Bashe: Hata usiposajiliwa, utapata mbolea kwa bei ya ruzuku

Bashe: Hata usiposajiliwa, utapata mbolea kwa bei ya ruzuku

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Ziara ya Rais Samia Suluh Hassan Mkoani Njombe, kijiji cha Mtwango.

Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe ametoa uhakika wa upatikanaji wa mbolea kwa bei ya ruzuku hata kwa wakulima ambao hawatakuwa wamesajiliwa baada ya muda huo kufika. Hii inatoa ahueni kwa wakulima waliokuwa na wasiwasi juu ya utaratibu huu mpya wa kujisajili ili kuwa mnufaika wa nafuu ya punguzo ya bei ya mbolea iliyotangazwa na serikali.

Waziri Bashe amewataka wakulima wote, hata wale wasiosajiliwa kufika kwa mawakala watakao orodheshwa hapo baadae ili kupata mbolea kwa bei ya ruzuku kwani serikali itaweka utaratibu wa kuwasajili hapohapo pasipo usumbufu. Katika kuhitimisha hotuba hii fupi, Rais amewaomba viongozi wa serikali kukusanya mapato vizuri kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa.​
 
Bashe anajitahidi sana katika Wizara ya kilimo kutatua changamoto za wakulima. Tatizo letu kubwa ni soko la uhakika la mazao yetu.
 
Bashe anajitahidi sana katika Wizara ya kilimo kutatua changamoto za wakulima. Tatizo letu kubwa ni soko la uhakika la mazao yetu.
Kwenye hili la mbolea bado shida kubwa itakuwepo, nikikutana na bashe nitamueleza.

Serikali iweke ruzuku kwa mbolea yote Kama ilivyo kwenye mafuta, kila petrol station ukienda unakutana tayari na bei ya ruzuku kwa kuwa ilishawewa kabla mafuta hayajafika petrol station.

Kwenye mbolea kutumia baadhi ya mawakala itakua shida tu, kwa kuwa kwanza wauzaji sio wengi alafu haohao hapohapo uwape tena wachache mbolea za ruzuku wawauzie wakulima.

Kumonitor hili ni shida na hata hiyo ya ruzuku itauzwa kwa bei ya kawaida.
 
Mbolea ilitakiwa ikishawekewa ruzuku haina haja ya process za usajili.mbolea lazima inatumiwa na wakulima.hakuna shughuli mbadala.
Labda ni kuizuia mipakani tu is iendele nje ya mipaka yetu.
Iuzwe kama petrol na mafuta ya gari.
Kuratibu ni kuongeza gharama na pia kuweka ulaji usiositaili.
 
Ruzuku iwekwe kwenye mbolea yote kama ilivyokua kwa mafuta,usajili huu utaleta urasimu na wengine kupigwa kwenye bei
 
Rais alisisitiza wakulima wajotokeze kwa wingi kujiandikisha wapate ruzuku, kinyume na hapo wasiojiandikisha hawatapata ruzuku, sijui Bashe ametoa wapi haya maelezo yake.

Kama wote waliojiandikisha na wasiojiandikisha watapata ruzuku, sasa kwanini wapoteze fedha kutengeneza hivyo vitambulisho?
 
Ziara ya Rais Samia Suluh Hassan Mkoani Njombe, kijiji cha Mtwango.

Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe ametoa uhakika wa upatikanaji wa mbolea kwa bei ya ruzuku hata kwa wakulima ambao hawatakuwa wamesajiliwa baada ya muda huo kufika. Hii inatoa ahueni kwa wakulima waliokuwa na wasiwasi juu ya utaratibu huu mpya wa kujisajili ili kuwa mnufaika wa nafuu ya punguzo ya bei ya mbolea iliyotangazwa na serikali.

Waziri Bashe amewataka wakulima wote, hata wale wasiosajiliwa kufika kwa mawakala watakao orodheshwa hapo baadae ili kupata mbolea kwa bei ya ruzuku kwani serikali itaweka utaratibu wa kuwasajili hapohapo pasipo usumbufu. Katika kuhitimisha hotuba hii fupi, Rais amewaomba viongozi wa serikali kukusanya mapato vizuri kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa.​

Hata hivyo uzalishaji viwandani umerejea katika mwenendo wa kawaida baada ya Covid 19 kupita. Hivyo sina uhakika wa hiyo inayoitwa ruzuku maana naona ni hadaa ya kisiasa zaidi. Kila mtu anauziwa bila hata kujisajili maana bei ya mbolea imerejea kwenye bei zake za kawaida.
 
Ziara ya Rais Samia Suluh Hassan Mkoani Njombe, kijiji cha Mtwango.

Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe ametoa uhakika wa upatikanaji wa mbolea kwa bei ya ruzuku hata kwa wakulima ambao hawatakuwa wamesajiliwa baada ya muda huo kufika. Hii inatoa ahueni kwa wakulima waliokuwa na wasiwasi juu ya utaratibu huu mpya wa kujisajili ili kuwa mnufaika wa nafuu ya punguzo ya bei ya mbolea iliyotangazwa na serikali.

Waziri Bashe amewataka wakulima wote, hata wale wasiosajiliwa kufika kwa mawakala watakao orodheshwa hapo baadae ili kupata mbolea kwa bei ya ruzuku kwani serikali itaweka utaratibu wa kuwasajili hapohapo pasipo usumbufu. Katika kuhitimisha hotuba hii fupi, Rais amewaomba viongozi wa serikali kukusanya mapato vizuri kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa.​
Hongera Sana Mheshimiwa Dr
 
Wameweka bei ya mbolea kwa importer/dealer.lakini mtu wa kufikisha mbolea kwa mkulima kijijini ni maduka ya rejareja ya agrovet .sasa hakuna taarifa ya uhakika jinsi itakavyokuwa .agrovet watapata faida gani .tulikuwa twanunua Yara/ETG TUWAUZIA wakulima sasa kizungumkuti.
 
Back
Top Bottom