Barua za uteuzi Zanzibar zinaandikwa kwa ufasaha, Jamuhuri igeni

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Barua zote za uteuzi za Rais wa Zanzibar zina kifungu Cha sheria au katiba kinachompa Rais mamlaka ya uteuzi.

Barua za Muungano zinakosa hiki kipengele muhimu sijui kwanini, naamini ipo haja ya kuiga wenzetu wanavyooandika.

Japo font, mpangilio wa haya barua za Msigwa zinavutia zaidi.

Mwisho, pamoja na katiba kutoa mamlaka baadhi ya nafasi zimetamkwa kwenye sheria za taasisi anayokwenda kusimamia mteule, kifungu Cha sheria kinachotoa mamlaka ni vyema kikainishwa pia.

Wapo wateule ambao hata kifungu Cha katiba na sheria kilichowafanya wateuliwe hawakijui....... na Hawa ndio wengi kwa taasisi za umma.
 
Kwahiyo wasipoweka hicho kipengele wanakuwa wamekiuka sheria?
 
Barua? Kwamba Msigwa huwa anatuandikia "barua" za teuzi na tenguzi?
 
Mmmh, wewe mleta Mada unamtafuta jiwe. Wewe hujui teuzi nyingi za jiwe ziko nje ya sheria sasa unataka aweke kipengele gani cha sheria?
 
Nadhani unaongelea taarifa kwa vyombo vya habari
Rais anapoteua mtu, katibu mkuu kiongozi anaandika barua ya uteuzi, humu kuna kila kitu
 
Zipo nyanja kibao tuu sheria inakiukwa hapa nchini kwetu, na imekuwa ni desturi kama vile tunaongozana kwa miiko na hisia.
 
Wapinzani ndio walituchelewesha tena hata barua haina ulazima wa kuandika sie tuko chama kimoja kama enzi za TANU au nasema uongo ndugu zangu?
 
Acha waendelee hivyo hivyo, kwa sababu hata viapo na katiba yenyewe awaheshimu!
 
Hilo tu, ndo unaona ni ufasaha wa kuigwa? Yaani kila siku liwe darasa la sheria na katiba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…