BASATA: Wawanyime Kibali Waigizaji Wa Bongo Movies Wanaopiga Picha Za Uchi

Ibrahim300

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2010
Posts
390
Reaction score
68
Hii Bongo Movies siku hizi imekuwa kama laana kwa kizazi cha siku hizi nchini Tanzania. Ni jambo la kusikitisha kuwa kila siku kila wakati utasikia mwigizaji huyu ama yule amepiga picha za ufuska na kuzianika kwa mtandao.

Jambo lililoniudhi zaidi ni hivi majuzi nilipoingia katika blog fulani ya udaku ya Jambo Tanzanian na kuona stori na picha za wasanii wa Bongo Movies wamepiga picha wakiwa uchi. Tatizo ni kuwa picha hizo hazikuwa fumanizi wala nini bali zilikuwa ni picha zilizopigwa kwa zamu. Wamejipanga matumbo yao huku wakitabasamu mbele ya kamera bila haya wala uoga wowote.

Utamaduni wa kiafrika umeenda wapi jamaa?

Nimepongeza hatua ya BASATA kumfungia Snura video yake ya 'kimajanga' na nawaomba kama wana uwezo wa kuwafungia hawa wasanii wengine wanaochukua advantage ya miili yao ili kudhania watapata umaarufu ingekuwa vyema.

Tatizo hili naliona limeanza kuenea hadi shule za sekondari na hivi karibuni nahofia shule za misingi wanashika mkondo. Kuna blogs nyingi zinazoonyesha wanafunzi nao wakipiga picha za uchi.

Serikali kama inaweza kuingiza mkono wake kwa janga hili naona itakuwa ni bora kwani itaokoa jahazi kutozama.

Kuna ule msemo wa kiswahili unaosema 'samaki mkunje angali bado mbichi.'
 
Hakuna mwanamke ambaye atapata kibali katika hiyo industry, make wanafanana kama njiti za kiberiti...
 
Sasa kwani ofice za Basata zimo humu jf?
 
Sasa kwani ofice za Basata zimo humu jf?

Wacha kuogopa kufikiria wewe. Nimetoa tu maoni yangu hapa. Waishi dunia gani wewe ama umejibu ili ufurahishe watu? coz me sioni kitu cha kufurahisha hapa.

Watu wakitoa maoni yao katika vyombo vya habari haimaanishi lazima maoni yao yatimizwe
 
Wacha kuogopa kufikiria wewe. Nimetoa tu maoni yangu hapa. Waishi dunia gani wewe ama umejibu ili ufurahishe watu? coz me sioni kitu cha kufurahisha hapa.

Watu wakitoa maoni yao katika vyombo vya habari haimaanishi lazima maoni yao yatimizwe
Xaxa na yeye katoa maoni kuendana na ujazo wa akili yake.unaweza kuta akili yake ni nusu na robo tutafanyaje xaxa?
 
Wacha kuogopa kufikiria wewe. Nimetoa tu maoni yangu hapa. Waishi dunia gani wewe ama umejibu ili ufurahishe watu? coz me sioni kitu cha kufurahisha hapa.

Watu wakitoa maoni yao katika vyombo vya habari haimaanishi lazima maoni yao yatimizwe

Nimekusaidia kufikiri maana ingekua vyema ukaenda kazin kwao panapohusika halafu ukatupa taarifa umefanikisha au la!ni maoni tu
 
unamaoni mazuri sana,wanaharibu maadili na wanatumia filamu kama kujitangaza na si kuelimisha jamii.
 
Nimekusaidia kufikiri maana ingekua vyema ukaenda kazin kwao panapohusika halafu ukatupa taarifa umefanikisha au la!ni maoni tu

Jamiiforum hutembelewa na watu kila aina so kuweka maoni yangu hapa huwezi kujua nani atayasoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…