Duh!Aisee,inauma saana.Kwa mfano huyo Hr wenu nae ni member humu jamvini,na ktk fukua fukua zake akafanikiwa ku uona huo uzi uliou post huoni kua utakua umekiotesha nyasi kibarua chako?Cause,obvious atajua ni wewe.
Ni ofisi ya umma au ya binafsi?
Je kazi ilitangazwa?
Kama ni ofisi binafsi/private na kazi aikutangazwa,
ulitaka afuge karatasi za nini wakati watu wanataka paper-less offices?
nampa pole sana huyo dada kama hii stori ni kweli!
inawezekana ametumia hela kuandaa hiyo application alafu mpuuzi mwingine anamfanyia unyama
lakini hr kama alichana akijua kuwa nafasi tayari inamwenyewe yuko sahii
inawezekana kuna cv,ambayo si vizuri ionekane kwa kila mtu
nikirudi kwa mtoa thread ,sijambo jema kudisclose information za ofisini kwako
vingine vinafanywa kulinda maslahi ya ofisi
siku nyingine jitahidi kuleta thread za kutia matumaini sio za kutisha wadogo zetu
kama kuna uwezekano wa kujiajiri inakuwa bora zaidi kuliko kutafuta vibarua ofisini kwa watu
nipe mtaji nijiajiri