Bashe: Serikali itawalinda wakulima kwa gharama zote

Bashe: Serikali itawalinda wakulima kwa gharama zote

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
BASHE : SERIKALI ITAWALINDA WAKULIMA KWA GHARAMA ZOTE

Tanganyika, Katavi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe ameweka wazi msimamo wa serikali juu ya kuwalinda wakulima nchini kufuatia muingiliano wa kisekta wa mara kwa mara ambao husababisha wakulima kubeba mzigo mkubwa zaidi wa gharama za uzalishaji.

Naibu Waziri Bashe ameyasema hayo kufuatia taarifa ya wilaya ya Tanganyika juu ya Mamlaka ya Wanayapori nchini (TAWA) kuweka alama za mipaka Kwenye maeneo ya misitu ya Tongwe ambayo hapo awali maeneo hayo yalikuwa yamekwishagawiwa kwa wakulima wadogo na wawekezaji wa kilimo huku maamuzi ya kurasimisha maeneo hayo kwa TAWA yakiwa yamefanywa pasipo vikao kushirikisha wadau wa pande zote pamoja na halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Naibu Waziri Bashe amesema “Haiwezekani TAWA kutumia vibaya Mamlaka waliyinayo, waliwezaje kuingia na kuweka alama bila kushirikisha uongozi wa vijiji, kata au wilaya? Vitendo vya namna ni kumgombanisha Rais pamoja na wananchi ambao wamekwishakupatiwa mashamba Kwa ajili uwekezaji kwenye sekta ya kilimo”

Bashe ameongeza ya kuwa “Masuala ya namna hii yanahitaji mashauriano zaidi baina ya Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mali Asili na Utalii ili kuhakikisha tunalinda maslahi ya pande zote bila kuwapa mzigo wananchi ambao sehemu kubwa ya maisha yao wamekuwa wakitegemea kilimo”

Aidha Mhe. Bashe ameongeza ya kuwa “Kama taifa tumekuwa na mipango ya kuwa na maeneo ya viwanda, maeneo ya wanyamapori, na maeneo ya usafirishaji lakini hakuna Mpango wa kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo. Kwa dunia ya sasa ili kila jambo lifanikiwe lazima liwekewe utararibu rasmi ambao utatoa mwanga Kwa wawekezaji na taifa Kwa ujumla”

Katika kuhitimisha ziara yake kwenye wilaya hiyo ya Tanganyika, Mhe. Bashe ameitaka kutenga eneo la ekari 1,000 kwa ajili ya Kilimo cha mbegu kufuatia mkoa wa Katavi kuwa kitovu cha uzalishaji wa mbegu ambapo watafiti wa Taasisi za TARI na ASA wamepewa jukumu la kufanikisha zoezi hilo Kwa haraka ili kufikia malengo ya kitaifa kwenye uzalishaji na upatikanaji wa mbegu nchini.

#SamiaKaziIendele
#KilimoTanzania

IMG-20211004-WA0300.jpg

IMG-20211004-WA0301.jpg

IMG-20211004-WA0299.jpg
 
Wakati mahindi yanakosa wanunuzi wakati mjini watu wanakosa chakula alikuwa yupo break time au ? Au hakupewa Memo ?

Serikali inachojua ni kuwakata wakulima wasiuze nje iwapo kuna njaa (scarcity) na kuwasahau iwapo kuna excess
 
Hawa Tawa ni watu hatari saana kwa Taifa letu,sio huko tu hata kijiji cha nyatwali bunda hao jamaa wanadai ardhi eti ni yao,wanakwamisha wawekezaji katika sector ya utalii,serikali iwaamgalie saana hawa jamaa aisee TAWA imekua TAWA.
 
Kwa hili la TAWA kujimilikisha eneo la Msitu wa hifadhi wa Tongwe West na East, ambayo tayari inamilikiwa na Halmashauri ya Tanganyika na maeneo mengine, tena bila kuwashirikisha, kiukweli ni kumshauri vibaya rais na kumgombanisha na wananchi na mamlaka nyingine.

Mimi najiuliza ikiwa Tanzania maeneo yenye misitu ni zaidi ya hekta milioni 48 ambapo, kati ya hayo ambayo yamehifadhiwa kisheria ni chini ya asilimia 30 ni kwa nini TAWA wasipeleke nguvu zao kwenye hayo maeneo ambayo hayajahifadhiwa badala ya kupora ya wenzao ambayo wanayamiliki?
 
Aende Mabibo aone Madalali wanavyowapiga Wakulima
 
BASHE : SERIKALI ITAWALINDA WAKULIMA KWA GHARAMA ZOTE

Tanganyika, Katavi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe ameweka wazi msimamo wa serikali juu ya kuwalinda wakulima nchini kufuatia muingiliano wa kisekta wa mara kwa mara ambao husababisha wakulima kubeba mzigo mkubwa zaidi wa gharama za uzalishaji.

Naibu Waziri Bashe ameyasema hayo kufuatia taarifa ya wilaya ya Tanganyika juu ya Mamlaka ya Wanayapori nchini (TAWA) kuweka alama za mipaka Kwenye maeneo ya misitu ya Tongwe ambayo hapo awali maeneo hayo yalikuwa yamekwishagawiwa kwa wakulima wadogo na wawekezaji wa kilimo huku maamuzi ya kurasimisha maeneo hayo kwa TAWA yakiwa yamefanywa pasipo vikao kushirikisha wadau wa pande zote pamoja na halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Naibu Waziri Bashe amesema “Haiwezekani TAWA kutumia vibaya Mamlaka waliyinayo, waliwezaje kuingia na kuweka alama bila kushirikisha uongozi wa vijiji, kata au wilaya? Vitendo vya namna ni kumgombanisha Rais pamoja na wananchi ambao wamekwishakupatiwa mashamba Kwa ajili uwekezaji kwenye sekta ya kilimo”

Bashe ameongeza ya kuwa “Masuala ya namna hii yanahitaji mashauriano zaidi baina ya Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mali Asili na Utalii ili kuhakikisha tunalinda maslahi ya pande zote bila kuwapa mzigo wananchi ambao sehemu kubwa ya maisha yao wamekuwa wakitegemea kilimo”

Aidha Mhe. Bashe ameongeza ya kuwa “Kama taifa tumekuwa na mipango ya kuwa na maeneo ya viwanda, maeneo ya wanyamapori, na maeneo ya usafirishaji lakini hakuna Mpango wa kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo. Kwa dunia ya sasa ili kila jambo lifanikiwe lazima liwekewe utararibu rasmi ambao utatoa mwanga Kwa wawekezaji na taifa Kwa ujumla”

Katika kuhitimisha ziara yake kwenye wilaya hiyo ya Tanganyika, Mhe. Bashe ameitaka kutenga eneo la ekari 1,000 kwa ajili ya Kilimo cha mbegu kufuatia mkoa wa Katavi kuwa kitovu cha uzalishaji wa mbegu ambapo watafiti wa Taasisi za TARI na ASA wamepewa jukumu la kufanikisha zoezi hilo Kwa haraka ili kufikia malengo ya kitaifa kwenye uzalishaji na upatikanaji wa mbegu nchini.

#SamiaKaziIendele
#KilimoTanzania

View attachment 1962748
View attachment 1962749
View attachment 1962750
Heading hiyo siyo kweli. Sio mkulima bali anakandamizwa huku serikali ikiwalinda mabwanyenye yenye mitaji katika kilimo inayopata kupitia mkulima wa kitanzania ambaye kuchwakutwa halindwi na haendelei

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Huyu anapelekewa moto mahindi tunauza elfu 5 mbolea tunanunua 110,000!!!!
 
Hivi bashe yupo humu nna shida na mawasiliano nae
 
Ni awamu ya Kwanza tu ya Uongozi wa nchi hii ndiyo iliyowalinda wakulima kwa nguvu zote.

Hizi awamu nyingine ni stories tu za kujipendekeza!
 
Back
Top Bottom