Bashe anapaswa kujibu hili, amefeli kwenye kilimo. Hili la mbolea limeumbua, angalia idadi

Bashe anapaswa kujibu hili, amefeli kwenye kilimo. Hili la mbolea limeumbua, angalia idadi

Per Diem

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2018
Posts
2,189
Reaction score
3,724
Kuna nguvu ilitumika sana kwenye suala la mbolea mwaka jana, nyimbo zilitungwa na sifa ziliimbwa kwa waziri bashe kuhusu mbolea ya ruzuku.

Bashe akasema anataka kumuinua mkulima ndio maana anasaidia wakulima wote wapate mbolea ya ruzuku.

Hafla ya mbolea ya ruzuku kwa wakulima ilifanyika mbeya siku ya nanenane na mgeni rasmi alikua raisi samia. Karibu nusu ya mawaziri walihudhuria ile hafla ya ugawaji mbolea ya ruzuku.

Bajeti ikasifiwa kuwa ni ya kihistoria haijawahi kutokea. Sasa leo mwaka wa bajeti umeisha turudi kwenye uhalisia kuhusu hayo yaliyofanyika mwaka jana, tuone ukweli na uongo ulipo.

Lengo ilikuwa ni kusajili wakulima milioni 7, waliofanikiwa kusajiliwa ni wakulima milioni 2, waliofanikiwa kupata mbolea ni wakulima laki 8.

Haya waziri alipaswa kuyasema na sio kuyamezea. lengo ni kuwajuza kama ilivyofanyika wakati wa uzinduzi, huo ndo utakua msema ukweli na utasaidia watu wajue mapungufu yapo wapi na kukusaidia kuyatatua.

Chini ni idadi ya wakulima kila mkoa waliopata mbolea ya ruzuku. Mkoa kama rukwa na katavi ambao unasifika kwa kilimo, waliopata mbolea ni 10,000 tu. Mkoa ambao una wakulima zaidi ya laki 5 (sensa). Hapo tafsiri yake wakulima zaidi ya laki 490,000 hawakupata hiyo mbolea.

Bado tunataka tusubiri mwaka ujao?

20230510_121252.jpg
 
1. CCM ni tatizo kuu nchini.
Mtu yeyote akitaka kuliona na kulijua hilo liko wazi tu kama bahari au ziwa lisivyojificha.

2. Bashe ni fisadi - amezaliwa na kulelewa kifisadi, amefika hapo kifisadi na anatenda kifisadi. What do we expect?

3. "Utawala" wa nchi unaendeshwa na mfumo wa kifisadi - aliyekuwa Waziri Mkuu Awamu ya Nne aliwahi kukiri wazi wazi. Hata Mwl Nyerere aliwahi kukiri kuwepo kwa hiyo kitu kwenye utawala wake, Awamu ya Kwanza.
Kwa hiyo Bashe hayuko peke yake. Ni mfumo. Ni kundi, ni mtandao mpana na wenye nguvu. Na umekomaa sasa.

Kila Awamu nchini imekuwa na magenge yake ya kifisadi. Yanabadilishana tu kula kwa zamu, na kutesa kwa zamu. Propaganda za usafi au uadilifu ni uongo wa kitoto.

4. "Miradi" mingi ya Serikali, kwa sehemu kubwa, hulenga kwanza kuwanufaisha wao/wapigaji.
Chenji inayobaki au makombo hiyo ndio halali ya wananchi. Yaani hata mradi wa shs 10 million, ndani yake kuna upigaji! Kila mahali!!

Tofauti huwa ni upatikanaji/ukosefu wa taarifa (publicity) za ufisadi.
Ila hii nchi imekuwa ikitafunwa haswa.

Solutions:
Tumeshajaribu njia nyingi - kuunda TAKUKURU, 'Vitengo', Tume/Kamati, 'Task Forces' nk nk lakini TUKAFELI. Matokeo ndiyo haya haya ya akina Bashe, Mwigulu, Januari na wenzao. Yatosha sasa!

Njia pekee na sahihi ni kupata Katiba Mpya, na hii hatujawahi kuijaribu. Ajabu kweli!

Lazima tuanzie kutibu matatizo yetu kwenye shina. Katiba ndiyo shina.
Pamoja na manufaa mengine, tutakuwa na "nguvu" (sio hii geresha ya sasa) ya kuwachagua na kuwawajibisha viongozi na watendaji wa Serikali.
Tutaibiwa na kunyonywa hadi lini?
 
Kuna nguvu ilitumika sana kwenye suala la mbolea mwaka jana, nyimbo zilitungwa na sifa ziliimbwa kwa waziri bashe kuhusu mbolea ya ruzuku.

Bashe akasema anataka kumuinua mkulima ndio maana anasaidia wakulima wote wapate mbolea ya ruzuku.

Hafla ya mbolea ya ruzuku kwa wakulima ilifanyika mbeya siku ya nanenane na mgeni rasmi alikua raisi samia. Karibu nusu ya mawaziri walihudhuria ile hafla ya ugawaji mbolea ya ruzuku.

Bajeti ikasifiwa kuwa ni ya kihistoria haijawahi kutokea. Sasa leo mwaka wa bajeti umeisha turudi kwenye uhalisia kuhusu hayo yaliyofanyika mwaka jana, tuone ukweli na uongo ulipo.

Lengo ilikuwa ni kusajili wakulima milioni 7, waliofanikiwa kusajiliwa ni wakulima milioni 2, waliofanikiwa kupata mbolea ni wakulima laki 8.

Haya waziri alipaswa kuyasema na sio kuyamezea. lengo ni kuwajuza kama ilivyofanyika wakati wa uzinduzi, huo ndo utakua msema ukweli na utasaidia watu wajue mapungufu yapo wapi na kukusaidia kuyatatua.

Chini ni idadi ya wakulima kila mkoa waliopata mbolea ya ruzuku. Mkoa kama rukwa na katavi ambao unasifika kwa kilimo, waliopata mbolea ni 10,000 tu. Mkoa ambao una wakulima zaidi ya laki 5 (sensa). Hapo tafsiri yake wakulima zaidi ya laki 490,000 hawakupata hiyo mbolea.

Bado tunataka tusubiri mwaka ujao?

View attachment 2617905
Kwa hiyo hoja Yako ni ipi? Kwnaza mpaka hapo amefaulu maana kiasi kikubwa Cha mbolea kimeenda kwenye Mikoa inayozalisha chakula..

Pili pesa zimekuja kupatikana wakati msimu wa Kilimo umekwishaanza Kwa hiyo ulitegemea iwaje?

Mwisho usajili unaendelea na mbolea zipo za kutosha so msimu ujao Hautakuwa na Changamoto kama za msimu uliopita..

Mnahangaika sana na Bashe baada ya nyie kushindwa kufanya hata hicho alichofanikisha Waziri Bashe.
 
Sasa pesa ambazo zingetakiwa kuongezwa kwenye ruzuku ya mbolea kwa wakulima ndo zinaenda kufanya maonyesho ya shamba darasa, siyo? waache hizi janja janja za kupiga pesa za umma.
 
1. CCM ni tatizo kuu nchini.
Mtu yeyote akitaka kuliona na kulijua hilo liko wazi tu kama bahari au ziwa lisivyojificha.

2. Bashe ni fisadi - amezaliwa na kulelewa kifisadi, amefika hapo kifisadi na anatenda kifisadi. What do we expect?

3. "Utawala" wa nchi unaendeshwa na mfumo wa kifisadi - aliyekuwa Waziri Mkuu Awamu ya Nne aliwahi kukiri wazi wazi. Hata Mwl Nyerere aliwahi kukiri kuwepo kwa hiyo kitu kwenye utawala wake, Awamu ya Kwanza.
Kwa hiyo Bashe hayuko peke yake. Ni mfumo. Ni kundi, ni mtandao mpana na wenye nguvu. Na umekomaa sasa.

Kila Awamu nchini imekuwa na magenge yake ya kifisadi. Yanabadilishana tu kula kwa zamu, na kutesa kwa zamu. Propaganda za usafi au uadilifu ni uongo wa kitoto.

4. "Miradi" mingi ya Serikali, kwa sehemu kubwa, hulenga kwanza kuwanufaisha wao/wapigaji.
Chenji inayobaki au makombo hiyo ndio halali ya wananchi. Yaani hata mradi wa shs 10 million, ndani yake kuna upigaji! Kila mahali!!

Tofauti huwa ni upatikanaji/ukosefu wa taarifa (publicity) za ufisadi.
Ila hii nchi imekuwa ikitafunwa haswa.

Solutions:
Tumeshajaribu njia nyingi - kuunda TAKUKURU, 'Vitengo', Tume/Kamati, 'Task Forces' nk nk lakini TUKAFELI. Matokeo ndiyo haya haya ya akina Bashe, Mwigulu, Januari na wenzao. Yatosha sasa!

Njia pekee na sahihi ni kupata Katiba Mpya, na hii hatujawahi kuijaribu. Ajabu kweli!

Lazima tuanzie kutibu matatizo yetu kwenye shina. Katiba ndiyo shina.
Pamoja na manufaa mengine, tutakuwa na "nguvu" (sio hii geresha ya sasa) ya kuwachagua na kuwawajibisha viongozi na watendaji wa Serikali.
Tutaibiwa na kunyonywa hadi lini?
Wakala wa katiba mpya katika ubora wako, umeandika mengi lakini lengo haswa ni kuipigia debe katiba mpya.

Uwepo wa katiba mpya hauondoi hulka ya wizi, kama imekuwepo tangu taifa hili likiwa changa haiwezi kuondolewa kwa vifungu vya kanuni za katiba mpya.
 
Suala la mbole ni nyeti sana katika usalama wa chakula, kimsingi ni usalama wa nchi.

Nashangaa sana vyombo vya ulinzi hasa TISS, ni kama hawaoni hii party ya chakula kuwa nyeti kwa usalama wa nchi.

Ilitakiwa iwe mguu kwa mguu kuhakikisha hii wizara ya kilimo na wote wadau hawaleti mchezo mchezo.
 
Wakala wa katiba mpya katika ubora wako, umeandika mengi lakini lengo haswa ni kuipigia debe katiba mpya.

Uwepo wa katiba mpya hauondoi hulka ya wizi, kama imekuwepo tangu taifa hili likiwa changa haiwezi kuondolewa kwa vifungu vya kanuni za katiba mpya.
Wewe ni wakala hivyo unadhani kila mtu ni wakala, mimi ni Mtanzania ninayejitambua. Hilo ulitambue.


Hatujawahi kuwa na Katiba Mpya, sasa kwa nini tuamini hisia zako?

Kwanza tupate katiba mpya, hayo ya kuwaje tutajua wenyewe!
 
Back
Top Bottom