Bashungwa: Serikali inatakeleza Mradi wa kununua magari 150 ya Zimamoto na kuyasambaza Nchini

Bashungwa: Serikali inatakeleza Mradi wa kununua magari 150 ya Zimamoto na kuyasambaza Nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Serikali inaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kulipatia vitendea kazi ambapo sasa inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji.

Bashungwa ameeleza hayo tarehe 03 Februari 2025 wakati akijibu swali la Mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel Shangai aliyetaka kujua Je, lini Serikali itanunua gari la Zimamoto Wilaya ya Ngorongoro.

“Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji” amesema Bashungwa

Amesema pindi magari 150 ya kuzima moto na uokoaji yatakapofika nchini, yatakayosambazwa nchi nzima ikiwemo Wilaya ya Ngorongoro.
WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.32_e65dc1aa.jpg
Aidha, amesema Serikali inayoonzwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeshaliwezesha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kununua magari 12 ya kisasa ambapo moja wapo lilitumiaka kuzima moto katika jengo gorofa la TRA Kariakoo.

Bashungwa amesema Serikali ipo mbioni kununua helikopta moja maalum kwa ajili ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambayo yataenda sambamba na kuwapatia Mafunzo Maafisa, Wakaguzi na Askari wa Jeshi hilo.

Soma, Pia: Bunge la 12 Mkutano wa 18 Kikao cha Tano, Februari 3, 2025 asubuhi
 
Magari ya zimamoto nunueni nyumbu Kibaha wanatengeneza kwa bei nafuu kwa nini mkanunue nje ????
 
Kipaumbele cha hii serikali ni ku-make headlines tu!
 
He cannot be serious 150 fire engines kwa nchi nzima
 
Ni pesa mingi saana yaani ! Nasisitiza wakanunue kiwanda cha nyumbu Kibaha wanatengeneza magari ya Fire kwa bei nafuu sana.
 
RIP MAGU ulizuia ununuzi wa drone za kuzimia moto sasa wanataka helicopter kabisa
 

MAGARI 150 YA ZIMAMOTO YANUNULIWA NA KUSAMBAZWA NCHI NZIMA: BASHUGWA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Serikali inaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kulipatia vitendea kazi ambapo sasa inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji.

Bashungwa ameeleza hayo tarehe 03 Februari 2025 wakati akijibu swali la Mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel Shangai aliyetaka kujua Je, lini Serikali itanunua gari la Zimamoto Wilaya ya Ngorongoro.

“Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji” amesema Bashungwa

Amesema pindi magari 150 ya kuzima moto na uokoaji yatakapofika nchini, yatakayosambazwa nchi nzima ikiwemo Wilaya ya Ngorongoro.

Aidha, amesema Serikali inayoonzwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeshaliwezesha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kununua magari 12 ya kisasa ambapo moja wapo lilitumiaka kuzima moto katika jengo gorofa la TRA Kariakoo.

Bashungwa amesema Serikali ipo mbioni kununua helikopta moja maalum kwa ajili ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambayo yataenda sambamba na kuwapatia Mafunzo Maafisa, Wakaguzi na Askari wa Jeshi hilo.
 

Attachments

  • UNUNUZI WA MAGARI 150 YA ZIMAMOTO.MP4
    67.4 MB
  • WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.28.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.28.jpeg
    358 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.30.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.30.jpeg
    499 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.31.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.31.jpeg
    507.1 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.32.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-03 at 11.46.32.jpeg
    509.6 KB · Views: 2
Mahitaji ni kiasi gani na sisi tumenunua kiasi gani? Hapo ndio tunaweza kupima.
 
Tanbihi :
Uki comment chochote nje ya kumuunga mkono Bashungwa kwenye hili imekula kwako.....
 
Back
Top Bottom