Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali, wakiwemo Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, pamoja na Wajumbe wa Bodi ya EITI kutoka mataifa mbalimbali duniani, wakiwemo wawakilishi wa kampuni kubwa zinazojihusisha na uchimbaji na utafutaji wa rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia, pamoja na asasi za kiraia.
"Nimshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha Tanzania ni moja ya nchi wanachama wa EITI zinazotekeleza masuala ya uwazi wa mapato yanayolipwa na kampuni zinazofanya shughuli katika sekta ya madini, mafuta na gesi asilia," amesema Bashungwa.
Aidha, Bashungwa ametumia fursa hiyo kuwahakikishia Watanzania, wawekezaji, na wageni kutoka nje ya nchi kuwa Tanzania ni nchi yenye amani, utulivu zikiwemo fursa nyingi, na ni mahali sahihi kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali, ikiwemo sekta ya utalii.
Naye, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema kuwa kufanyika kwa mkutano huo wa kimataifa ni kielelezo cha kazi nzuri zinazofanyika chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia, ambazo zimevutia mikutano mingi ya aina hii kufanyika nchini.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Shughuli za TEITI, CPA Ludovick Utouh, ameeleza kuwa mkutano huo wa Bodi ya Wakurugenzi wa Uwazi na Uwajibikaji katika Sekta ya Uziduaji Kimataifa (EITI) unahusisha wanachama 57 kutoka mataifa mbalimbali duniani.